Hoja za Utanganyika na Uzanzibari ni Hoja Muflis za Ujinga wa Ukosefu Elimu ya Uraia. Tuwatoe Ujinga Huu Kwa Elimu ya Uraia au Tuwaache na Ujinga Wao?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,714
114,046
Wanabodi

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na kwa Maslahi ya Taifa, kila Jumatano kwenye gazeti la Mwananchi na Jumapili kwenye gazeti la Nipashe na kwenye kipindi cha KMT on Channel Ten TV, kila siku za Jumapili saa 3:00 usiku na marudio Jumatano saa 9:30 alasiri.

Hoja ya leo ni hoja za Utanganyika na Uzanzibari ambazo ni hoja muflis zinazosababishwa watu wanaitwa vitimbakwiri kujivunia uraia ambao haupo kutokana na ujinga tuu wa ukosefu wa elimu ya uraia kuhusu uraia wa Tanzania. Kwenye uraia, hakuna Mtanganyika wala Mzanzibari, tuna uraia mmoja tuu, Mtanzania. Swali ni jee tuwatoe ujinga hawa vitimbakwiri muflis wanaotaka kutubagua kwa Utanganyika na Uzanzibari kwa kuwaelimisha elimu ya uraia, au tuwaache tuu na ujinga wao kujisikia sifa kujinasibisha na kujivunia Utanganyika na Uzanzibari?.

Hili ni Nipashe la Leo.
20240519_171120.jpg


Ukosefu wa Elimu ya Uraia Kuhusu Katiba, Sheria, Haki na Wajibu, ndio umesababisha, huu ubaguzi wa Utanganyika, na Uzanzibari, watu wakielimishwa kuhusu uraia, hawa vitimbakwiri muflis wanaoleta ujinga wa ubaguzi wa kunyoosheana vidole vya Utanganyika na Uzanzibari, ujinga huu utawatoka, wataerevuka na tutakuwa na Utanzania pekee!.

Hivi karibuni, kumeibuka hoja za kibaguzi za baadhi ya wanasiasa, kutoa kauli za kibaguzi za kuwanyooshea watu vidole na kuwaita “Wao Wazanzibari”, “Sisi Watanganyika”. Miongozi mwa watu wanaotoa kauli hizo ni baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, waliofilisika kisiasa, na baadhi ya wanaolaani kauli hizo, ni baadhi ya viongozi wa chama tawala, ambapo nimemsikia mmoja wa viongozi hao, akilaani vikali kauli hizo bungeni kwa maneno makali kabisa!, huko pia ni kufilisika kisiasa.

NB. Aliyesema wanasiasa wanaojinasibisha na Utanganyika na Uzanzibari, dini zao, kanda zao, au kabila zao, ni watu muflis, waliofilisika kisiasa, sio mimi ni Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, na akaiandikia kitabu kinaitwa “Nyufa”. Mwalimu alisema dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana, ni kama kula nyama ya mtu, ukiishakula huwezi kuacha!.

Uraia ni hoja ya kikatiba na kisheria. Kabla ya Muungano, tulikuwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar, hivyo tulikuwa na uraia wa Tanganyika, na uraia wa Zanzibar. Baada ya muungano, tukaungana kuwa nchi moja ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwa na uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania.

Baada ya Muungano, majina ya nchi hizi zote mbili, nchi ya Tanganyika, na nchi ya Zanzibar, yalibadilika na kuwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, hivyo jina la Tanganyika likafutwa, ila jina la Zanzibar, liliendelea kuwepo, kutokana na uadimu na uadhimu wa huu muungano wetu.

Uadimu wa Muungano
Miungano ya nchi zote duniani ni miungano ya aina mbili kuu,

1. Muungano wa Union, ambapo nchi mbili zinaungana na kuunda nchi moja. Zile nchi zote mbili zilizoungana , zote zinakufa na kuunda nchi moja mpya. Hivyo ndivyo ulivyo muungano wetu kimataifa, ni muungano wa Unioni, ile nchi ya Tanganyika imekufa, ile nchi ya Zanzibar imekufa, imezaliwa nchi moja mpya ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye urais mmoja tuu, uraia wa Tanzania. Hakuna tena uraia wa Tanganyika, wala uraia wa Zanzibar, kuna uraia mmoja wa Tanzania. Tanganyika haipo nafasi yake imechukuliwa na Tanzania Bara, na Zanzibar japo ipo, ila sio nchi ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye utawala wake wa ndani, lakini hakuna uraia wa Zanzibar, uraia ni mmoja tuu wa Tanzania.

2. Muungano wa Federation, ni nchi mbili au zaidi, zinaungano kuwa nchi moja, lakini zile nchi zote mbili zinaendelea kuwa utawala wake wa ndani, na serikali zao, chini ya utawala mkuu wan chi ya federal state, kama Marekani. Vivyo hivyo muungano wetu kwa ndani ya muungano ni muungano wa federation yenye nchi mbili, Tanzania na Zanzibar, yenye marais wawili, Rais wa JMT “mwenye R kubwa, na rais wa Zanzibar mwenye r ndogo, zenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya SMZ, mabunge mawili, Bunge la JMT na BLW, na zenye mahakama mbili, Mahakama ya JMT na Mahakama ya Zanzibar, ila kwenye uraia, bado ni uraia mmoja tuu wa JMT, ila kwa Zanziar, wana ukaazi, ule ukaazi sio uraia ni utambulisho tuu wa wakaazi wa Zanzibar lakini wote ni Watanzania.

Hivyo muungano wa Tanzania ni muungano adimu pekee duniani ambao kwa upande mmoja ni muungano wa union na upande wa pili ni muungano wa federation, hakuna muungano wa aina hii popote duniani.

Uadhimu wa Muungano.
Muungano wetu licha ya kuwa ni muungano adimu, pia ni muungano adhimu, wenye dhima ya kuungana milele!. Miungano yote duniani unaundwa kwa mikataba ya kisheria ya muungano. Mikataba hiyo inakuwa na kipengele cha jinsi ya kuivunja miungano hiyo. Kwenye zile Articles of Union za Muungano wetu, hakuna kipengele cha jinsi ya kuuvunja, muungano, hivyo zile Hati za Muungano sio mkataba wa muungano, ni makubaliano ya muungano, (not a contract, but an agreement) yenye dhima ya muungano wa milele, na ndio maana tunasema “muungano tutaulinda kwa gharama yoyote”.

Tangu tumeungana, na mimi tangu nimezaliwa na kupata akili, sikumbuki hata mara moja, kusikia vipindi vya elimu ya uraia kuhuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, hali inayopelekea Baadhi ya Watanzania kuanza kujinasibisha na Utanganyika wao, na Uzanzibari wao.

Kwa vile Tanganyika ilifutwa na jina la Tanganyika kufutwa, utanganyika nao ukafutika, Watanganyika tunajisabisha kwa Utanzania wetu, lakini kwa vile kwa vile jina la Zanzibar, halikufutwa, na kuna Uzanzibari ukaazi, hivyo baadhi ya Wanzanzibari, wanajinasibisha kwa Uzanzibari wao kama uraia wa Zanzibar, badala ya kujinasibisha na Utanzania wao, kungekuwa na vipindi vya elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria, haki na wajibu, kusingekuwepo, vitimbakwiri wowote, wanaojinasibisha kwa Utanganyika wao, au Uzanzibari wao kwasababu, uraia wa JMT ni uraia mmoja tuu, hakuna uraia wa Tanganyika, wala hakuna urais wa Zanzibar, kuna uraia mmoja tuu, uraia wa JMT.

Wiki ijayo, nitaendelea na kuwaletea hizi chokochoko za kuuchokoa muungano na kuanza kunyoosheasha vidole vya ubaguzi wa “Utanganyika na Uzanzibari” zilianzia wapi, dawa yake ni nini na tiba ya kudumu ya kuitibu sumu hii na kuiangamiza kabisa.

View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=fPhb1_0doZmgD7T4
Wakati huo huo, naendelea na darasa langu la elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria na haki on Channel Ten kila Jumapili saa 3:00 usiku.
Karibuni.

Paskali
 
Nafikiri mada yako ingejikita kwanini wanasiasa wanatumia hoja ya utanganyika na Zanzibar.
Hoja kuu aliyotumia mwalimu Nyerere kuzima hoja ya G55 mwaka 95 ni kwa sababu wale walikuwa wabunge wa ccm, na sera ya CCM ilikuwa serikali mbili hivyo hoja yao ilikuwa batili kwani ilitakiwa ianzie ndani ya chama.
Kwanini watanganyika wanadai serikali yao?
Sababu kuu ni uvunjanji wa katiba unaofanywa na viongozi wakati CCM ambayo inaunda serikali imejaa kimya.
Hivi rais wa Zanzibar anapata wapi mamlaka ya kugawa uraia.
Rais Samia alitumia vigezo vipi kuongeza kiwango cha asilimia ya misaada kwenda Zanzibar .
Kwanini serikali ya Zanzibar haichangii gharama za kuendesha muungano lakini wakati huo huo wanapata asilimia 2 ya mapato ya muungano, wanapata mapato ya payee ambayo hawachangii hata senti tano.
Kwanini wazanzibar wanaajiriwa kwenye nafasi zisizo za muungano Kama mkuu wilaya, waziri wa uchukuzi na katibu wake na wameshiriki kuuza bandari za Tanzania bila kuzigusa za Zanzibar.
Time ya Nyalari, tume ya jaji Kissanga na tume ya Warioba zote zilipendekeza serikali tatu nao walikuwa wajinga.
Kwanini Tanganyika ndio ibebe gharama ya muungano zaidi wakati Zanzibar ndio wanufaika wakubwa.
Zanzibar waliondoka kinyemela swala la gesi na mafuta kinyemela baada ya kuhisi wao Wana vitu hivyo na uongozi wa rais wa muungano atakuwa mtanganyoka Ila tumeona Samia mkataba wake wa kwanza akiwa rais wa muungano ulikuwa wa gesi kwenda Kenya.
Ni swala la muda serikali ya Tanganyika kurudi ndio maana jaji Warioba alisema ni heri watanganyika wakapewa serikali yao kabla ya kuidai.
 
Dhumuni la Muungano kwa mawazo ya mwalimu Nyerere ilikuwa ni kujenga nchi moja ambayo ni JMT ( Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania), na ndio mana serikali ya Tanganyika ikajisalimisha kwenye serikali ya JMT mapema sana ila shida imekuwa kwa Hawa ndugu zetu wazanzibar, hawa wanataka kujitenga na JMT, mana mpaka Sasa wanakatiba yao, Wana rais wao, wana mamlaka yao ya mapato , na sisi bara tuna ya kwetu ambayo ni TRA ,
Hii TRA sio Tanzania revenue authority ila ni Tanganyika revenue authority, ndo mana ukinunua bidhaa zenji ukiingia nayo bara unakatwa Kodi,
mana JMT na SMZ sio nchi moja,
Wazanzibar Wana vitambulisho vyao vya uzanzibar.
Lissu, Mbowe wako sawa tuwaunge mkono kuidai Tanganyika yetu
 
Wanabodi

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na kwa Maslahi ya Taifa, kila Jumatano kwenye gazeti la Mwananchi na Jumapili kwenye gazeti la Nipashe na kwenye kipindi cha KMT on Channel Ten TV, kila siku za Jumapili saa 3:00 usiku na marudio Jumatano saa 9:30 alasiri.

Hoja ya leo ni hoja za Utanganyika na Uzanzibari ambazo ni hoja muflis zinazosababishwa watu wanaitwa vitimbakwiri kujivunia uraia ambao haupo kutokana na ujinga tuu wa ukosefu wa elimu ya uraia kuhusu uraia wa Tanzania. Kwenye uraia, hakuna Mtanganyika wala Mzanzibari, tuna uraia mmoja tuu, Mtanzania. Swali ni jee tuwatoe ujinga hawa vitimbakwiri muflis wanaotaka kutubagua kwa Utanganyika na Uzanzibari kwa kuwaelimisha elimu ya uraia, au tuwaache tuu na ujinga wao kujisikia sifa kujinasibisha na kujivunia Utanganyika na Uzanzibari?.

Hili ni Nipashe la Leo.
View attachment 2994081

Ukosefu wa Elimu ya Uraia Kuhusu Katiba, Sheria, Haki na Wajibu, ndio umesababisha, huu ubaguzi wa Utanganyika, na Uzanzibari, watu wakielimishwa kuhusu uraia, hawa vitimbakwiri muflis wanaoleta ujinga wa ubaguzi wa kunyoosheana vidole vya Utanganyika na Uzanzibari, ujinga huu utawatoka, wataerevuka na tutakuwa na Utanzania pekee!.

Hivi karibuni, kumeibuka hoja za kibaguzi za baadhi ya wanasiasa, kutoa kauli za kibaguzi za kuwanyooshea watu vidole na kuwaita “Wao Wazanzibari”, “Sisi Watanganyika”. Miongozi mwa watu wanaotoa kauli hizo ni baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, waliofilisika kisiasa, na baadhi ya wanaolaani kauli hizo, ni baadhi ya viongozi wa chama tawala, ambapo nimemsikia mmoja wa viongozi hao, akilaani vikali kauli hizo bungeni kwa maneno makali kabisa!, huko pia ni kufilisika kisiasa.

NB. Aliyesema wanasiasa wanaojinasibisha na Utanganyika na Uzanzibari, dini zao, kanda zao, au kabila zao, ni watu muflis, waliofilisika kisiasa, sio mimi ni Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, na akaiandikia kitabu kinaitwa “Nyufa”. Mwalimu alisema dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana, ni kama kula nyama ya mtu, ukiishakula huwezi kuacha!.

Uraia ni hoja ya kikatiba na kisheria. Kabla ya Muungano, tulikuwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar, hivyo tulikuwa na uraia wa Tanganyika, na uraia wa Zanzibar. Baada ya muungano, tukaungana kuwa nchi moja ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwa na uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania.

Baada ya Muungano, majina ya nchi hizi zote mbili, nchi ya Tanganyika, na nchi ya Zanzibar, yalibadilika na kuwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, hivyo jina la Tanganyika likafutwa, ila jina la Zanzibar, liliendelea kuwepo, kutokana na uadimu na uadhimu wa huu muungano wetu.

Uadimu wa Muungano
Miungano ya nchi zote duniani ni miungano ya aina mbili kuu,

1. Muungano wa Union, ambapo nchi mbili zinaungana na kuunda nchi moja. Zile nchi zote mbili zilizoungana , zote zinakufa na kuunda nchi moja mpya. Hivyo ndivyo ulivyo muungano wetu kimataifa, ni muungano wa Unioni, ile nchi ya Tanganyika imekufa, ile nchi ya Zanzibar imekufa, imezaliwa nchi moja mpya ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye urais mmoja tuu, uraia wa Tanzania. Hakuna tena uraia wa Tanganyika, wala uraia wa Zanzibar, kuna uraia mmoja wa Tanzania. Tanganyika haipo nafasi yake imechukuliwa na Tanzania Bara, na Zanzibar japo ipo, ila sio nchi ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye utawala wake wa ndani, lakini hakuna uraia wa Zanzibar, uraia ni mmoja tuu wa Tanzania.

2. Muungano wa Federation, ni nchi mbili au zaidi, zinaungano kuwa nchi moja, lakini zile nchi zote mbili zinaendelea kuwa utawala wake wa ndani, na serikali zao, chini ya utawala mkuu wan chi ya federal state, kama Marekani. Vivyo hivyo muungano wetu kwa ndani ya muungano ni muungano wa federation yenye nchi mbili, Tanzania na Zanzibar, yenye marais wawili, Rais wa JMT “mwenye R kubwa, na rais wa Zanzibar mwenye r ndogo, zenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya SMZ, mabunge mawili, Bunge la JMT na BLW, na zenye mahakama mbili, Mahakama ya JMT na Mahakama ya Zanzibar, ila kwenye uraia, bado ni uraia mmoja tuu wa JMT, ila kwa Zanziar, wana ukaazi, ule ukaazi sio uraia ni utambulisho tuu wa wakaazi wa Zanzibar lakini wote ni Watanzania.

Hivyo muungano wa Tanzania ni muungano adimu pekee duniani ambao kwa upande mmoja ni muungano wa union na upande wa pili ni muungano wa federation, hakuna muungano wa aina hii popote duniani.

Uadhimu wa Muungano.
Muungano wetu licha ya kuwa ni muungano adimu, pia ni muungano adhimu, wenye dhima ya kuungana milele!. Miungano yote duniani unaundwa kwa mikataba ya kisheria ya muungano. Mikataba hiyo inakuwa na kipengele cha jinsi ya kuivunja miungano hiyo. Kwenye zile Articles of Union za Muungano wetu, hakuna kipengele cha jinsi ya kuuvunja, muungano, hivyo zile Hati za Muungano sio mkataba wa muungano, ni makubaliano ya muungano, (not a contract, but an agreement) yenye dhima ya muungano wa milele, na ndio maana tunasema “muungano tutaulinda kwa gharama yoyote”.

Tangu tumeungana, na mimi tangu nimezaliwa na kupata akili, sikumbuki hata mara moja, kusikia vipindi vya elimu ya uraia kuhuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, hali inayopelekea Baadhi ya Watanzania kuanza kujinasibisha na Utanganyika wao, na Uzanzibari wao.

Kwa vile Tanganyika ilifutwa na jina la Tanganyika kufutwa, utanganyika nao ukafutika, Watanganyika tunajisabisha kwa Utanzania wetu, lakini kwa vile kwa vile jina la Zanzibar, halikufutwa, na kuna Uzanzibari ukaazi, hivyo baadhi ya Wanzanzibari, wanajinasibisha kwa Uzanzibari wao kama uraia wa Zanzibar, badala ya kujinasibisha na Utanzania wao, kungekuwa na vipindi vya elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria, haki na wajibu, kusingekuwepo, vitimbakwiri wowote, wanaojinasibisha kwa Utanganyika wao, au Uzanzibari wao kwasababu, uraia wa JMT ni uraia mmoja tuu, hakuna uraia wa Tanganyika, wala hakuna urais wa Zanzibar, kuna uraia mmoja tuu, uraia wa JMT.

Wiki ijayo, nitaendelea na kuwaletea hizi chokochoko za kuuchokoa muungano na kuanza kunyoosheasha vidole vya ubaguzi wa “Utanganyika na Uzanzibari” zilianzia wapi, dawa yake ni nini na tiba ya kudumu ya kuitibu sumu hii na kuiangamiza kabisa.

View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=fPhb1_0doZmgD7T4
Wakati huo huo, naendelea na darasa langu la elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria na haki on Channel Ten kila Jumapili saa 3:00 usiku.
Karibuni.

Paskali

Kama 2 ni muungano wa federation na kilanchi inaendelea kua na utawala wa ndani sasa je raisi wa tanganyika yuko wapi?.
 
Wanabodi

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na kwa Maslahi ya Taifa, kila Jumatano kwenye gazeti la Mwananchi na Jumapili kwenye gazeti la Nipashe na kwenye kipindi cha KMT on Channel Ten TV, kila siku za Jumapili saa 3:00 usiku na marudio Jumatano saa 9:30 alasiri.

Hoja ya leo ni hoja za Utanganyika na Uzanzibari ambazo ni hoja muflis zinazosababishwa watu wanaitwa vitimbakwiri kujivunia uraia ambao haupo kutokana na ujinga tuu wa ukosefu wa elimu ya uraia kuhusu uraia wa Tanzania. Kwenye uraia, hakuna Mtanganyika wala Mzanzibari, tuna uraia mmoja tuu, Mtanzania. Swali ni jee tuwatoe ujinga hawa vitimbakwiri muflis wanaotaka kutubagua kwa Utanganyika na Uzanzibari kwa kuwaelimisha elimu ya uraia, au tuwaache tuu na ujinga wao kujisikia sifa kujinasibisha na kujivunia Utanganyika na Uzanzibari?.

Hili ni Nipashe la Leo.
View attachment 2994081

Ukosefu wa Elimu ya Uraia Kuhusu Katiba, Sheria, Haki na Wajibu, ndio umesababisha, huu ubaguzi wa Utanganyika, na Uzanzibari, watu wakielimishwa kuhusu uraia, hawa vitimbakwiri muflis wanaoleta ujinga wa ubaguzi wa kunyoosheana vidole vya Utanganyika na Uzanzibari, ujinga huu utawatoka, wataerevuka na tutakuwa na Utanzania pekee!.

Hivi karibuni, kumeibuka hoja za kibaguzi za baadhi ya wanasiasa, kutoa kauli za kibaguzi za kuwanyooshea watu vidole na kuwaita “Wao Wazanzibari”, “Sisi Watanganyika”. Miongozi mwa watu wanaotoa kauli hizo ni baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, waliofilisika kisiasa, na baadhi ya wanaolaani kauli hizo, ni baadhi ya viongozi wa chama tawala, ambapo nimemsikia mmoja wa viongozi hao, akilaani vikali kauli hizo bungeni kwa maneno makali kabisa!, huko pia ni kufilisika kisiasa.

NB. Aliyesema wanasiasa wanaojinasibisha na Utanganyika na Uzanzibari, dini zao, kanda zao, au kabila zao, ni watu muflis, waliofilisika kisiasa, sio mimi ni Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, na akaiandikia kitabu kinaitwa “Nyufa”. Mwalimu alisema dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana, ni kama kula nyama ya mtu, ukiishakula huwezi kuacha!.

Uraia ni hoja ya kikatiba na kisheria. Kabla ya Muungano, tulikuwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar, hivyo tulikuwa na uraia wa Tanganyika, na uraia wa Zanzibar. Baada ya muungano, tukaungana kuwa nchi moja ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwa na uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania.

Baada ya Muungano, majina ya nchi hizi zote mbili, nchi ya Tanganyika, na nchi ya Zanzibar, yalibadilika na kuwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, hivyo jina la Tanganyika likafutwa, ila jina la Zanzibar, liliendelea kuwepo, kutokana na uadimu na uadhimu wa huu muungano wetu.

Uadimu wa Muungano
Miungano ya nchi zote duniani ni miungano ya aina mbili kuu,

1. Muungano wa Union, ambapo nchi mbili zinaungana na kuunda nchi moja. Zile nchi zote mbili zilizoungana , zote zinakufa na kuunda nchi moja mpya. Hivyo ndivyo ulivyo muungano wetu kimataifa, ni muungano wa Unioni, ile nchi ya Tanganyika imekufa, ile nchi ya Zanzibar imekufa, imezaliwa nchi moja mpya ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye urais mmoja tuu, uraia wa Tanzania. Hakuna tena uraia wa Tanganyika, wala uraia wa Zanzibar, kuna uraia mmoja wa Tanzania. Tanganyika haipo nafasi yake imechukuliwa na Tanzania Bara, na Zanzibar japo ipo, ila sio nchi ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye utawala wake wa ndani, lakini hakuna uraia wa Zanzibar, uraia ni mmoja tuu wa Tanzania.

2. Muungano wa Federation, ni nchi mbili au zaidi, zinaungano kuwa nchi moja, lakini zile nchi zote mbili zinaendelea kuwa utawala wake wa ndani, na serikali zao, chini ya utawala mkuu wan chi ya federal state, kama Marekani. Vivyo hivyo muungano wetu kwa ndani ya muungano ni muungano wa federation yenye nchi mbili, Tanzania na Zanzibar, yenye marais wawili, Rais wa JMT “mwenye R kubwa, na rais wa Zanzibar mwenye r ndogo, zenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya SMZ, mabunge mawili, Bunge la JMT na BLW, na zenye mahakama mbili, Mahakama ya JMT na Mahakama ya Zanzibar, ila kwenye uraia, bado ni uraia mmoja tuu wa JMT, ila kwa Zanziar, wana ukaazi, ule ukaazi sio uraia ni utambulisho tuu wa wakaazi wa Zanzibar lakini wote ni Watanzania.

Hivyo muungano wa Tanzania ni muungano adimu pekee duniani ambao kwa upande mmoja ni muungano wa union na upande wa pili ni muungano wa federation, hakuna muungano wa aina hii popote duniani.

Uadhimu wa Muungano.
Muungano wetu licha ya kuwa ni muungano adimu, pia ni muungano adhimu, wenye dhima ya kuungana milele!. Miungano yote duniani unaundwa kwa mikataba ya kisheria ya muungano. Mikataba hiyo inakuwa na kipengele cha jinsi ya kuivunja miungano hiyo. Kwenye zile Articles of Union za Muungano wetu, hakuna kipengele cha jinsi ya kuuvunja, muungano, hivyo zile Hati za Muungano sio mkataba wa muungano, ni makubaliano ya muungano, (not a contract, but an agreement) yenye dhima ya muungano wa milele, na ndio maana tunasema “muungano tutaulinda kwa gharama yoyote”.

Tangu tumeungana, na mimi tangu nimezaliwa na kupata akili, sikumbuki hata mara moja, kusikia vipindi vya elimu ya uraia kuhuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, hali inayopelekea Baadhi ya Watanzania kuanza kujinasibisha na Utanganyika wao, na Uzanzibari wao.

Kwa vile Tanganyika ilifutwa na jina la Tanganyika kufutwa, utanganyika nao ukafutika, Watanganyika tunajisabisha kwa Utanzania wetu, lakini kwa vile kwa vile jina la Zanzibar, halikufutwa, na kuna Uzanzibari ukaazi, hivyo baadhi ya Wanzanzibari, wanajinasibisha kwa Uzanzibari wao kama uraia wa Zanzibar, badala ya kujinasibisha na Utanzania wao, kungekuwa na vipindi vya elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria, haki na wajibu, kusingekuwepo, vitimbakwiri wowote, wanaojinasibisha kwa Utanganyika wao, au Uzanzibari wao kwasababu, uraia wa JMT ni uraia mmoja tuu, hakuna uraia wa Tanganyika, wala hakuna urais wa Zanzibar, kuna uraia mmoja tuu, uraia wa JMT.

Wiki ijayo, nitaendelea na kuwaletea hizi chokochoko za kuuchokoa muungano na kuanza kunyoosheasha vidole vya ubaguzi wa “Utanganyika na Uzanzibari” zilianzia wapi, dawa yake ni nini na tiba ya kudumu ya kuitibu sumu hii na kuiangamiza kabisa.

View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=fPhb1_0doZmgD7T4
Wakati huo huo, naendelea na darasa langu la elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria na haki on Channel Ten kila Jumapili saa 3:00 usiku.
Karibuni.

Paskali

Hakuna hata mtu ana muda wa kusoma hilo gazeti lako. Ni hivi, hakuna uwezekano wa kutetea muungano huu kwa hoja. Hapa unapoteza muda wako bure. Tumechoka na muungano wenye kero zisizotatulika.
 
Back
Top Bottom