Kwa mambo yanavyoendelea kuhusu wasafirishaji haramu wa binadamu tusishangae kuona kuna viongozi watatumbuliwa

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
943
4,457
Nimesoma kitu kinachoitwa usafirishaji haramu wa binadamu huko Duniani na mbinu zinazotumiwa. Takwimu zinaonyesha kwamba hii biashara ni kubwa labda namba tatu baada ya biashara ya silaha na madawa ya kulevya.

Nimejikuta kusoma kutokana na kuona ndani ya wiki mbili zimekamatwa V8 tatu nchini zikiwa na wahamiaji haramu ambao ukiwaangalia kwenye picha unaona wamedhoofu sana.

Taarifa zinaonyesha kwamba Duniani biashara hii inafanywa na viongozi wa umma na kisiasa. Inafanywa na matajiri wakubwa ambao kabla ya kufanya haya ukikuta kutengeneza network nzuri na wanasiasa waliopo madarakani kuepusha mkono wa sheria.

Tanzania kwa hali hii inayoendelea ni Ishara kwamba wanasiasa wanatafuta fedha za uchaguzi 2025. Katika hali hii hakuna mwanasiasa atakayekamatwa na vyombo vya dola then hao waliomkamata wakabaki salama. Ukijitia kukamata lazima aidha uondolewe kwenye kiti au usimamishwe kazi.

Mimi siyo mtabiri ila kwa ukamataji unaofanywa na Polisi na Uhamiaji siku si nyingi utasikia viongozi wa taasisi hizi kwenye mikoa na makao makuu wametambuliwa. Watatumbuliwa kwa sababu wanaosafirisha hawa wahalifu ni wabunge, ni mawaziri, madiwani, watendaji wa vijiji, wafadhili wa vyama vya siasa nk.

Dalili hizi zimeonekana Duniani kote ambapo mfumo wa serikali umeruhusu wenye fedha kupanga safu ya utawala wanayotaka.

Tumeona namna ambavyo wanaopambana na madawa wanatumbuliwa kila siku; siyo kwamba wanakosea ila wanaingilia anga za wenyewe. Na mimi pia niwaandae kisaikologia viongozi wa polisi kwenye root zote zinazotumiwa na hawa viongozi kupitisha magendo yao kwamba wajiandae kutumbuliwa.

Niwatake waliopo makao makuu ya hizi taasisi kujiandaa kisaikolojia kwani muda si muda usishangae fedha ikapenya bungeni wabunge wakaanza kupiga kelele kwanini hawa watu wanakamatwa Morogoro, Manyara, Iringa, Dodoma, Mbeya.......utasikia kwanini wasizuiliwe huko mipakani na wataconculude viongozi wameshindwa kazi waondolewe.

IGP na Mkuu wa Uhamiaji msikubali kudhibitiwa na wahalifu hawa wanaowaza matumbo yao. Pelekeni kikosi wanapoingilia Tanga, Kilimanjaro , Arusha na huko Mara mkalinde mpaka. Bora wawapige Majungu mtumbuliwe kwa kuwadhibiti kuliko kuogopa kudhibiti.

Mwisho; tuambieni hizi V8 mlizokamata zimesajiliwa kwa majina gani? Msipowataja hao wamiliki mnawafanya wengine nao kuendelea kutumia malori na mashangingi kushamirisha uhalifu huu. Kwanini hakuna mmiliki wa V8 aliyekamatwa na kuhojiwa hadi sasa?
 
Mwisho; tuambieni hizi V8 mlizokamata zimesajiliwa kwa majina gani? Msipowataja hao wamiliki mnawafanya wengine nao kuendelea kutumia malori na mashangingi kushamirisha uhalifu huu. Kwanini hakuna mmiliki wa V8 aliyekamatwa na kuhojiwa hadi sasa?
Hapa ndio msingi wa hoja yako ulipo. Mara nyingi tumeona polisi wakijinadi kukamata either sijui boti yenye magendo kwenye bandari bubu, shehena ya madawa ya kilevya, wahamiaji haramu.

Lakini hatujawahi kusikia waliokamatwa ni akina nani na wana connection na akina nani. Yani hizi habari huishia juu kwa juu.

Hii inaonyesha kuna syndicate ambayo ina mkono mrefu ambayo haizuiliki na hata hizi kamata kamata za kikuda ni kuchomeana tu au kuzungukana kwa member ili kuharibiana ila mwisho wa siku wanayamaliza kimya kimya.
 
Kwahiyo kwa kuwa umeshawatisha kwamba watashughulikiwa basi tena wataona ni bora wasiwaudhi wale wakubwa wenye biashara zao !

Kunguru muoga hukimbiza mbawa zake !!
Hatar sn !.
 
LUGHA YA KIINGEREZA PIA ITUMIKE NA JESHI LA POLISI / UHAMIAJI WANAPORUSHA HABARI YOUTUBE DUNIA IFAHAMU TATIZO

Mimi ningependa habari hizi uhamiaji kuahabaridha dunia na ukanda huu wa Pembe ya Afrika, Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika kwa kuweka habari hizi kwa lugha ya Kiingereza ili dunia ifahamu kwa haraka ukubwa wa wimbi hili la wakimbizi kutoka Eritrea, Ethiopia, Somalia wanaokatika Tanzania wakiruhusiwa kupita Kenya kuelekea Kusini mwa Afrika kama kweli wanataka biashara hii ya usafirishaji binadamu ipungue.

Mfano : Wahamiaji: Safari toka Congo kupitia Brazil mpaka Canada kwa miguu

16 December 2023
Unveiling Ethiopia's Southern Route: The Perils and Promises of Ethiopian Migrants to South Africa, Abiy Ahmed, IOM, UNHCR

SOUTH SOUTH MIGRATION

View: https://m.youtube.com/watch?v=bfHuwb6iwuA
 
Lugha ya kiswahili inayotumiwa na Polisi na idara ya Uhamiaji kuelezea tatizo la biashara ya usafirishaji binadamu haitoshi kuufahamisha ulimwengu tatizo, labda kama kutakuwepo wanaofaidika na biashara hii ndiyo maana hakuna juhudi za makusudi kuifahamisha dunia kwa kutumia lugha ya Kiingereza kuwa jela na mahabusu zetu zimejaa wahamiaji wenye ndoto za kutoka kiuchumi Afrika ya Kusini kuelekea Ulaya na Marekani


View: https://m.youtube.com/watch?v=yxe1PXVLTII
 
Kwahiyo kwa kuwa umeshawatisha kwamba watashughulikiwa basi tena wataona ni bora wasiwaudhi wale wakubwa wenye biashara zao !

Kunguru muoga hukimbiza mbawa zake !!
Hatar sn !.
Nimewakilisha wajue nguvu inayowakataza kutangaza wamiliki wa haya ma V8 ndiyo inayotumika kunyamazisha wabunge na viongozi wa dola wasihoji.

Hakuna siku utasikia mbunge akimwambia waziri wa mambo ya ndani awataje wamiliki wa haya magari yanayokatwa labda ikamatwe gari ya mwanasiasa mwenye damu ya kunguni
 
Ukiona mpaka wanatangaza kua wamekamata basi negotiation huko chini ilifeli.

Ama lah hao ni mbuzi wa kafara ili ionekane jeshi lipo kazini.

Kama uko road basi lazima utakua ushaona au kukutana na kisanga cha trafki mpenda rushwa kuikataa hata 20k yako, kuna muda wanapiga mdefu ila kuna muda inabidi report iende kua yupo kazini, bila kukukamata na kukuandkia itaonekana hafanyi kazi.
 
Juhudi binafsi zisizokuwa na mguso katika habari zinazobidi kuvuka mipaka wakati kamishana wa uhamiaji mkoa wa Iringa alivyotoa onyo kimataifa kwa lugha yetu ya kiswahili kuwa Tanzania siyo sehemu salama kwa wahamiaji haramu wanaokatiza nchini, hakika ingekuwa vyema kwenda kimataifa kuzuia biashara hiyo na ni kwa kutoa taarifa kwa lugha ya kimataifa kila wanaporipoti habari hizi za hatari

2018 24 February
83 immigrant from Ethiopia detained in Tanzania


View: https://m.youtube.com/watch?v=ub35WECQr94
7.3K views · 6 years ago...more
Source : Bongo View TV
 
Nimewakilisha wajue nguvu inayowakataza kutangaza wamiliki wa haya ma V8 ndiyo inayotumika kunyamazisha wabunge na viongozi wa dola wasihoji.

Hakuna siku utasikia mbunge akimwambia waziri wa mambo ya ndani awataje wamiliki wa haya magari yanayokatwa labda ikamatwe gari ya mwanasiasa mwenye damu ya kunguni
Duh 🙄 !
Lakini msg sent. !’🙏😅
 
Nimesoma kitu kinachoitwa usafirishaji haramu wa binadamu huko Duniani na mbinu zinazotumiwa. Takwimu zinaonyesha kwamba hii biashara ni kubwa labda namba tatu baada ya biashara ya silaha na madawa ya kulevya.

Nimejikuta kusoma kutokana na kuona ndani ya wiki mbili zimekamatwa V8 tatu nchini zikiwa na wahamiaji haramu ambao ukiwaangalia kwenye picha unaona wamedhoofu sana.

Taarifa zinaonyesha kwamba Duniani biashara hii inafanywa na viongozi wa umma na kisiasa. Inafanywa na matajiri wakubwa ambao kabla ya kufanya haya ukikuta kutengeneza network nzuri na wanasiasa waliopo madarakani kuepusha mkono wa sheria.

Tanzania kwa hali hii inayoendelea ni Ishara kwamba wanasiasa wanatafuta fedha za uchaguzi 2025. Katika hali hii hakuna mwanasiasa atakayekamatwa na vyombo vya dola then hao waliomkamata wakabaki salama. Ukijitia kukamata lazima aidha uondolewe kwenye kiti au usimamishwe kazi.

Mimi siyo mtabiri ila kwa ukamataji unaofanywa na Polisi na Uhamiaji siku si nyingi utasikia viongozi wa taasisi hizi kwenye mikoa na makao makuu wametambuliwa. Watatumbuliwa kwa sababu wanaosafirisha hawa wahalifu ni wabunge, ni mawaziri, madiwani, watendaji wa vijiji, wafadhili wa vyama vya siasa nk.

Dalili hizi zimeonekana Duniani kote ambapo mfumo wa serikali umeruhusu wenye fedha kupanga safu ya utawala wanayotaka.

Tumeona namna ambavyo wanaopambana na madawa wanatumbuliwa kila siku; siyo kwamba wanakosea ila wanaingilia anga za wenyewe. Na mimi pia niwaandae kisaikologia viongozi wa polisi kwenye root zote zinazotumiwa na hawa viongozi kupitisha magendo yao kwamba wajiandae kutumbuliwa.

Niwatake waliopo makao makuu ya hizi taasisi kujiandaa kisaikolojia kwani muda si muda usishangae fedha ikapenya bungeni wabunge wakaanza kupiga kelele kwanini hawa watu wanakamatwa Morogoro, Manyara, Iringa, Dodoma, Mbeya.......utasikia kwanini wasizuiliwe huko mipakani na wataconculude viongozi wameshindwa kazi waondolewe.

IGP na Mkuu wa Uhamiaji msikubali kudhibitiwa na wahalifu hawa wanaowaza matumbo yao. Pelekeni kikosi wanapoingilia Tanga, Kilimanjaro , Arusha na huko Mara mkalinde mpaka. Bora wawapige Majungu mtumbuliwe kwa kuwadhibiti kuliko kuogopa kudhibiti.

Mwisho; tuambieni hizi V8 mlizokamata zimesajiliwa kwa majina gani? Msipowataja hao wamiliki mnawafanya wengine nao kuendelea kutumia malori na mashangingi kushamirisha uhalifu huu. Kwanini hakuna mmiliki wa V8 aliyekamatwa na kuhojiwa hadi sasa?

Google auto translator

With the things that are going on about human traffickers, we should not be surprised to see that some leaders will be purged​


I have read something called human trafficking in the world and the methods used. Statistics show that this business is probably number three after the illegal arms and drug trade internationally.

I found myself reading from seeing that within two weeks, three V8s have been arrested in the country with illegal immigrants who, if you look at them in the picture, you can see that they are very weak.

Information shows that in the world this business is done by public and political leaders. It is done by the rich who, before doing this, create a good network with politicians in power to avoid the hand of the law.

In Tanzania, this ongoing situation is a sign that politicians are looking for money for the 2025 election. In this situation, no politician will be arrested by the state agencies, then those who arrested him will remain safe. If you commit an arrest, you must either be removed from the seat or suspended.

I am not a forecaster, but with the arrests made by the Police and Immigration, not many days later you will hear that the leaders of these institutions in the regions and headquarters have been identified. They will be exposed because those who transport these criminals are members of parliament, ministers, councilors, village officials, donors of political parties, etc.

These symptoms have been seen all over the world where the government system has allowed the wealthy to organize the hierarchy they want.

We have seen the way that those who struggle with drugs are killed every day; It's not that they are wrong, but they are interfering in their own space. And I should also psychologically prepare the police leaders on all the routes used by these leaders to pass their contraband so that they prepare to be exposed.

I want those present at the headquarters of these institutions to prepare themselves psychologically because soon don't be surprised when money penetrates the parliament and MPs start shouting why these people are being arrested in Morogoro, Manyara, Iringa, Dodoma, Mbeya.......you will hear why they should not be detained at the borders and they will conclude that the leaders have failed jobs should be removed.

The IGP and the Head of Immigration do not accept to be controlled by these criminals who think their guts. Send the squad when they invade Tanga, Kilimanjaro, Arusha and in Mara, guard the border. It is better that they beat the goblins and be recognized for controlling them than to be afraid to control them.

Finally; tell us what names are these V8s you caught registered under? If you do not name the owners, you are making others continue to use trucks and vans to promote this crime. Why has no V8 owner been arrested and questioned so far?
 
Back
Top Bottom