Jof3
JF-Expert Member
- Jan 28, 2013
- 660
- 313
Ndugu zangu wana JamiiForums huko kwenu Hali ya umeme ikoje baada ya mvua?
Huku kwetu tuna siku 3 mfululizo hatuna umeme maeneo ya vikindu kilongoni tumeshapiga simu weee jamaa wamekausha.
Wengi Kula yetu inategemea ufanye kazi kwenye computer ndio upate riziki. Sijui hawa jamaa wanashida gani.
Halafu hii tabia ya watumishi wa TANESCO kuchangisha wananchi vimichango ndio tabia gani? Hii ni aibu Kwa taifa. Imefika hatua nikahisi labda nipo ukimbizini kama sipo kwenye nchi yangu.
Cha kushangaza nimesherehekea sikukuu ya muungano nikiwa gizani dah inauma Sana. Imezoeleka umeme ukija utasikia watoto wanapiga kelele "huooooo".
TANESCO fanyeni kazi Kwa weledi.
Huku kwetu tuna siku 3 mfululizo hatuna umeme maeneo ya vikindu kilongoni tumeshapiga simu weee jamaa wamekausha.
Wengi Kula yetu inategemea ufanye kazi kwenye computer ndio upate riziki. Sijui hawa jamaa wanashida gani.
Halafu hii tabia ya watumishi wa TANESCO kuchangisha wananchi vimichango ndio tabia gani? Hii ni aibu Kwa taifa. Imefika hatua nikahisi labda nipo ukimbizini kama sipo kwenye nchi yangu.
Cha kushangaza nimesherehekea sikukuu ya muungano nikiwa gizani dah inauma Sana. Imezoeleka umeme ukija utasikia watoto wanapiga kelele "huooooo".
TANESCO fanyeni kazi Kwa weledi.