Anayedaiwa kukamatwa na polisi mwili wake wakutwa ukielea ziwani

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
20,570
25,091
Habari hii nimeisikia asubuhi hii kupitia RFA magazeti, mwenye taarifa atujuze ni nani ukizingatia kuna yule mwandishi wa kanda ya ziwa anayedaiwa kuandika sakata la mkuu wa mkoa kukamatwa na polisi akiwa Musoma.

========
Jeshi la polisi mkoani Kagera linaendelea kufanya uchunguzi wa kifo cha kijana Lucas Baraka (20), mkazi wa kisiwa cha Goziba wilayani Muleba mkoani Kagera aliyekuwa anafanya kazi ya kupakua dagaa kwenye mitumbwi baada ya mwili wake kukutwa unaelea katika Ziwa Victoria.

Kaimu Kamanda wa Jeshi wa polisi Kagera, Yusuph Daniel amethibitisha tukio hilo kutokea, ambapo mwili wa kijana huyo ulikutwa unaelea Juni 12 majira ya saa saba mchana na wavuvi waliofika eneo hilo kwaajili ya shughuli zao za uvuvi wa Samaki.

Kamanda Yusuph amesema uchunguzi unaendelea wa kubaini nini kimesababisha kifo cha kijana huyo na kuwatoa hofu baadhi ya wananchi wanaoamini kuwa kijana huyo kauliwa kuwa Jeshi la Polisi litahakikisha wale wote waliohusika bila kujali kama ni mtumishi wa Jeshi la Polisi au la watachukuliwa hatua stahiki endapo watathibitika kufanya mauaji hayo, na kuwaomba wananchi wawe watulivu wakati uchunguzi unaendelea.

 
Kuna watu wao kwenda Mbinguni hawataki kabisaaa...

Unatoaje roho ya mtu? Unamdhulumu maisha yake, Unampiga mtu risasi unamkata mapanga anavyolia wewe husikii hata huruma! Kuna watu ni makatilii wana laana
 
Habari hii nimeisikia asubuhi hii kupitia RFA magazeti, mwenye taarifa atujuze ni nani ukizingatia kuna yule mwandishi wa kanda ya ziwa anayedaiwa kuandika sakata la mkuu wa mkoa kukamatwa na polisi akiwa Musoma.
Kusanya taarifa kamili ndio ukimbilie kupost
 
Hata wewe kusanya,kwani umeshaandaa mtu wa kuwa anakukusanyia taarifa wewe unakuja kusoma tu?
Rejea nilichokiandika sasa utakuta tunachokikadili.
Gazeti Mwananchi leo Jumapili.
 

Attachments

  • IMG-20240615-WA0059-1.jpg
    IMG-20240615-WA0059-1.jpg
    113.8 KB · Views: 2
Kuna watu wao kwenda Mbinguni hawataki kabisaaa...

Unatoaje roho ya mtu? Unamdhulumu maisha yake, Unampiga mtu risasi unamkata mapanga anavyolia wewe husikii hata huruma! Kuna watu ni makatilii wana laana
Kabisa kuna watu ni makatili vibaya na tunaishia nao kitaa,Ila huwez mjua ukichanganya umeisha halaf unaandikiwa R.I.P(Return if possible)
 
Back
Top Bottom