Aliyeidanganya EFF ya Afrika ya Kusini ndiye anayeidanganya ACT Wazalendo ya Tanzania?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,890
35,179
Julius Malema wakati wa harakati zake za kisiasa na wakati wa Kampeni za mwaka huu, alijiegemeza Sana kwenye kukishambulia chama cha siasa cha pili kwa ukubwa nchini Afrika ya Kusini.

Malema alikuwa anaonesha kuwa tatizo la Afrika ya kusini ni "wazungu" wanaobebwa na ANC kuwepo kwake madarakani.

Akajenga hoja kuwa ili Afrika ya Kusini ikombolewe kiuchumi na kijamii, ni lazima kwanza ANC itoke madarakani ili chama chake cha Economic Freedom Fighters (EFF) kiweze kupambana na wazungu kikiwa madarakani.

Ghafla aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma, akaunda chama na kukipa jina la uMkhonto we Sizwe (MK) ambacho kina mfanano kifalsafa na kisera na ANC isipokuwa kwenye sera ya utaifishaji migodi ya dhahabu na Platinum.

EFF ikapoteza uungwaji mkono na MK ikachukua zaidi ya Viti 58 huku Democratic Alliance (DA) iliyokuwa inapigwa vita na EFF ikijiongezea Viti 5 na EFF yenyewe ikipoteza Viti 5 vya ubunge.

Leo hii DA iliyokuwa inashambuliwa na EFF ndiyo Iko kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuunda serikali ya mseto na ANC kuliko ilivyo Kwa EFF ya Julius Malema.

Hapa Tanzania ACT wako bize kupambana na CHADEMA badala ya kujijenga yenyewe. Mwisho wa siku CHADEMA ama itaongoza nchi au itakuwa chama kikuu Cha upinzani wakati huo ACT itakuwa haina nguvu za kisiasa Zanzibar.
 
Julius Malema wakati wa harakati zake za kisiasa na wakati wa Kampeni za mwaka huu, alijiegemeza Sana kwenye kukishambulia chama cha siasa cha pili kwa ukubwa nchini Afrika ya Kusini...
Zitto ni mmojawapo wa wanasiasa niliokuwa nawaona wako makini sana nchi hii, sijui nani alimdanganya kujianzishia hicho kijiwe cha ACT, chama kipo Zanzibar tu halafu mafaniko makubwa wanayojisifia nayo ni kumiliki ofisi na kuchambua sera!
 
Ni kweli. Japo haina afya sana kwa chama cha upinzani kuunda serikali ya mseto na chama tawala.

Kwasabb hapa Afrika vyama vyote vya upinzani vinavyoingia kwenye serikali ya mseto na chama tawala huwa vinasambratika baadaye.

Fuatiia chama cha Morgan Nchangarai (rip) pale Zimbabwe.

Fuatlia CUF pale Zanzibar na hata Kenya ile miungano yao bandia huuwa inafutika.
 
Julius Malema wakati wa harakati zake za kisiasa na wakati wa Kampeni za mwaka huu, alijiegemeza Sana kwenye kukishambulia chama cha siasa cha pili kwa ukubwa nchini Afrika ya Kusini.

Malema alikuwa anaonesha kuwa tatizo la Afrika ya kusini ni "wazungu" wanaobebwa na ANC kuwepo kwake madarakani.

Akajenga hoja kuwa ili Afrika ya Kusini ikombolewe kiuchumi na kijamii, ni lazima kwanza ANC itoke madarakani ili chama chake cha Economic Freedom Fighters (EFF) kiweze kupambana na wazungu kikiwa madarakani.

Ghafla aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma, akaunda chama na kukipa jina la uMkhonto we Sizwe (MK) ambacho kina mfanano kifalsafa na kisera na ANC isipokuwa kwenye sera ya utaifishaji migodi ya dhahabu na Platinum.

EFF ikapoteza uungwaji mkono na MK ikachukua zaidi ya Viti 58 huku Democratic Alliance (DA) iliyokuwa inapigwa vita na EFF ikijiongezea Viti 5 na EFF yenyewe ikipoteza Viti 5 vya ubunge.

Leo hii DA iliyokuwa inashambuliwa na EFF ndiyo Iko kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuunda serikali ya mseto na ANC kuliko ilivyo Kwa EFF ya Julius Malema.

Hapa Tanzania ACT wako bize kupambana na CHADEMA badala ya kujijenga yenyewe. Mwisho wa siku CHADEMA ama itaongoza nchi au itakuwa chama kikuu Cha upinzani wakati huo ACT itakuwa haina nguvu za kisiasa Zanzibar.
😆😆😆😆
 
Lengo na madhumuni ya ACT wazalendo ni kuhakikisha inaififisha CDM na huo mchongo unatoka serikalini, na ndio maana utaona wanauma na kupuliza, ila nayo ACT itakufa tu kama CUF
 
Julius Malema wakati wa harakati zake za kisiasa na wakati wa Kampeni za mwaka huu, alijiegemeza Sana kwenye kukishambulia chama cha siasa cha pili kwa ukubwa nchini Afrika ya Kusini.

Malema alikuwa anaonesha kuwa tatizo la Afrika ya kusini ni "wazungu" wanaobebwa na ANC kuwepo kwake madarakani.

Akajenga hoja kuwa ili Afrika ya Kusini ikombolewe kiuchumi na kijamii, ni lazima kwanza ANC itoke madarakani ili chama chake cha Economic Freedom Fighters (EFF) kiweze kupambana na wazungu kikiwa madarakani.

Ghafla aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma, akaunda chama na kukipa jina la uMkhonto we Sizwe (MK) ambacho kina mfanano kifalsafa na kisera na ANC isipokuwa kwenye sera ya utaifishaji migodi ya dhahabu na Platinum.

EFF ikapoteza uungwaji mkono na MK ikachukua zaidi ya Viti 58 huku Democratic Alliance (DA) iliyokuwa inapigwa vita na EFF ikijiongezea Viti 5 na EFF yenyewe ikipoteza Viti 5 vya ubunge.

Leo hii DA iliyokuwa inashambuliwa na EFF ndiyo Iko kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuunda serikali ya mseto na ANC kuliko ilivyo Kwa EFF ya Julius Malema.

Hapa Tanzania ACT wako bize kupambana na CHADEMA badala ya kujijenga yenyewe. Mwisho wa siku CHADEMA ama itaongoza nchi au itakuwa chama kikuu Cha upinzani wakati huo ACT itakuwa haina nguvu za kisiasa Zanzibar.
Scenario ya Africa Kusini haiwezi kuwepo Tanzania kwa sababu:
Africa kusini ina vyama vingi vikuu vikiwa vinne vyenye sera tofauti wakati Tanzania kuna vyama viwili tu CCM na CHADEMA. ACT na vingine ni vibaraka wa CCM ( alias CCM B) Hivyo hata wananchi wakihadaika wakavipa kura hivyo CCM B itakuwa rahisi sana CCM kuunda serikali kwa sababu vitapewa maelekezo nini cha kufanya.

Fikiria vyama ambavyo huwezi kuvisikia vikuzungumzia issues hadi CHADEMA walumbane na CCM au serikali ndipo huibuka kwa pamoja mbele ya waandishi wa habari na mmoja wa wenyeviti wa hivyo vyama husoma tamko wanaloliita la pamoja la vyama ambalo huwa limeeandaliwa na CCN au serikali na wao kupewa kusoma tu tamko ambalo huwa linashambulia CHADEMA.
 
Tokea Malema na EFF waanze kutetea ushoga niliwaona hawana maana.
Vyama vyote vikubwa Africa Kusini vinaheshimu haki za mashoga na ndoa za jinsia moja zilipitishwa na utawala wa ANC chini ya Thabo Mbeki.
Pia Africa Kusini ushoga sio kipaumbele kwao ni jambo petty mno kuliko uhalifu, rushwa, matatizo ya umeme na ukosefu wa ajira.
 
Back
Top Bottom