matunduizi
JF-Expert Member
- Aug 20, 2018
- 6,686
- 15,592
Wamama wa miaka ya 90 kurudi nyuma walikuwa vyuma kwelikweli.
Walikuwa na uwezo wa kukuchapa na kukunyoosha kwa macho tu. Nakumbuka siku nilipotoroka nyumbani kwenda na magenge ya watoto mitaani kutembea. Bahati mbaya nikakutana naye amekaa katikati ya kundi la kinamama kuna jicho alinikata nilitoka mbio bila kupumzika hadi nyumbani nikisubiri usiku yatokanayo.
Hii ilikuwa inatukuta watoto wote mtaani, ukitoroka kwenda kudoea msosi kwa jirani macho tu yatakutoa kwenye ugali.
Leo nimeshangaa sana, dada na mtoto wake nyumbani, mtoto anamuabisha mbele za wageni, mtoto anakatwa kajicho flani kakizembe anacheka na kukapotezea.
Imekuaje wamama wa siku hizi wamepoteza utisho wa kianamke. Hawana ushawishi wa zile signal za kimaadili ambazo ilikuwa ukionyeshwa tu unakaa mguu sawa na kufuata maelekezo kabla hata uchapwa fimbo.
No hilo tu.
Walikuwa na uwezo wa kukuchapa na kukunyoosha kwa macho tu. Nakumbuka siku nilipotoroka nyumbani kwenda na magenge ya watoto mitaani kutembea. Bahati mbaya nikakutana naye amekaa katikati ya kundi la kinamama kuna jicho alinikata nilitoka mbio bila kupumzika hadi nyumbani nikisubiri usiku yatokanayo.
Hii ilikuwa inatukuta watoto wote mtaani, ukitoroka kwenda kudoea msosi kwa jirani macho tu yatakutoa kwenye ugali.
Leo nimeshangaa sana, dada na mtoto wake nyumbani, mtoto anamuabisha mbele za wageni, mtoto anakatwa kajicho flani kakizembe anacheka na kukapotezea.
Imekuaje wamama wa siku hizi wamepoteza utisho wa kianamke. Hawana ushawishi wa zile signal za kimaadili ambazo ilikuwa ukionyeshwa tu unakaa mguu sawa na kufuata maelekezo kabla hata uchapwa fimbo.
No hilo tu.