A
Anonymous
Guest
Mimi ni miongoni mwa Wafanyakazi wa Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Kitengo cha utafiti KILIMANJARO CLINICAL RESEARCH INSTITUTE (KCRI).
Katika kitengo hiki Waajiriwa wengi ni wale wa mkataba, kwani wao huwa wanaajiriwa kutokana na miradi iliyopo, hivyo pindi miradi inapoisha huwa mikataba yao pia huisha.
Sasa yapata mwezi wa tatu au wanne hatupati huduma za matibabu kupitia Bima za NHIF.
Tumejaribu kufuatilia kwa muda sasa lakini majibu tunayopewa yanakuwa ya kukatisha tamaa, kila siku ni stori zilezile za “linafuatiliwa” “linafanyiwa kazi” lakini siku zinazidi kwenda, mishahara inakatwa fedha kwa ajili ya bima lakini hakuna huduma ya Bima inapotokea wanahitaji huduma hiyo.
Tunateseka, wengi wetu ni Watoto kutoka familia duni na Wazazi wetu ndio hufaidika na bima hizo kupitia sisi.
Inapotokea huduma haipatikani kidogo inakuwa ni changamoto sana kwenye kutoa cash, kwani huo mwisho wa mwezi wenyewe unajikuta una madeni kila mahali.
Katika kitengo hiki Waajiriwa wengi ni wale wa mkataba, kwani wao huwa wanaajiriwa kutokana na miradi iliyopo, hivyo pindi miradi inapoisha huwa mikataba yao pia huisha.
Sasa yapata mwezi wa tatu au wanne hatupati huduma za matibabu kupitia Bima za NHIF.
Tumejaribu kufuatilia kwa muda sasa lakini majibu tunayopewa yanakuwa ya kukatisha tamaa, kila siku ni stori zilezile za “linafuatiliwa” “linafanyiwa kazi” lakini siku zinazidi kwenda, mishahara inakatwa fedha kwa ajili ya bima lakini hakuna huduma ya Bima inapotokea wanahitaji huduma hiyo.
Tunateseka, wengi wetu ni Watoto kutoka familia duni na Wazazi wetu ndio hufaidika na bima hizo kupitia sisi.
Inapotokea huduma haipatikani kidogo inakuwa ni changamoto sana kwenye kutoa cash, kwani huo mwisho wa mwezi wenyewe unajikuta una madeni kila mahali.