Amalizie kujenga au anunue gari

High Vampire

JF-Expert Member
Nov 17, 2012
2,915
2,134
Kuna jamaa yangu amejenga kanyumba kadogo kakuanzia maisha sasa anataka kununua gari ili imsaidie kutoka kwake na kurudi lakini ana boma tena kubwa la nyumba anataka aliache kwanza anunue sasa yuko njia panda amalizie kuliezeka au anunue gari
 
Kama ana sehemu ya kulala na room extra na hajaanza kuwa na familia kubwa anaweza kununua kagari ila aendelee kuwekeza kidogo kidogo kwenye nyumba.
 
Kuna mambo mengi sana hapo ya kuyaangalia kabla ya kufanya maamuzi, kwanza hongera zake kwa kujikwamua na fedheha za kupanga.
Pili, kama ameweza kuvumilia kadhia za usafiri hadi sasa hivi hadi amehamia kwenye nyumba yake ndogo sio mbaya akiendelea kuvumilia ili aezeke nyumba kubwa. Kama nyumba ipo maeneo mazuri, akiiezeka anaweza kuipangisha ikawa kama kitega uchumi ikaingiza pesa ambazo baade taratibu atanunua gari huku nyumba ikiwa imeezekwa.

Gari ukishalinunua lina gharama zake za matunzo, mafuta, service n.k hapo hatujaongelea mambo ya ajali, Mungu aepushie mbali.
Bora angeezeka nyumba kwanza kisha mambo ya gari yafuatie baadae.
 
asante sana japo anaona watu wanaendesha magari anatamani sana kuwa na gari na gari ni ghalama sana
 
asante sana japo anaona watu wanaendesha magari anatamani sana kuwa na gari na gari ni ghalama sana

Najua jinsi gani inahitaji moyo kujikana wakati uwezo unao, ila sio kila mara tunapata vitu vyote. Nnauhakika hatajutia kuezeka nyumba kwanza, vinginevyo kama kuna ulazima sana usioweza kusubiri wa kuwa na usafiri. Nimeona watu wakiuza magari kufanikisha ujenzi, ila kwa kuwa yeye tayari ana pa kujisitiri, amaweza kuamua kuvuta usafiri japo haitaleta faida sana kama akiezeka nyumba kwamnza.
 
Anunue gari mkuu loh! Kwani nani anapenda kushika bomba?teh! Kama anakaa kwake halipi pango yanini kujitesa?raha jipe mwenyewee ! Ujenzi upo tu ili mradi awe anawekeza aendeleze mjengo huo!
 
malizia nyumba gari utanunua tu kila siku yanatengenezwa magari ya design tofauti.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…