Mwanaukweli
JF-Expert Member
- May 18, 2007
- 4,786
- 1,710
Misa ya Mazishi ya wahanga wa mlipuko wa Jumapili iliyopita kwenye parokia teule ya Olasiti imeanza katika eneo lile lile mlipuko ulipotokea.
Misa inaongozwa na Muadhama Polycarp Kardinal Pengo, Askofu Mkuu wa Dar es Salaam.
Maandamano yalianzia toka chumba cha kuhifadhia maiti, miili ikapelekwa makao makuu ya Asofu Mkuu, Burka. Hivi sasa imeshawasili kanisani na Askofu Mkuu Lebulu amesali sala ya kuipokea miili kanisani.
Askofu Mkuu amemaliza sala hiyo, kuna wimbo wa maombolezo unaimbwa kwa sasa.
Askofu amemaliza kubariki maji.
Wanaopenda kufuata live bonyeza link hii: Radio Maria Tanzania - FM 89.1 - Dar es Salaam - Streema Player
======================================
Updates
======================================
Mahubiri ya Kardinali Pengo
Ndugu zangu,
==================
Update Neno la Askofu Malasusa
==================
Tunaagana na ndugu zetu katika mwili.
Ni ibada yenye majonzi lakini ni yenye furaha kwa kuwa ndugu zetu wamelala katika imani na wataupata uzima wa milele.
Natoa pole kwa wafiwa na kwa Baba Askofu Lebulu.
Yesu yu hai nasi tunaomwamini tutakuwa hai, hata miili itakapoharibika, tutaurithi uzima wa milele.
Kama alivyosema Kardinali tusilipe ubaya kwa ubaya, lakini tusiwe waoga. Tumtangaze bila woga. Tuelewe pia kuwa hatutahukumiwa tu kwa maovu tuliyotenda bali hata kwa mema ambayo hatukuyatenda
Risasi wanazopigwa watumishi wa Mungu, mioto ya kuchoma makanisa, mabomu wanayotupiwa waumini, yasitukatishe tamaa.
Askofu Malasusa anaseama pia: Anatamani kama angefariki katika ibada kama marehemu hawa. Heri wafu wafao katika Bwana.
==================
Update: Salamu za Waziri Mkuu
==================
Ni siku ya majonzi, lakini ni siku ya kuwaombea ndugu zetu marehemu.
Tukio hilo limetokea, tuwaombee ndugu zetu marehemu.
Kwa niaba ya Rais na serikali yote, nawapa pole, naungana na wafiwa na kuwaomba wajitahidi kubeba msiba huu.
Anawapa pole waumini wa Olasiti. Tukio limetokea katika mazingira yasiyotarajiwa. Waliokuwepo tukio hilo limewashtua na bila shaka litabaki.
Anamshukuru Baba Paroko. Alipomtembelea alifarijika kwa maneno yake ambayo leo yamesemwa tena na Kardinali.
Anatoa pole kwa Baba Askofu Mkuu Josephat Lebulu, Mungu ampe nguvu ya kuendelea kuongoza waamini.
Kwa Mwadhama Kardinali, pole tena. Kwa kuwa jambo hili limetokea katika kanisa katoliki.
Anawaombea viongozi wote wa dini wasikate tamaa.
Anasema kuwa ni kujidanganya kudhani kuwa ukiua muumini mmoja utaua ukristu, Haitawezekana.
Hawa waovu wachache, serikali tutawasaka na kuchukua hatua za kisheria. wanajua kuwa kwa hatua ya sasa, hawataweza kufuta ukristo kwa njia hiyo.
Ukristo na uislamu zina historia ndefu. Tutajidanganya kuwa mufti akiuawa ukristo utauliwa.
Serikali itashugulikia kikamilifu kundi ambalo lengo lao ni kuharibu amani yetu Tanzania. Wanataka tushindwa kuishi kwa amani. tusikubali tufikie hapo.
Anasema tumeagiza vyombo vyote husika vifanye kazi kuhakikisha utulivu na amani vinaendeleza. kamata kamata zitaongezeka. Lakini ni kwa kuondoa hali hii inayotishia usalama wetu.
Anaomba ushirikiano wa wananchi wote. Waovu wako miongoni mwetu.
Tutaisaidia sana serikali tukiwajulisha waovu hao. Ametoa rambi rambi Sh 100 milioni.
====================================
Update: Neno la Shukrani toka Askofu Mkuu Lebulu
====================================
Kwa niaba ya mapade, watawa, walei wote alitoa pole kwa familia ya kanisa la Arusha.
Kwa msiba huu anasema Wakristu tunajiuliza Mungu una ujumbe gani kwetu?
Alitoa pole, kwa ndugu za marehemu watatu. Alitoa pole kwa wafiwa na kusema hakika tumeguswa sana na hata hatuna maneno ya kuelezea, tuliwatembelea mahospitalini na hakika watu wa Mungu wameumizwa sana. Pole sana kwa waumini wa kanisa hili na wakaazi wa eneo hili. Alisisitiza Tusikate tamaa!
Alitoa pole kwa wanafamilia ya Mungu wa Olasiti waliokuwa kwenye siku yao ya furaha ya kufungua parokia yao.
Alitambua majitoleo waliyofanya wana Olasiti kwa kumjengea Mungu nyumba. Walijenga nyumba ya Mungu kwa nguvu zao bila ufadhili toka nje. Wakati wanataka kumtolea Mungu shukrani zao wamekatishwa, lakini hakuna kukata tamaa.
Alitoa shukrani kwa wale walioonesha moyo wa utu kulaani unyama ule.
Aliishukuru serikali ya wilaya, mkoa na serikali kuu waliokuwa pamoja katika msiba huu. Na anamshukuru Waziri mkuu kwa uwepo.
Anashukuru na Serikali ya Zanzibar kwa moyo wa utu, kwamba walimtembelea na waliwafariji wakristo wote wa Arusha.
Aliwaambia waumini Msiogope! Kristo akiwa upande wetu hakuna atakayetushinda.
Kristo ametuambia katika Injili ya Yohane: Msifadhaike mioyoni mwenu, mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Yesu aliwaambia pia Msiogope. Mkijua mafundisho yangu, mtaujua ukweli na ukweli utawaweka huru.
Anasema yeye kama baba anawaambia, lazima ifikie mahali tuseme INATOSHA, Tumwambie Mungu IMETOSHA. Wenye nguvu na silaha watatushinda, lakini tukiwa na Mungu hatutashindwa. Paulo na Sila walisali Milango ya gereza ikafunguka.
Tusali kwa nguvu zote.
Alimaliza kwa kuwaaga marehemu akiwataja kwa majina na kumwambia kila mmoja kwa heri!
================
Mapadre wa Arusha wakiwa wamebeba jeneza la mtoto Patricia.
Mapadre wakiwa wamebeba jeneza la mama Regina Laizer
Mapadre na Maaskofu mbele ya majeneza yaliyobeba miili ya marehemu wakati Askofu Lebulu anayabariki mara baada ya kuingia kanisani.
Askofu Lebulu akiwa ananyunyizia maji ya Baraka. Kulia ni Paroko wa Parokia hiyo. Kushoto kabisa ni Maaskofu Amani, Askofu Nkwande, Askofu Dallu, na aliyeshika fimbo yenye msalaba Kardinali Pengo.
Kardinali Pengo akisali sala, pamoja na Askofu Mkuu Josephat Lebulu
Misa inaongozwa na Muadhama Polycarp Kardinal Pengo, Askofu Mkuu wa Dar es Salaam.
Maandamano yalianzia toka chumba cha kuhifadhia maiti, miili ikapelekwa makao makuu ya Asofu Mkuu, Burka. Hivi sasa imeshawasili kanisani na Askofu Mkuu Lebulu amesali sala ya kuipokea miili kanisani.
Askofu Mkuu amemaliza sala hiyo, kuna wimbo wa maombolezo unaimbwa kwa sasa.
Askofu amemaliza kubariki maji.
Wanaopenda kufuata live bonyeza link hii: Radio Maria Tanzania - FM 89.1 - Dar es Salaam - Streema Player
======================================
Updates
======================================
Mahubiri ya Kardinali Pengo
Ndugu zangu,
Nafasi hii inaunganisha mawazo ya furaha na uchungu kutokana na kilichotukutanisha leo.
Mazingira haya yanaweka ugumu wa kupata cha kusema. Ila sisi ni watu wa imani. napenda kueleza imani yetu kama tunavyopaswa kuwa kwenye mazingira haya.
Tumejumuika ili kuwaweka kwenye nyumba ya milele hawa marehemu, lakini pia tunatumia nafasi hii kubariki Kanisa.
Kila mbatizwa ni kiungo cha mwili wa Kanisa. Kila kiungo cha mwili kinapaswa kuungana na kichwa cha Mwili ambae ni Yesu Mwenyewe
Kristo akipitia kwa mdomo wa mtume Paulo anatufundisha kuwa "Msijaribu kushindana na uovu kwa uovu, lakini shindeni uovu kwa wema".
Katika viongozi waanzilishi wa dini, ni Yesu peke yake aliyetolea uhai wake kujenga imani ya wafuasi wake. Viongozi wengine hawajikutoa sadaka wenyewe, na baadhi wametoa sadaka ya maisha ya watu wengine kwa ajili ya kueneza imani yao.
Sisi Wakristu Imani yetu inajengwa juu ya mwanzilishi wetu ambaye alitoa uhai wake ili kujenga imani yetu, na hakutoa uhai wa mtu yeyote kwa ajili ya kujenga imani yetu.
Katika masomo tuliyosikia leo, Somo la plili limetupa neno la Mtume Paulo Rum:12:17 linasisitiza hilo: usishinde uovu kwa uovu, bali shinda uovu kwa wema.
Soma la Kwanza limeeleza kuwa Paulo na Sila wanateswa kwa ubaya mkubwa sana na kuwekwa gerezani kwa ubaya. Na baada ya kufunguliwa kwa muujiza, askari wa magereza alitaka kujiua, lakini Paulo na Sila wakatenda lililo jema kuokoa maisha yake. Ni baada ya wema huo wokovu ulifika kwa askari huyo na jamaa yake yote wakaweza kumwamini Mungu.
Nawauliza waumini: "Wale waliotekeleza ubaya huu, akija mbele yetu akasema ni mimi ndiye, tungefanya nini kama waumini kwa kufuata mfano wa Yesu?"
Mimi nawaambia "Tujifunze kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo: 'Tusidiriki kulipia uovu kwa uovu, lakini tutende mema ili kushinda uovu'."
Lakini haya hayaondoi majukumu ya serikali, ambayo yanabaki, na si mimi ninayepaswa kuyasema, wenye mamlaka wanayajua majukumu yao. Mimi nawaambia ninyi waumini.
Uovu si kitu kinachopendeza. Warumi waliwatesa wakristo kwa karne tatu, na haikusaidia chochote Himaya ya Warumi, ambayo baadaye ilisambaratika. Lakini imani yetu imebaki.
Amemalizia kwa kusema:
Tukio hili na tukio la mauaji ya Padre Mushi, isiwe sababu ya kuacha amani ya nchi yetu isambaratike.
Lakini ni jukumu la wananchi wotte kuhakikisha nchi yetu haisambaratiki.
Wenye mamlaka watimize wajibu wao. Sisi wakristo tusamehe, tusijibu uovu, tudumishe amani na upendo katika taifa letu.
Tumsifu Yesu Kristu.Mazingira haya yanaweka ugumu wa kupata cha kusema. Ila sisi ni watu wa imani. napenda kueleza imani yetu kama tunavyopaswa kuwa kwenye mazingira haya.
Tumejumuika ili kuwaweka kwenye nyumba ya milele hawa marehemu, lakini pia tunatumia nafasi hii kubariki Kanisa.
Kila mbatizwa ni kiungo cha mwili wa Kanisa. Kila kiungo cha mwili kinapaswa kuungana na kichwa cha Mwili ambae ni Yesu Mwenyewe
Kristo akipitia kwa mdomo wa mtume Paulo anatufundisha kuwa "Msijaribu kushindana na uovu kwa uovu, lakini shindeni uovu kwa wema".
Katika viongozi waanzilishi wa dini, ni Yesu peke yake aliyetolea uhai wake kujenga imani ya wafuasi wake. Viongozi wengine hawajikutoa sadaka wenyewe, na baadhi wametoa sadaka ya maisha ya watu wengine kwa ajili ya kueneza imani yao.
Sisi Wakristu Imani yetu inajengwa juu ya mwanzilishi wetu ambaye alitoa uhai wake ili kujenga imani yetu, na hakutoa uhai wa mtu yeyote kwa ajili ya kujenga imani yetu.
Katika masomo tuliyosikia leo, Somo la plili limetupa neno la Mtume Paulo Rum:12:17 linasisitiza hilo: usishinde uovu kwa uovu, bali shinda uovu kwa wema.
Soma la Kwanza limeeleza kuwa Paulo na Sila wanateswa kwa ubaya mkubwa sana na kuwekwa gerezani kwa ubaya. Na baada ya kufunguliwa kwa muujiza, askari wa magereza alitaka kujiua, lakini Paulo na Sila wakatenda lililo jema kuokoa maisha yake. Ni baada ya wema huo wokovu ulifika kwa askari huyo na jamaa yake yote wakaweza kumwamini Mungu.
Nawauliza waumini: "Wale waliotekeleza ubaya huu, akija mbele yetu akasema ni mimi ndiye, tungefanya nini kama waumini kwa kufuata mfano wa Yesu?"
Mimi nawaambia "Tujifunze kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo: 'Tusidiriki kulipia uovu kwa uovu, lakini tutende mema ili kushinda uovu'."
Lakini haya hayaondoi majukumu ya serikali, ambayo yanabaki, na si mimi ninayepaswa kuyasema, wenye mamlaka wanayajua majukumu yao. Mimi nawaambia ninyi waumini.
Uovu si kitu kinachopendeza. Warumi waliwatesa wakristo kwa karne tatu, na haikusaidia chochote Himaya ya Warumi, ambayo baadaye ilisambaratika. Lakini imani yetu imebaki.
Amemalizia kwa kusema:
Tukio hili na tukio la mauaji ya Padre Mushi, isiwe sababu ya kuacha amani ya nchi yetu isambaratike.
Lakini ni jukumu la wananchi wotte kuhakikisha nchi yetu haisambaratiki.
Wenye mamlaka watimize wajibu wao. Sisi wakristo tusamehe, tusijibu uovu, tudumishe amani na upendo katika taifa letu.
==================
Update Neno la Askofu Malasusa
==================
Tunaagana na ndugu zetu katika mwili.
Ni ibada yenye majonzi lakini ni yenye furaha kwa kuwa ndugu zetu wamelala katika imani na wataupata uzima wa milele.
Natoa pole kwa wafiwa na kwa Baba Askofu Lebulu.
Yesu yu hai nasi tunaomwamini tutakuwa hai, hata miili itakapoharibika, tutaurithi uzima wa milele.
Kama alivyosema Kardinali tusilipe ubaya kwa ubaya, lakini tusiwe waoga. Tumtangaze bila woga. Tuelewe pia kuwa hatutahukumiwa tu kwa maovu tuliyotenda bali hata kwa mema ambayo hatukuyatenda
Risasi wanazopigwa watumishi wa Mungu, mioto ya kuchoma makanisa, mabomu wanayotupiwa waumini, yasitukatishe tamaa.
Askofu Malasusa anaseama pia: Anatamani kama angefariki katika ibada kama marehemu hawa. Heri wafu wafao katika Bwana.
==================
Update: Salamu za Waziri Mkuu
==================
Ni siku ya majonzi, lakini ni siku ya kuwaombea ndugu zetu marehemu.
Tukio hilo limetokea, tuwaombee ndugu zetu marehemu.
Kwa niaba ya Rais na serikali yote, nawapa pole, naungana na wafiwa na kuwaomba wajitahidi kubeba msiba huu.
Anawapa pole waumini wa Olasiti. Tukio limetokea katika mazingira yasiyotarajiwa. Waliokuwepo tukio hilo limewashtua na bila shaka litabaki.
Anamshukuru Baba Paroko. Alipomtembelea alifarijika kwa maneno yake ambayo leo yamesemwa tena na Kardinali.
Anatoa pole kwa Baba Askofu Mkuu Josephat Lebulu, Mungu ampe nguvu ya kuendelea kuongoza waamini.
Kwa Mwadhama Kardinali, pole tena. Kwa kuwa jambo hili limetokea katika kanisa katoliki.
Anawaombea viongozi wote wa dini wasikate tamaa.
Anasema kuwa ni kujidanganya kudhani kuwa ukiua muumini mmoja utaua ukristu, Haitawezekana.
Hawa waovu wachache, serikali tutawasaka na kuchukua hatua za kisheria. wanajua kuwa kwa hatua ya sasa, hawataweza kufuta ukristo kwa njia hiyo.
Ukristo na uislamu zina historia ndefu. Tutajidanganya kuwa mufti akiuawa ukristo utauliwa.
Serikali itashugulikia kikamilifu kundi ambalo lengo lao ni kuharibu amani yetu Tanzania. Wanataka tushindwa kuishi kwa amani. tusikubali tufikie hapo.
Anasema tumeagiza vyombo vyote husika vifanye kazi kuhakikisha utulivu na amani vinaendeleza. kamata kamata zitaongezeka. Lakini ni kwa kuondoa hali hii inayotishia usalama wetu.
Anaomba ushirikiano wa wananchi wote. Waovu wako miongoni mwetu.
Tutaisaidia sana serikali tukiwajulisha waovu hao. Ametoa rambi rambi Sh 100 milioni.
====================================
Update: Neno la Shukrani toka Askofu Mkuu Lebulu
====================================
Kwa niaba ya mapade, watawa, walei wote alitoa pole kwa familia ya kanisa la Arusha.
Kwa msiba huu anasema Wakristu tunajiuliza Mungu una ujumbe gani kwetu?
Alitoa pole, kwa ndugu za marehemu watatu. Alitoa pole kwa wafiwa na kusema hakika tumeguswa sana na hata hatuna maneno ya kuelezea, tuliwatembelea mahospitalini na hakika watu wa Mungu wameumizwa sana. Pole sana kwa waumini wa kanisa hili na wakaazi wa eneo hili. Alisisitiza Tusikate tamaa!
Alitoa pole kwa wanafamilia ya Mungu wa Olasiti waliokuwa kwenye siku yao ya furaha ya kufungua parokia yao.
Alitambua majitoleo waliyofanya wana Olasiti kwa kumjengea Mungu nyumba. Walijenga nyumba ya Mungu kwa nguvu zao bila ufadhili toka nje. Wakati wanataka kumtolea Mungu shukrani zao wamekatishwa, lakini hakuna kukata tamaa.
Alitoa shukrani kwa wale walioonesha moyo wa utu kulaani unyama ule.
Aliishukuru serikali ya wilaya, mkoa na serikali kuu waliokuwa pamoja katika msiba huu. Na anamshukuru Waziri mkuu kwa uwepo.
Anashukuru na Serikali ya Zanzibar kwa moyo wa utu, kwamba walimtembelea na waliwafariji wakristo wote wa Arusha.
Aliwaambia waumini Msiogope! Kristo akiwa upande wetu hakuna atakayetushinda.
Kristo ametuambia katika Injili ya Yohane: Msifadhaike mioyoni mwenu, mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Yesu aliwaambia pia Msiogope. Mkijua mafundisho yangu, mtaujua ukweli na ukweli utawaweka huru.
Anasema yeye kama baba anawaambia, lazima ifikie mahali tuseme INATOSHA, Tumwambie Mungu IMETOSHA. Wenye nguvu na silaha watatushinda, lakini tukiwa na Mungu hatutashindwa. Paulo na Sila walisali Milango ya gereza ikafunguka.
Tusali kwa nguvu zote.
Alimaliza kwa kuwaaga marehemu akiwataja kwa majina na kumwambia kila mmoja kwa heri!
================
- Rais wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa aliyeitaka Serikali kutumia msamiati wa mwenye macho haambiwi tazama na kukomesha mpasuko wa kidini aliosema unalitafuna taifa.
Watu watatu, waliofariki katika shambulio la bomu katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti, mkoani Arusha wamezikwa jana na mamia ya watu, huku ulinzi ukiwa umeimarishwa kuliko kawaida na viongozi wa dini na Serikali kutoa kauli nzito. Marehemu hao, ni Regina Loning'o Laizer (45), James Gabriel(16) na Patricia Joachim Assey(9) walizikwa katika eneo la kanisa hilo Katoliki, mazishi yaliyohudhuriwa na maaskofu wanane wa majimbo tofauti ya Kanisa Katoliki, Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT), Askofu Alex Malasusa, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na viongozi mbalimbali wa dini, Serikali na kisiasa.
Kauli za viongozi
Rais wa (TEC), Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa
Katika ibada hiyo ya viongozi mbalimbali wa kidini, walitoa salama zao akiwamo Rais wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa aliyeitaka Serikali kutumia msamiati wa mwenye macho haambiwi tazama na kukomesha mpasuko wa kidini aliosema unalitafuna taifa.Mkuu wa Kanisa la KKKT, Askofu Dk Alex Malasusa
Askofu huyo alisema kuwa miongo mitatu sasa, Serikali imekaa kimya, ikishuhudia mafundisho na mihadhara ya kidini inayochochea na kuhamasisha uhasama kati ya Ukristo na Uislamu, bila kuchukua hatua kukomesha hali hiyo. "Matukio mbalimbali yanayoashiria uhasama wa kidini yanayotokea nchini. Kuna mihadhara, CD, DVD, machapisho na mafundisho yanayotishia maisha na usalama wa viongozi wa kanisa na waumini wao, ambayo yamefuatiwa na uchomomaji wa makanisa," alisema Askofu Ngalalekumtwa.
Alitaja mfano wa kongamano la Januari 15, mwaka juzi iliyofanyika Ukumbi wa Diamond Jubillee jijini Dar es Salaam kuwa moja ya mikutano iliyojaribu kuchochea chuki ya kidini kati ya Waislamu na Wakristo kwa kudai kuwa Serikali ya Tanzania inaongozwa kwa mfumo Kikristo ulioasisiwa na Hayati Mwalimu Julius Nyerere.
Askofu huyo alisema kwamba katika kongamano hilo, washiriki waliaminishwa kuwa Serikali inatoa fedha za ruzuku kujenga shule na taasisi za kanisa kutokana na kuwapo mkataba maalumu kati ya kanisa na Serikali, jambo ambalo siyo kweli. "Kinachosikitisha zaidi ni kwamba Serikali haikukanusha madai na uchochezi huo, licha ya mambo hayo kufanyika na kusemwa hadharani kwa wahusika kuzunguka nchi nzima kueneza chuki na uchochezi huo," alisema Askofu Ngalalekumtwa.
Alisema kuwa tukio la Arusha ni la kikatili na aibu kwa taifa akiwataka wenye dhamana ya ulinzi na usalama kuchukua hatua kudhibiti hali hiyo akionya kuwa wasipofanya hivyo watahukumiwa kwa kosa la kukaa kimya mambo yakiharibika mikononi mwao. "Wote wenye jukumu la kulinda na kuitunza amani waifanye kazi hiyo bila uoga. Wasipofanya hivyo iko siku watahukumiwa," alisema Dk Malasusa.
Mwakilishi wa Muungano wa Madhehebu ya Kikristo mkoani Arusha, Askofu Stanley Hotay
Aliwataka viongozi wa kisiasa kuepuka kutumia jukwaa la dini kutimiza malengo ya kisiasa, akionya kuwa makanisa hayana itikadi, bali waumini ndiyo wenye itikadi mbalimbali. "Sote tuliomo ndani ya jahazi lazima tuwakemee na kuwadhibiti vichaa wanaojaribu kutoboa jahazi letu kwani tusipofanya hivyo maji yatajaa ndani, chombo kitazama na sote tutaangamia," alisema Askofu Hotay.
Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo
Ibada hiyo iliyohudhuriwa pia na baadhi ya viongozi wa dini ya Kiislamu, ilioongozwa na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo aliyetoa wito kwa waumini wa kanisa hilo, kutolipiza kisasi, akisema kuwa waliohusika ni watu wasiofuata dini. "Tusilipize uovu kwa uovu, yapaswa kushinda uovu kwa wema…; Tuache kunyoosheana kidole kutokana na tukio hili," alisema Kardinali Pengo. Pengo ambaye hivi karibuni, alinukuliwa na vyombo vya habari akieleza kuwa shambulio hilo halina uhusiano na masuala ya kidini hasa kutokana na taarifa za uhakika alizopewa akisema waliotekeleza shambulio hilo ni waovu wenye nia ya kuligawa taifa na kuliingiza katika migogoro ya kidini.
Mbowe, James Mbatia mingoni mwa wanasiasa waliohudhuria
Viongozi wa kisiasa waliohudhuria ni pamoja na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia na wabunge kadhaa.
Salamu za Serikali - Waziri Mkuu Pinda
Akitoa salamu za Serikali katika ibada hiyo ya mazishi, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alitoa pole kwa tukio hilo akaeleza kuwa yoyote anayedhani kuua muumini mmoja, Askofu au Mufti ataua Ukristo au Uislamu, hajui kuwa hiyo haitawezekana. Pinda alisema Serikali imetoa Sh100 milioni ikiwa ni rambirambi zake akiongeza kuwa dini za Kikristo na Kiislamu zina historia ndefu duniani. "Itakuwa ni kujidanganya kuwa ukiua kiongozi wa dini leo utaifuta dini hiyo, kwani kwa kuamini hivyo hiyo ni ndoto," alisema Pinda.
Waziri Mkuu, alisema kwamba Serikali imeagiza vyombo vyote vya usalama nchini, vifanye kazi usiku na mchana kuhakikisha amani na utulivu unaendelezwa nchini. Aliwataka Watanzania kuwa watulivu, hasa watakaposikia kamatakamata inaendelea na kueleza kuwa lengo la hatua hiyo ni kulinda amani ya nchi.
Ulinzi waimarishwa
Ulinzi uliimarishwa eneo lote kuzunguka kanisa hilo, barabara za kuingia Parokia hiyo na katikati ya Jiji la Arusha. Maofisa wa Polisi na Usalama kutoka makao makuu jijini Dar es Salaam na Maofisa Usalama wa Taifa kutoka maeneo mbalimbali waliimarisha ulinzi. Askari wenye silaha za moto na mabomu, waliranda juu ya kanisa hilo kwa kupeana zamu, huku baadhi wakiwa na miwani na kuona mbali. Maeneo mengine askari wanafunzi wa Chuo cha Polisi Moshi, walikuwa wameimarisha ulinzi na kuwapekua waliowatilia shaka
Mapadre wa Arusha wakiwa wamebeba jeneza la mtoto Patricia.
Mapadre wakiwa wamebeba jeneza la mama Regina Laizer
Mapadre na Maaskofu mbele ya majeneza yaliyobeba miili ya marehemu wakati Askofu Lebulu anayabariki mara baada ya kuingia kanisani.
Askofu Lebulu akiwa ananyunyizia maji ya Baraka. Kulia ni Paroko wa Parokia hiyo. Kushoto kabisa ni Maaskofu Amani, Askofu Nkwande, Askofu Dallu, na aliyeshika fimbo yenye msalaba Kardinali Pengo.
Kardinali Pengo akisali sala, pamoja na Askofu Mkuu Josephat Lebulu