A
Anonymous
Guest
Mimi sio mtu wa mitandao sana lakini nimeona malalamiko kadhaa yanayoandikwa na Jamii Forums kuhusu mambo mbalimbali yanafanyiwa kazi hasa kuhusu huku kwenye shughuli zetu tunazozifanya kwenye miradi.
Mimi ni mmoja wa Wakandarasi wadogo ambao tumekuwa tukifanya kazi na Mkandarasi Mkuu wa Mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR, Kampuni ya Yapi Merkezi tangu Februari 2022.
Hadi kufikia leo naandika andiko hili, kupitia Kampuni ya Mzamiru Development Ltd namdai Mkandarasi huyo kiasi cha Tsh. Milioni 440 (fedha za Kitanzania), nimekuwa nikidai malipo yangu tangu Januari, Mwaka huu (2023) lakini nazungushwa kulipwa.
Nilianza kufanya nao kazi kuanzia Lot 1 (awamu ya kwanza), nawakodisha magari ya maji yanayotumika kwenye mradi, ikaendelea hivyo pia Lot 2.
Nimeambatanisha na sample ya mkataba wa ukodishaji vifaa.
Huko siku za nyuma nilikuwa nalipwa japo sio katika kiwango ambacho tumekubaliana, mfano unaweza kudai Milioni 100 lakini wakakupa Milioni 10 na kuahidi kuendelea kukulipa baada ya muda.
Utaratibu tuliowekeana ni kuwa kila mwezi tunatakiwa kulipwa kiasi fulani, lakini ilipofika mwezi wa kumi na mbili mwaka jana (2022) ndipo malipo yalipoanza kukwama.
Mpaka sasa naendelea nao kwenye Awamu ya Tatu yaani Lot 3, hakuna malipo na magari yangu niliyowakodisha bado yapo kwenye kazi.
Nimesumbuka sana kufuatilia malipo yangu lakini sioni dalili za kulipwa, hofu yangu ni kuwa inawezekana mambo yakawa magumu zaidi siku za mbele hivyo kunipa hasara kubwa.
Naomba Serikali isaidie watu kama sisi ambao ni Wakandarasi tunaopambana kujiweka kwenye mstari, kwani mtaji wangu niliowekeza hapo haunisaidii peke yangu, kuna Watanzania wenzangu wengi wanaofaidika kupitia ajira hiyo.
Mimi ni mmoja wa Wakandarasi wadogo ambao tumekuwa tukifanya kazi na Mkandarasi Mkuu wa Mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR, Kampuni ya Yapi Merkezi tangu Februari 2022.
Hadi kufikia leo naandika andiko hili, kupitia Kampuni ya Mzamiru Development Ltd namdai Mkandarasi huyo kiasi cha Tsh. Milioni 440 (fedha za Kitanzania), nimekuwa nikidai malipo yangu tangu Januari, Mwaka huu (2023) lakini nazungushwa kulipwa.
Nilianza kufanya nao kazi kuanzia Lot 1 (awamu ya kwanza), nawakodisha magari ya maji yanayotumika kwenye mradi, ikaendelea hivyo pia Lot 2.
Nimeambatanisha na sample ya mkataba wa ukodishaji vifaa.
Huko siku za nyuma nilikuwa nalipwa japo sio katika kiwango ambacho tumekubaliana, mfano unaweza kudai Milioni 100 lakini wakakupa Milioni 10 na kuahidi kuendelea kukulipa baada ya muda.
Utaratibu tuliowekeana ni kuwa kila mwezi tunatakiwa kulipwa kiasi fulani, lakini ilipofika mwezi wa kumi na mbili mwaka jana (2022) ndipo malipo yalipoanza kukwama.
Mpaka sasa naendelea nao kwenye Awamu ya Tatu yaani Lot 3, hakuna malipo na magari yangu niliyowakodisha bado yapo kwenye kazi.
Nimesumbuka sana kufuatilia malipo yangu lakini sioni dalili za kulipwa, hofu yangu ni kuwa inawezekana mambo yakawa magumu zaidi siku za mbele hivyo kunipa hasara kubwa.
Naomba Serikali isaidie watu kama sisi ambao ni Wakandarasi tunaopambana kujiweka kwenye mstari, kwani mtaji wangu niliowekeza hapo haunisaidii peke yangu, kuna Watanzania wenzangu wengi wanaofaidika kupitia ajira hiyo.