Achoma nyumba moto na kumuua Baba yake wa Kambo kwa kumpasua kichwa kwa jembe

Kipis

JF-Expert Member
Jul 23, 2011
494
69
Katika hali isiyo ya kawaida, kijana mmoja kwa jina la Mussa shebe mkazi wa kijiji cha Nachiungo kilichopo mkoani Lindi wilaya ya Ruangwa, anatafutwa na polisi kwa kosa la mauaji.

Kwa mujibu wa majirani, kijana huyo alikuwa na mgogoro na wazazi wake kwa siku za nyuma hali iliyopelekea kwa siku ya jana kuamua kutekeleza uhalifu huo.

Aidha siku ya tukio ambayo ilikuwa Jana majira ya saa sita usiku, kijana huyo alitoka nyumbani kwake kuelekea sehemu ya tukio, na baada ya kufika moja kwa moja aliufunga mlango kwa nje, na kuanza kuwasha moto na hatimae nyumba kuanza kushika Moto.

Katika hali ya kutaka kujinasua wazazi wa kijana huyo, walifanikiwa kuvunja mlango na kutoka nje hali iliyopelekea kushambuliwa kirahisi kwa Baba wa kijana huyo kwa kupigwa na jembe kichwani na kisha baada ya kutekeleza shambulio hilo alitokomea kusikojulikana.

Katika kuokoa maisha ya majeruhi huyo, alikimbizwa haspitali ya wilaya ya Ruangwa lakini majeruhi Alifia njiani.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa madakitari, marehemu amepasuliwa fuvu kutokana na shambulio hilo hali iliyopelekea damu kuvujia kwenye ubongo na hatimae kufariki dunia.

Update
Mshukiwa wa mauaji tayari ametiwa mbaroni siku ya jana jioni katika kijiji cha Nangurugai yupo chini ya ulinzi wa ofisi ya mtendaji, huku kukisubiriwa mamlaka zingine kwa hatua zaidi.

Hatua hiyo ilifikiwa mara tu baada ya mwili wa marehemu kupumzishwa hapo jana kwenye makazi yake ya milele.
 
Katika hali isiyo ya kawaida, kijana mmoja kwa jina la Mussa shebe mkazi wa kijiji cha Nachiungo kilichopo mkoani Lindi wilaya ya Ruangwa, anatafutwa na polisi kwa kosa la mauaji.

Kwa mujibu wa majirani, kijana huyo alikuwa na mgogoro na wazazi wake kwa siku za nyuma hali iliyopelekea kwa siku ya jana kuamua kutekeleza uhalifu huo.

Aidha siku ya tukio ambayo ilikuwa Jana majira ya saa sita usiku, kijana huyo alitoka nyumbani kwake kuelekea sehemu ya tukio, na baada ya kufika moja kwa moja aliufunga mlango kwa nje, na kuanza kuwasha moto na hatimae nyumba kuanza kushika Moto.

Katika hali ya kutaka kujinasua wazazi wa kijana huyo, walifanikiwa kuvunja mlango na kutoka nje hali iliyopelekea kushambuliwa kirahisi kwa Baba wa kijana huyo kwa kupigwa na jembe kichwani na kisha baada ya kutekeleza shambulio hilo alitokomea kusikojulikana.

Katika kuokoa maisha ya majeruhi huyo, alikimbizwa haspitali ya wilaya ya Ruangwa lakini majeruhi Alifia njiani.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa madakitari, marehemu amepasuliwa fuvu kutokana na shambulio hilo hali iliyopelekea damu kuvujia kwenye ubongo na hatimae kufariki dunia.
Aisee
 
Katika hali isiyo ya kawaida, kijana mmoja kwa jina la Mussa shebe mkazi wa kijiji cha Nachiungo kilichopo mkoani Lindi wilaya ya Ruangwa, anatafutwa na polisi kwa kosa la mauaji.

Kwa mujibu wa majirani, kijana huyo alikuwa na mgogoro na wazazi wake kwa siku za nyuma hali iliyopelekea kwa siku ya jana kuamua kutekeleza uhalifu huo.

Aidha siku ya tukio ambayo ilikuwa Jana majira ya saa sita usiku, kijana huyo alitoka nyumbani kwake kuelekea sehemu ya tukio, na baada ya kufika moja kwa moja aliufunga mlango kwa nje, na kuanza kuwasha moto na hatimae nyumba kuanza kushika Moto.

Katika hali ya kutaka kujinasua wazazi wa kijana huyo, walifanikiwa kuvunja mlango na kutoka nje hali iliyopelekea kushambuliwa kirahisi kwa Baba wa kijana huyo kwa kupigwa na jembe kichwani na kisha baada ya kutekeleza shambulio hilo alitokomea kusikojulikana.

Katika kuokoa maisha ya majeruhi huyo, alikimbizwa haspitali ya wilaya ya Ruangwa lakini majeruhi Alifia njiani.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa madakitari, marehemu amepasuliwa fuvu kutokana na shambulio hilo hali iliyopelekea damu kuvujia kwenye ubongo na hatimae kufariki dunia.
Hatari,baba wa watu kamlea kaambulia kuuwawa!
 
Back
Top Bottom