Afanya sherehe ya harusi bila Bibi Harusi, baada ya kikeni kuzingua dakika za jioni

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
51,027
111,005
Katika hali isiyo ya kawaida katika Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi, Edward Futakamba Mkazi wa Kata ya Nsemulwa amewashangaza wengi baada ya kufanya sherehe ya harusi licha ya Bibi harusi kugoma kufunga ndoa hiyo.

Edward aliyekuwa akiishi na Mwanamke aitwaye Marry na kufanikiwa kupata Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka mitatu ambapo baadae waliamua kwa pamoja kufunga ndoa na taratibu zikaendelea ikiwemo kutoa mahari ya shilingi 1,200,000/- na maandalizi ya harusi kufanyika ili ndoa ifungwe July 26 mwaka huu.

Kwa mujibu wa Katibu wa Kamati ya harusi hiyo Simon Moshi amesema siku nne kabla ya tarehe hiyo walipata taarifa kuwa upande wa Bibi harusi wameweka pingamizi kanisani la kuzuia ndoa hiyo “Tulijaribu kuwatafuta kuongea nao ili angalau hili suala liende kama lilivyokuwa lakini ikashindikana, tukaona haiwezekani Watu wametoa mchango yao alafu hili suala likatishwe”

“Sababu ambayo sisi tuliambiwa kama kamati walisema kwamba kwanza bwanaharusi alikuja amechangamka kwenye send off na wakasema kwamba kuna laki mbili haijamalizwa ya mahari”amesema Katibu wa Kamati ya harusi.

“Kupata na kukosa yote ni sehemu ya maisha, cha msingi sana ikiwa kama Mtu unaweza kusherehekea na kufurahia ukipata basi ni vizuri pia hata ukikosa pia usherehekee na kufurahia kwa sababu mpango wa Mungu yeye ndio anayejua” amesema Edward Futakamba.
 
Katika hali isiyo ya kawaida katika Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi, Edward Futakamba Mkazi wa Kata ya Nsemulwa amewashangaza wengi baada ya kufanya sherehe ya harusi licha ya Bibi harusi kugoma kufunga ndoa hiyo.

Edward aliyekuwa akiishi na Mwanamke aitwaye Marry na kufanikiwa kupata Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka mitatu ambapo baadae waliamua kwa pamoja kufunga ndoa na taratibu zikaendelea ikiwemo kutoa mahari ya shilingi 1,200,000/- na maandalizi ya harusi kufanyika ili ndoa ifungwe July 26 mwaka huu.

Kwa mujibu wa Katibu wa Kamati ya harusi hiyo Simon Moshi amesema siku nne kabla ya tarehe hiyo walipata taarifa kuwa upande wa Bibi harusi wameweka pingamizi kanisani la kuzuia ndoa hiyo “Tulijaribu kuwatafuta kuongea nao ili angalau hili suala liende kama lilivyokuwa lakini ikashindikana, tukaona haiwezekani Watu wametoa mchango yao alafu hili suala likatishwe”

“Sababu ambayo sisi tuliambiwa kama kamati walisema kwamba kwanza bwanaharusi alikuja amechangamka kwenye send off na wakasema kwamba kuna laki mbili haijamalizwa ya mahari”amesema Katibu wa Kamati ya harusi.

“Kupata na kukosa yote ni sehemu ya maisha, cha msingi sana ikiwa kama Mtu unaweza kusherehekea na kufurahia ukipata basi ni vizuri pia hata ukikosa pia usherehekee na kufurahia kwa sababu mpango wa Mungu yeye ndio anayejua” amesema Edward Futakamba.
Sasa sendoff ya nini wakati watu walikuwa wanaishi na wamezaa au hao hawajui maana ya sendoff?
 
Katika hali isiyo ya kawaida katika Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi, Edward Futakamba Mkazi wa Kata ya Nsemulwa amewashangaza wengi baada ya kufanya sherehe ya harusi licha ya Bibi harusi kugoma kufunga ndoa hiyo.

Edward aliyekuwa akiishi na Mwanamke aitwaye Marry na kufanikiwa kupata Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka mitatu ambapo baadae waliamua kwa pamoja kufunga ndoa na taratibu zikaendelea ikiwemo kutoa mahari ya shilingi 1,200,000/- na maandalizi ya harusi kufanyika ili ndoa ifungwe July 26 mwaka huu.

Kwa mujibu wa Katibu wa Kamati ya harusi hiyo Simon Moshi amesema siku nne kabla ya tarehe hiyo walipata taarifa kuwa upande wa Bibi harusi wameweka pingamizi kanisani la kuzuia ndoa hiyo “Tulijaribu kuwatafuta kuongea nao ili angalau hili suala liende kama lilivyokuwa lakini ikashindikana, tukaona haiwezekani Watu wametoa mchango yao alafu hili suala likatishwe”

“Sababu ambayo sisi tuliambiwa kama kamati walisema kwamba kwanza bwanaharusi alikuja amechangamka kwenye send off na wakasema kwamba kuna laki mbili haijamalizwa ya mahari”amesema Katibu wa Kamati ya harusi.

“Kupata na kukosa yote ni sehemu ya maisha, cha msingi sana ikiwa kama Mtu unaweza kusherehekea na kufurahia ukipata basi ni vizuri pia hata ukikosa pia usherehekee na kufurahia kwa sababu mpango wa Mungu yeye ndio anayejua” amesema Edward Futakamba.

Watu wengine bana ni wapumbavu sana hapo wameona kama vile wamemkomoa bwana harusi

Alafu kesho na kesho kutwa anakuja kuoa mwanamke mwingine anapata nao watoto

Alafu siku mshikaji akija kufa ndo unakuja kusikia wale wapumbavu wamejitokeza kudai mali
 
wamemponza mtoto wao kwa upumbavu wao sasa wako wanajuta

kesho jamaa anaona mwingine wao wabaki na singo mama
 
Back
Top Bottom