Watoto wawili iwe sera mahususi ya uzazi wa mpango kwa Tanzania ya sasa

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,966
46,736
Hali ya maisha nchini imezidi kuwa ngumu zaidi, hali ni ngumu zaidi kwa familia zenye watu wengi ambao ni tegemezi kwa angalau wanafamilia wachache wenye kipato ambacho nacho ni kidogo. Matokeo yake watu wengi wamekuwa wakiishi maisha ya mkononi kwa mdomoni tu "hand to mouth" kwa sasa jambo ambalo ni hatari sana.

Mwaka 1980 China baada ya kuona idadi ya watu wake inaongezeka kwa kasi huku kiwango cha umaskini bado kikiwa juu na ikiwa na malengo makubwa ya maendeleo ilianzisha sera ya mtoto mmoja kwa familia moja. Sera hiyo ililegezwa mwaka 2015 ambapo familia ziliruhusiwa kuwa na watoto hadi wawili.

Kwa sasa wastani wa mwanamke kuzaa watoto Tanzania ni watoto 5! Hiki ni kiwango mara mbili zaidi ya wastani wa kidunia. Hiki ni kiwango kikubwa sana kulinganisha na hali ya uchumi ya raia wengi. Hali hii inachangia kuzoretesha kasi ya maendeleo, kuongeza ugumu wa maisha na umaskini kwa kiasi kikubwa.

Ni wakati wa sasa serikali ya Tanzania kulipa umuhimu jambo hili na kuja na sera mahususi ya kuhamasisha wananchi kutozaa watoto zaidi ya wawili. Watoto wawili iwe ni ukomo hadi hali ya uchumi itakopukwa nzuri.
 
Tupo wachache sana ndio maana akili zimelala, tunatakiwa kuwa wengi, si ajabu huko mitaani kukuta vijana wameamka asubuhi wanakaa kwenye vibaraza kuota jua, tuko slow sana.

Hata hivyo uwingi ni ni nguvu kazi, zinahitajika strategies madhubuti za kuitumia hizo nguvu kazi.
 
Mbona mininao wa 8 na hakuna anae soma shule ya serikali. Pombe nakunywa. Bange navuta. Pia nishajenga vibanda kadhaa na chuma nasukuma.
Ebu vijana acheni uvivu, fanyeni kazi kwa bidii. Yaani mkisha toka hukk vinijini mkafika Daslam mkaanza kula chips sijui hua mnakuaje wallah...🤨
 
Bwashee kama wewe nguvu za kupata watoto zimeisha basi hiyo ni juu yako, lakini usitupangie juu wa uwezo wetu wa kuzaa.
Ni afadhali serikali ielimishe watu kuzaa idadi ya watoto wanaoweza kuwatunza, lakini siyo kupanga idadi ya watoto. Acha watu tupige mabao mpaka fundi alipoishia 😂😂
 
Usitupangie watoto wa kuzaa bhana. Kama ww huna uwezo wa kulea ni wewe. Kuna wengine Wana watoto 7 na wote wanasoma nje. Kula anakula kama kawaida mpaka wanasaza...

Mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe na ndo huongoza kuwa na watoto wengi. Ila matajiri ata sielewag mbegu zao huwa wanapelekaga wapi, unakuta watoto 2 au 3 . Itbd wapewe elimu watu km Hawa.
 
Hali ya maisha nchini imezidi kuwa ngumu zaidi, hali ni ngumu zaidi kwa familia zenye watu wengi ambao ni tegemezi kwa angalau wanafamilia wachache wenye kipato ambacho nacho ni kidogo...
Wale wa kule huwaambii kitu. Kila mtoto anakuja na riziki yake watakwambia na Ni maamlisho ya mkubwa, unquestionable watasema. Outcome ndio wanatengeneza pc kubwa ya panya road na vibaka wengine.
 
Hali ya maisha nchini imezidi kuwa ngumu zaidi, hali ni ngumu zaidi kwa familia zenye watu wengi ambao ni tegemezi kwa angalau wanafamilia wachache wenye kipato ambacho nacho ni kidogo...
Airdhi yote hii ,ACHA ibaki ilivyo ,watu wazae bwana
 
Sasa mbona vijana waliogeuka wachuuzi wa bidhaa za Kichina kweny barabara za miji wakitolewa barabarani hawaendi kwenye hiyo ardhi badala yake wanatishia wanasiasa tu??
Airdhi yote hii ,ACHA ibaki ilivyo ,watu wazae bwana
 
Miafrika inazaana kama mbwa na haina mipango thabiti ya malezi na makuzi ya watoto wao...

Unakuta mimama ya kiafrika imepagata watoto kila mahali huku hali zao zikitia kinyaa sana.
Walikuja kuomba unga kwako? Umewahi kusikia wanaomba msaada kwako? Waache maana maisha haya Kila mtu na faraja yake. "Masikini na wanangu, tajiri na Mali zake"
 
Back
Top Bottom