Hii game ya Usma na Berkane itakuwa kipimo tosha Cha uhuru wa CAF ya Motsepe

Kwa wasioelewa Hawa watu washaleta siasa kwenye mpira, Kuna eneo ambalo Morocco na Algeria wamekua wakiligombania muda mrefu, limekua likileta utata kwenye mipaka Yao mpaka Leo hakuna suluhu, sasa berkane(ya Morocco) kwenye jezi Yao wameweka ramani ya Morocco(sijui kwanini sasa au ndo chokochoko) inayoonyesha Ramani nzima ya Morocco ikiwepo na Hilo eneo linalogombaniwa na Algeria,


CAF walishaipitisha hii jezi kama official kit ya berkane, sasa walipokutana na usm Alger ya Algeria, walioenda Algeria mechi ya kwanza ugenini, serikali ya Algeria wakazizuia jersey za berkane zisitumike, waliona kama watakua wanakubali kushindwa, kwanini wawaruhusu berkane waonyeshe ujumbe kwenye jersey zao wakiwa wameweka ramani ya Morocco ikijumuisha na lile eneo ambalo bado wanaligombania.


Berkane wakasema hawawezi kuingia uwanjani hawana jersey maana jersey zao serikali imezichukua, mechi haikuchezwa, CAF wakawapa berkane ushindi wa mezani 3-0, Jana napo usm kagoma kuingiza timu uwanjani
Daaah!! Wenzetu weupe hakika WANA MISIMAMO THABITI HASA.

INgekuwa hapa kwetu tungeacha tu kwa kigezo cha UTULIVU NA AMANI
 
Ni jambo zito kuliko watu wengi wanavyo fikiri. Kwa mfano tumekuwa na kutokuelewana na Malawi, sasa chukulia timu ya Malawi inacheza na moja ya timu zetu za Kariakoo halafu waweke ramani kwenye jezi zao inayoonesha ziwa Nyasa lipo kwao. Kamwe serikali haiwezi kubali hiyo jezi itumike na ikiruhusu wananchi wataidharau sana hiyo serikali. Moja ya sababu ya Morocco kujitoa OAU kipindi kile ilikuwa ni huu mgogoro wao na Algeria, ukiwa nje unaweza ona ni issue ndogo lakini kumbe ni kubwa sana. Nafikiri CAF ndio wenye makosa kuruhusu jezi kuwa na ramani ambayo ina mgogoro na haya ni kinyume na taratibu za FIFA
Nami nakubali Caf ndio wenye shida jersey zinaweza kuwa na bendera ila sio ramani
Endapo Caf walijua kuwa hii jersey italeta shida walipaswa kuzuia isitumike kwa Algeria mi naona wako sawa
 
Mbona tayari USM Algers alishapokonywa point 3 na magoli matatu na hao hao caf baada ya mechi ya kwanza kule Algeria?
Sheria za mpila zipo wazi sana kiasi ambacho nyeupe huwezi kuiita nyeusi
Hata mtoano unapora mtu points? Hawa caf hawana akili toka lini mtoano ukawa na points?
 
Kwa wasioelewa Hawa watu washaleta siasa kwenye mpira, Kuna eneo ambalo Morocco na Algeria wamekua wakiligombania muda mrefu, limekua likileta utata kwenye mipaka Yao mpaka Leo hakuna suluhu, sasa berkane(ya Morocco) kwenye jezi Yao wameweka ramani ya Morocco(sijui kwanini sasa au ndo chokochoko) inayoonyesha Ramani nzima ya Morocco ikiwepo na Hilo eneo linalogombaniwa na Algeria,


CAF walishaipitisha hii jezi kama official kit ya berkane, sasa walipokutana na usm Alger ya Algeria, walioenda Algeria mechi ya kwanza ugenini, serikali ya Algeria wakazizuia jersey za berkane zisitumike, waliona kama watakua wanakubali kushindwa, kwanini wawaruhusu berkane waonyeshe ujumbe kwenye jersey zao wakiwa wameweka ramani ya Morocco ikijumuisha na lile eneo ambalo bado wanaligombania.


Berkane wakasema hawawezi kuingia uwanjani hawana jersey maana jersey zao serikali imezichukua, mechi haikuchezwa, CAF wakawapa berkane ushindi wa mezani 3-0, Jana napo usm kagoma kuingiza timu uwanjani
USM hana sababu, ameshapigwa tayari
 
Kwa wasioelewa Hawa watu washaleta siasa kwenye mpira, Kuna eneo ambalo Morocco na Algeria wamekua wakiligombania muda mrefu, limekua likileta utata kwenye mipaka Yao mpaka Leo hakuna suluhu, sasa berkane(ya Morocco) kwenye jezi Yao wameweka ramani ya Morocco(sijui kwanini sasa au ndo chokochoko) inayoonyesha Ramani nzima ya Morocco ikiwepo na Hilo eneo linalogombaniwa na Algeria,


CAF walishaipitisha hii jezi kama official kit ya berkane, sasa walipokutana na usm Alger ya Algeria, walioenda Algeria mechi ya kwanza ugenini, serikali ya Algeria wakazizuia jersey za berkane zisitumike, waliona kama watakua wanakubali kushindwa, kwanini wawaruhusu berkane waonyeshe ujumbe kwenye jersey zao wakiwa wameweka ramani ya Morocco ikijumuisha na lile eneo ambalo bado wanaligombania.


Berkane wakasema hawawezi kuingia uwanjani hawana jersey maana jersey zao serikali imezichukua, mechi haikuchezwa, CAF wakawapa berkane ushindi wa mezani 3-0, Jana napo usm kagoma kuingiza timu uwanjani
Maelezo yamenyooka sana, sasa hao USM nao wametoa sababu gani ya kutoingiza timu uwanjani! Hawajaenda kabisa Morocco au vipi!?
 
Maelezo yamenyooka sana, sasa hao USM nao wametoa sababu gani ya kutoingiza timu uwanjani! Hawajaenda kabisa Morocco au vipi!?
Mkuu wao hawaafiki kitendo Cha berkane kupewa ushindi wa 3-0 mezani, hata we ungeingiza timu kutafuta goli nne za jasho? Wakati mwenzako kapewa ya bure

Msimamo wa usm Alger ni kua mambo ya serikali hayamuhusu
 
Mkuu wao hawaafiki kitendo Cha berkane kupewa ushindi wa 3-0 mezani, hata we ungeingiza timu kutafuta goli nne za jasho? Wakati mwenzako kapewa ya bure

Msimamo wa usm Alger ni kua mambo ya serikali hayamuhusu
Kweli ni ngumu kwenda kutafuta magoli manne. Kwa hiyo hawajaenda kabisa Morocco au sio
 
Wazee mmeandika uongo..ishu ipo hivi Algeria anaishutumu Morocco kusupport maseparist kwenye eneo la kybilia ambalo lipo ndani ya mipaka ya Algeria kwa kulipiza Algeria nae anaunga mkono uhuru kamili wa Jimbo la western Sahara ambalo Morocco anadai ni lake..
IMG_20240429_184504.jpg
 
Namaanisha ile mechi ya kwanza kule Algeria CAF waliwalima magoli matatu na kuwapa Berkane, swali langu kosa la USMA lilikuwa nini?
Mi nadhani hapa ndio siasa za Caf ziliingia
Kosa la USMA ni kwamba jersey za Berkane zilizuiwa maana zilikuwa na bendera ambayo ni ishara mbaya kwa upande wa Algeria kutokana na migogoro Yao
Mamlaka za Algeria zikawaambia Berkane watafute jersey zingine wakagoma na hivyo hawakuweza kuingia uwanjani Caf wakawapa ushindi Berkane ambao hawakuingia uwanjani maana jersey zao zilitaifishwa kwa kuwa na ujumbe ambao sio mzuri kwa Algeria
Kuja huku Morroco USM wakagoma kuja nadhani Berkane atapewa ushindi acheze na Zamaleki
Ni upuuzi wa Afrikan football
 
Back
Top Bottom