JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,321
- 5,490
Naomba ujumbe huu mfupi tu uwafikie wanaohusika kuwa hapa kwenye Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli (Magufuli Bus Terminal), upande wa jengo la abiria na sehemu nyingine kadhaa hakuna umeme.
Leo ni siku ya pili sasa hali bado ni tete, hakuna umeme na usiku usalam wa abiria unakuwa shakani, wale ambao wanalala stendi au wanakuwepo kwa ajili ya upanda abasi ya usiku.
Jengo la Utawala umeme upo, sisi wafanyakazi tuliopo hapa hata sisi pia tunahofu juu ya usalama wetu, vibaka wapo kama wote wanasoma mchezo.
Naamini ujumbe huu ukiwafikia viongozi wetu kupita JF watashughulikia mapema.
Hii ni stendi kubwa kuliko zote za mabasi nchini lakini inatia aibu kwa kukosa huduma ya umeme.
Leo ni siku ya pili sasa hali bado ni tete, hakuna umeme na usiku usalam wa abiria unakuwa shakani, wale ambao wanalala stendi au wanakuwepo kwa ajili ya upanda abasi ya usiku.
Jengo la Utawala umeme upo, sisi wafanyakazi tuliopo hapa hata sisi pia tunahofu juu ya usalama wetu, vibaka wapo kama wote wanasoma mchezo.
Naamini ujumbe huu ukiwafikia viongozi wetu kupita JF watashughulikia mapema.
Hii ni stendi kubwa kuliko zote za mabasi nchini lakini inatia aibu kwa kukosa huduma ya umeme.