Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,465
- 23,768
Kipindi cha Kikwete walipinga sana suala la Ufisaidi. Hili walilisimamia kidete kwa kweli tunashukuru lilisikika maana ni kweli lilitamaraki.
Kipindi cha Magufuli chorus ilibadilika ikawa ni Makonda hivi Makonda vile. Wakalalamika tu Magufuli ni Dikteta n.k. Magufuli akafariki.
Wakajaribu kusikilizia upepo haukwenda sawa. Wakaja na suala la Katiba mpya. Likaenda enda wakaliacha. Hawajawa na consistency katika hili jambo la msingi sana. Wameiacha hoja hii ya msingi ya Katiba Mpya.
Sasa wanadakia na kusimamia kila tamko linalosemwa na wanasisiem. Na hasa hasa matamko ya Makonda. Inashangaza. Hawana tena data mbalimbali za msingi za kuelezea ufisadi ambao unafanyika. Hawana muda wa kuelezea madhambi mbalimbali na mapungufu wanayoyaona.
Watanzania wana maisha magumu hakuna wa kuwasemea. Kwa sasa kila mtu anaimba wimbo wake. Lema amekazana na kauli ya Makonda ndo imekuwa sera yake. Hana jipya.
Lini tutapata upinzani imara wa kweli? Mwacheni Zitto yeye anakula pension. Huyo msimguse yupo ICU. safari hii hana cha kukosoa.
Kipindi cha Magufuli chorus ilibadilika ikawa ni Makonda hivi Makonda vile. Wakalalamika tu Magufuli ni Dikteta n.k. Magufuli akafariki.
Wakajaribu kusikilizia upepo haukwenda sawa. Wakaja na suala la Katiba mpya. Likaenda enda wakaliacha. Hawajawa na consistency katika hili jambo la msingi sana. Wameiacha hoja hii ya msingi ya Katiba Mpya.
Sasa wanadakia na kusimamia kila tamko linalosemwa na wanasisiem. Na hasa hasa matamko ya Makonda. Inashangaza. Hawana tena data mbalimbali za msingi za kuelezea ufisadi ambao unafanyika. Hawana muda wa kuelezea madhambi mbalimbali na mapungufu wanayoyaona.
Watanzania wana maisha magumu hakuna wa kuwasemea. Kwa sasa kila mtu anaimba wimbo wake. Lema amekazana na kauli ya Makonda ndo imekuwa sera yake. Hana jipya.
Lini tutapata upinzani imara wa kweli? Mwacheni Zitto yeye anakula pension. Huyo msimguse yupo ICU. safari hii hana cha kukosoa.