Aibu gani uliipata kwenye gari kwa mara ya kwanza?

Living Pablo

JF-Expert Member
May 17, 2020
3,498
10,881
Mkiazima magari ya watu waulizeni kwanza wahusika msije mkatia aibu mtaani

Kuna mwenzenu huku kaazima Mercedes kwa ajili ya safari kwa mara ya kwanza, usiku ulipoingia alishindwa kufahamu wapi pa kuwashia taa hivyo akaamua ashikilie flashing light lever ( HIZO KWENYE MSHALE PICHANI ) mpaka mwisho wa safari

Na mwingine alipewa Volkswagen Golf akashindwa kupiga reverse, akadanganya watu gari betri limekufa ili wamsaidie kusukuma ili apark

Kuna jamaa alivyopewa Toyota Aqua akashangaa haiungurumi kumbe ni hybrid


Nimeitoa Facebook

Binafsi mimi kwa upande wangu mara ya kwanza niliendesha Townace niliikuta imepakiwa na bro nikaweka D then nikaendesha kimbembe nikawa nahangaika kutoa funguo bila kuzima gari, nikajikuta naweka N gari inatembea nilichanganyikiwa sana maana gari ilikuwa inaenda mtaroni nikakanyaga brake tu alaf nikamuita bro ikabidi awahi kuja kuizima.

JE WEWE ULIVYO PEWA GARI KWA MARA YA KWANZA KIPI KILIKUTOKEA EMBU TUJUZE ??
 
Mwandishi wa global amefanya nini mkuu?
Alikua wa kike anaongea hajui anacho ripoti mkuu ukiingia instagram kwenye account yao utaikuta habari
Wameandika hivi nahisi(gari ya ambulance imepata ajali mwenge) utasikia kinachoongeleka ingawa sijajua kama ni global wenyewe au global tofauti yani watu tu walio jiamulia kujifungulia account ya au inayo fanana na global!!!

Kwa faida tu jamaa wamekubali kosa alilofanya dereva wao na Alhamudullillah niko poa na gari yetu wanaitengeneza.
 
Niliendesha Land Cruiser 250 series ikiwa inapiga hazard lights kwanzia Makuyuni hadi Arusha mjini alafu kibati mbaya.

Ila haikua ushamba ni haraka nikakosa muda wa kutafuta ile triangle nikaizimia mjini baada ya kutafuta kwa dakika 10
 
Mala ya kwanza nimetoka kuchukua gari sikuwa najua hata ku drive asee,wakati namsubiri dereva maana tulikuwa sehemu tofauti kuwasha gari mzee huwa taa zinawaka kisha zinapotea zile za ishara mbalimbali sasa ikabaki ya Handbrake nikaanza kumpigia simu mshikaji wangu akaniambia mbona hiyo ni handbrake light dah nilijiona fala kinoma😀.

Na kabla ya hapo mshikaji wangu nae ilimtoa ushamba yeye kashazoea gari zile manual na zile za kutumia funguo sasa amekaa kwenye usukani kuwasha bhana kumbe push to start inataka ukanyage brake kisha una push start button inawaka yeye nae ikamtoa ushamba akabaki anahangaika hadi tulipomcheck Clearing agent aliyenitolea gari akamuelekeza😀.
 
Back
Top Bottom