Angalia nyendo zako usije kuwa deleted

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Aug 6, 2020
3,663
6,896
Hivi karibuni nimehamia Mkoa fulani katika harakati za utafutaji, kama unavyojua maisha popote pale maadam unapambania mkate wa kila siku.

Siku kadhaa zilizo pita nikiwa naelekea katika harakati zangu njiani nikakutana na gari imepaki,nje kulikuwa na mwamba mmoja anafuta bastola yake kwa kitambaa na huku mwengine anafungua mlango wa nyuma wa gari

Na ile bastola ina kiwambo cha kuzuia sauti isitoke, wapenda movie kama mimi nadhani mmeshawa kuziona hizi bastola,,, kwa mtazamo wangu ama jamaa alishampiga mtu risasi ndo wamtupe porini au ndo alikuwa katika maandalizi ya kumpiga risasi,,, tulikuwa kwenye Boda Boda tukapita kama kishada kwakuwa hatukutaka ushahidi au kuwa miongoni mwa wahanga,, maana ishu kama hizo hamkawii na nyinyi kupotezwa ili kuondoa ushahidi


Ninachotaka kusema hapa watu huwa hawapotezwi bila sababu lazima kuwe na jambo ambalo litapelekea waweze kupotezwa na wahusika

Na mambo haya mara nyingi huwa ni kudhulumiana katika biashara au mambo ya kutembea na wake za watu au uanaharakati fulani hivi ambao unagusa maslahi ya watu na mambo kama hayo.

Haya mambo yanafanyika duniani kote, na kuna watu ambao ni wakali wa hayo
mambo yani simu moja tu wanafanya kazi chap.

Kubwa ni kujitahidi kadri ya uwezo wako kuepukana na mambo hayo ambayo kwa namna moja au nyingine inaweza kukufanya ukawa deleted chap

Kumbuka kunguru muoga huficha mbawa zake, jiepushe na vihatarishi vyote ambavyo vinaweza kuwa sababu ya kupotezwa.

Ni hayo tu!
 
Umepita na boda boda kama kishada kwa mwendo wa roketi, lkn umeweza kuchunguza bastora ukaona ina kiwambo cha kuzuia sauti na ukachunguza idadi ya watu kwenye gari. Anyway JF riwaya zimekuwa nyingi
Sio ule mwendo mkali kivile chief,,, baada Ya kuwakaribia ndio tukaona hiyo ishu so tukaongeza wese,,, trust me chief
 
Hii ni chai
FB_IMG_17136160440648760.jpg
 
Hivi karibuni nimehamia Mkoa fulani katika harakati za utafutaji,,, kama unavyojua maisha popote pale maadam unapambania mkate wa kila siku.

Siku kadhaa zilizo pita nikiwa naelekea katika harakati zangu njiani nikakutana na gari imepaki,nje kulikuwa na mwamba mmoja anafuta bastola yake kwa kitambaa na huku mwengine anafungua mlango wa nyuma wa gari

Na ile bastola ina kiwambo cha kuzuia sauti isitoke,,, wapenda movie kama mimi nadhani mmeshawa kuziona hizi bastola,,, kwa mtazamo wangu ama jamaa alishampiga mtu risasi ndo wamtupe porini au ndo alikuwa katika maandalizi ya kumpiga risasi,,, tulikuwa kwenye Boda Boda tukapita kama kishada kwakuwa hatukutaka ushahidi au kuwa miongoni mwa wahanga,, maana ishu kama hizo hamkawii na nyinyi kupotezwa ili kuondoa ushahidi


Ninachotaka kusema hapa watu huwa hawapotezwi bila sababu lazima kuwe na jambo ambalo litapelekea waweze kupotezwa na wahusika

Na mambo haya mara nyingi huwa ni kudhulumiana katika biashara au mambo ya kutembea na wake za watu au uanaharakati fulani hivi ambao unagusa maslahi ya watu na mambo kama hayo.

Haya mambo yanafanyika duniani kote, na kuna watu ambao ni wakali wa hayo
mambo yani simu moja tu wanafanya kazi chap.

Kubwa ni kujitahidi kadri ya uwezo wako kuepukana na mambo hayo ambayo kwa namna moja au nyingine inaweza kukufanya ukawa deleted chap

Kumbuka kunguru muoga huficha mbawa zake,,,, jiepushe ni vihatarishi vyote ambavyo vinaweza kuwa sababu ya kupotezwa.

Ni hayo tu!
Bodaboda ilisimama mkaangalia jinsi jamaa anavyofuta Bastola..Tupe na Chapati Mbili mkuu chai tu sio Fair
 
Back
Top Bottom