Wanaodai Rais Magufuli hakuwa anapingwa ni waongo wakubwa

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,317
113,946
Nimeona ona humu JF baadhi ya watu wanadai kuwa eti kipindi cha Rais Magufuli watu ambao hivi sasa wanamkosoa Rais Samia, hawakuthubutu kumpinga hadharani kama ambavyo wanampinga huyu mama yao.

Hilo si kweli. Rais Magufuli alipingwa sana na watu. Tena watu wa kada zote.

Kudai kuwa hawa wanaomkosoa Samia hivi sasa enzi za Magufuli walikuwa kimya, huko ni kulazimisha uongo na ni kujisahaulisha kiumakusudi tu.

Magufuli alipingwa na CCM wenzake na alipingwa hata na wabeba maboksi maskini kama mimi na ushahidi upo [risiti zipo].

Kwa mfuatiliaji yeyote yule aliye makini na ambaye hasukumwi wala kuendeshwa na hisia, ukweli huo ni dhahiri kabisa.

Sasa hawa wajulikanao kama ‘chawa wa mama’ [weirdos] ni watu ambao hawatumii akili katika majadiliano yoyote yale yamhusuyo huyo mama yao.

Wao ni hisia tu kwa kwenda mbele. Huwezi kufanya nao majadiliano yoyote yale yaliyo ya maana.

Kwao kila kitu ni ‘whataboutism’ [sijui Kiswahili chake] tu.

Hawana kabisa hoja. Na hawawezi kabisa kujenga hoja.

Ukihoji chochote kuhusu Samia, wao jibu lao ni ‘what about Magufuli’.

No one is above criticism and no one is below praise.

And anybody can get it. That includes Samia as well.

Just suck it up, buttercups.
 
Mfano mtu anakomaa anasema heti bomba la mafuta pia walisaini IGa ,nikamuuliza bomba la mafuta sisi tumewekeza nini, kwanza bomba la mafuta mbona hakuna mfanano na bandari, ndio maana Uganda alikua anaweza kuamua kupitisha popote Kenya au Tanzania
 
Nimeona ona humu JF baadhi ya watu wanadai kuwa eti kipindi cha Rais Magufuli watu ambao hivi sasa wanamkosoa Rais Samia, hawakuthubutu kumpinga hadharani kama ambavyo wanampinga huyu mama yao.

Hilo si kweli. Rais Magufuli alipingwa sana na watu. Tena watu wa kada zote.

Kudai kuwa hawa wanaomkosoa Samia hivi sasa enzi za Magufuli walikuwa kimya, huko ni kulazimisha uongo na ni kujisahaulisha kiumakusudi tu.

Magufuli alipingwa na CCM wenzake na alipingwa hata na wabeba maboksi maskini kama mimi na ushahidi upo [risiti zipo].

Kwa mfuatiliaji yeyote yule aliye makini na ambaye hasukumwi wala kuendeshwa na hisia, ukweli huo ni dhahiri kabisa.

Sasa hawa wajulikanao kama ‘chawa wa mama’ [weirdos] ni watu ambao hawatumii akili katika majadiliano yoyote yale yamhusuyo huyo mama yao.

Wao ni hisia tu kwa kwenda mbele. Huwezi kufanya nao majadiliano yoyote yale yaliyo ya maana.

Kwao kila kitu ni ‘whataboutism’ [sijui Kiswahili chake] tu.

Hawana kabisa hoja. Na hawawezi kabisa kujenga hoja.

Ukihoji chochote kuhusu Samia, wao jibu lao ni ‘what about Magufuli’.

No one is above criticism and no one is below praise.

And anybody can get it. That includes Samia as well.

Just suck it up, buttercups.
Tatizo ni katiba yetu

Anayesema Magufuli hakupingwa ni mwongo,Mimi ni mwana ccm niliyekuwa na neutralize hoja nyingi sana za kumuhusu JPM

JPM tulimtetea kwenye tangible asset yanayohusiana na construction tu,

Kwenye suala la CAG Assad mimi pia nilimpinga live JPM

Masuala ya kukanyaga katiba tulimpinga live JPM

Mwenyekiti wa chama cha siasa ndie Rais wa nchi halafu yupo juu ya katiba

Wanaotakiwa kumsimamia Bunge na Mahakama ndio hao wanaomba pesa kwake za matumizi na wengine anawateua kwenye nafasi za uwaziri mkuu na wengine majaji

Tatizo wanaompinga Samia hawana hoja za msingi bali ni kelele za uzanzibar,utanganyika na udini tu

Na wale wanaomtetea pia sijaona hoja zao za msingi

Issue Tanzania hatuna mifumo/Institutional imara inayoweza kujisimamia,Mifumo yetu ni teua na tengua na nguvu hii ya teua na tengua anayo mtu mmoja
 
Hawa chawa wa mama [weirdos] wanaumia sana mama yao anapopingwa!

Kama hawataki apingwe, waende wakamwambie aache urais arudi zake kwao huko Unguja.
Bandiko lako namba moja lina ukweli kwa asilimia kubwa mno, lakini kuna sehemu hauko sawa. Ni hivi, hakuna mwanaccm yoyote alithubutu kumpinga Magufuli. Watu pekee walioweza kumpinga Magufuli ndani na nje ya bunge ni wapinzani, na viongozi wachache sana wa kidini tena wanahesabika. Hawa akina Slaa, Tibaijuka, Shivji nk walikuwa wameufyata, sio kwasababu waliona Magufuli yuko sahihi, ila walitaka waendelee kubaki hai kumsubiri rais mwingine wa kumkosoa, lakini sio Magufuli.

Wakati wa Magufuli hakukuwa na chombo chochote rasmi cha habari kilichothubutu kuandaa press, au mdahalo wa kujadili asichopenda Magufuli. Na baadhi ya online media au baadhi ya media chache zilizothubutu kuruhusu ukosoaji kwa Magufuli, zilifungiwa au kupewa adhabu kali, ikiwemo na kudhalilishwa na ushahidi upo wazi. Hao wanaosema kuwa kipindi cha Magufuli hakukosolewa kwa kiwango kikubwa wako sahihi, japo sio kuwa hakukosolewa kwa kuwa alikuwa sahihi, bali lile kundi lake la watu wasiojulikana lilifanya kazi yake vizuri ya kunyamazisha wakosoaji. Hata Magufuli kuanza kununua wapinzani kwenye ile siasa yake chafu ya kuunga mkono juhudi, ilikuwa ni kupunguza kukosolewa, na funga kazi ilikuwa ni kunajisi uchaguzi wa 2020 ili kuua rasmi ukosoaji kwenye bunge. Mitandao ya kijamii ndio pekee iliyofanikiwa kubaki kumkosoa Magufuli kwa kutumia fake ID bila kuumizwa. Lakini yoyote hasa wapinzani waliomkosoa waliuliwa, kutekwa, kuharibiwa sehemu zao za kuwaingizia vipato, kubambikiwa kesi na ukatili mwingine wa wazi kabisa.
 
Bandiko lako namba moja lina ukweli kwa asilimia kubwa mno, lakini kuna sehemu hauko sawa. Ni hivi, hakuna mwanaccm yoyote alithubutu kumpinga Magufuli. Watu pekee walioweza kumpinga Magufuli ndani na nje ya bunge ni wapinzani, na viongozi wachache sana wa kidini tena wanahesabika. Hawa akina Slaa, Tibaijuka, Shivji nk walikuwa wameufyata, sio kwasababu waliona Magufuli yuko sahihi, ila walitaka waendelee kubaki hai kumsubiri rais mwingine wa kumkosoa, lakini sio Magufuli.

Wakati wa Magufuli hakukuwa na chombo chochote rasmi cha habari kilichothubutu kuandaa press, au mdahalo wa kujadili asichopenda Magufuli. Na baadhi ya online media au baadhi ya media chache zilizothubutu kuruhusu ukosoaji kwa Magufuli, zilifungiwa au kupewa adhabu kali, ikiwemo na kudhalilishwa na ushahidi upo wazi. Hao wanaosema kuwa kipindi cha Magufuli hakukosolewa kwa kiwango kikubwa wako sahihi, japo sio kuwa hakukosolewa kwa kuwa alikuwa sahihi, bali lile kundi lake la watu wasiojulikana lilifanya kazi yake vizuri ya kunyamazisha wakosoaji. Hata Magufuli kuanza kununua wapinzani kwenye ile siasa yake chafu ya kuunga mkono juhudi, ilikuwa ni kupunguza kukosolewa, na funga kazi ilikuwa ni kunajisi uchaguzi wa 2020 ili kuua rasmi ukosoaji kwenye bunge. Mitandao ya kijamii ndio pekee iliyofanikiwa kubaki kumkosoa Magufuli kwa kutumia fake ID bila kuumizwa. Lakini yoyote hasa wapinzani waliomkosoa waliuliwa, kutekwa, kuharibiwa sehemu zao za kuwaingizia vipato, kubambikiwa kesi na ukatili mwingine wa wazi kabisa.
Umesema ukweli mtupu.
 
Nimeona ona humu JF baadhi ya watu wanadai kuwa eti kipindi cha Rais Magufuli watu ambao hivi sasa wanamkosoa Rais Samia, hawakuthubutu kumpinga hadharani kama ambavyo wanampinga huyu mama yao.

Hilo si kweli. Rais Magufuli alipingwa sana na watu. Tena watu wa kada zote.

Kudai kuwa hawa wanaomkosoa Samia hivi sasa enzi za Magufuli walikuwa kimya, huko ni kulazimisha uongo na ni kujisahaulisha kiumakusudi tu.

Magufuli alipingwa na CCM wenzake na alipingwa hata na wabeba maboksi maskini kama mimi na ushahidi upo [risiti zipo].

Kwa mfuatiliaji yeyote yule aliye makini na ambaye hasukumwi wala kuendeshwa na hisia, ukweli huo ni dhahiri kabisa.

Sasa hawa wajulikanao kama ‘chawa wa mama’ [weirdos] ni watu ambao hawatumii akili katika majadiliano yoyote yale yamhusuyo huyo mama yao.

Wao ni hisia tu kwa kwenda mbele. Huwezi kufanya nao majadiliano yoyote yale yaliyo ya maana.

Kwao kila kitu ni ‘whataboutism’ [sijui Kiswahili chake] tu.

Hawana kabisa hoja. Na hawawezi kabisa kujenga hoja.

Ukihoji chochote kuhusu Samia, wao jibu lao ni ‘what about Magufuli’.

No one is above criticism and no one is below praise.

And anybody can get it. That includes Samia as well.

Just suck it up, buttercups.
Nakubaliana naww kbs kuhusu hao chawa wa mama!! But kuhusu JPM kukubali kukosolewa hilo c kwel ndugu nyani, kwanza CCM hawakuthubu kumkosoa na wapinzani yeyote aliethubutu kumkusoa lazima akubali consequences. Viongoz wa dini waliothubutu kumkosoa walilazimika kuchunguzwa uraia wao!!! Tuwe wakwel tu hakupenda kukosolewa au kusikia asiyopenda!!!
 
Mfano mtu anakomaa anasema heti bomba la mafuta pia walisaini IGa ,nikamuuliza bomba la mafuta sisi tumewekeza nini ,kwanza bomba la mafuta mbona hakuna mfanano na bandari, ndio maana Uganda alikua anaweza kuamua kupitisha popote Kenya au Tanzania
😂😂 Mahali nimejua watetezi wa Samia wamepoteana ni hapo walipoanza kusema eti wanataka kujua kuhusu MoU ya hospitali za KCMC na Bugando! Yaani wanalazimisha iwe ni ukosoaji kwa sababu za kidini, wakiamini watatupoteza maboya tukae kimya. Halafu wanaokuja na hiyo kete dhaifu, huwa wanajinasibu ni wasomi hapa jukwaani.
 
Hata kama JPM alikuwa hapingwi... (Ingawa alipingwa vya kutosha) labda tuseme alijaribu ku-neutralize Media (Jambo ambalo huyu mama kasema sijui wakifanya nini atawaparura - kwahio huenda penye udhia anapenyeza Rupia)...

Anyway Hata Kama JPM alikuwa hapingwi ukiona mtu badala ya kujibu hoja ya upingaji analeta story kwamba fulani mbona hakupingwa ujue either ana umasikini wa hoja au anadhani two wrongs makes a right....; Kuna tatizo gani kama walipa Kodi kuamua kuanza kutumia Haki yake ya Kupinga Leo !!!!????
 
Tatizo ni katiba yetu

Anayesema Magufuli hakupingwa ni mwongo,Mimi ni mwana ccm niliyekuwa na neutralize hoja nyingi sana za kumuhusu JPM

JPM tulimtetea kwenye tangible asset yanayohusiana na construction tu,

Kwenye suala la CAG Assad mimi pia nilimpinga live JPM

Masuala ya kukanyaga katiba tulimpinga live JPM

Mwenyekiti wa chama cha siasa ndie Rais wa nchi halafu yupo juu ya katiba

Wanaotakiwa kumsimamia Bunge na Mahakama ndio hao wanaomba pesa kwake za matumizi na wengine anawateua kwenye nafasi za uwaziri mkuu na wengine majaji

Tatizo wanaompinga Samia hawana hoja za msingi bali ni kelele za uzanzibar,utanganyika na udini tu

Na wale wanaomtetea pia sijaona hoja zao za msingi

Issue Tanzania hatuna mifumo/Institutional imara inayoweza kujisimamia,Mifumo yetu ni teua na tengua na nguvu hii ya teua na tengua anayo mtu mmoja
Hoja ni makubaliano ya uwekezaji wa kinyonyaji bandari

Wananchi hatutaki
 
Nakubaliana naww kbs kuhusu hao chawa wa mama!! But kuhusu JPM kukubali kukosolewa hilo c kwel ndugu nyani, kwanza CCM hawakuthubu kumkosoa na wapinzani yeyote aliethubutu kumkusoa lazima akubali consequences. Viongoz wa dini waliothubutu kumkosoa walilazimika kuchunguzwa uraia wao!!! Tuwe wakwel tu hakupenda kukosolewa au kusikia asiyopenda!!!

Uko sahihi kabisa, hawa wanaosema kuwa Magufuli hakukosolewa kwa sehemu kubwa wako sahihi. Tatizo ninaloliona kwao ni kumtumia mtu muovu kama sehemu ya kipimo cha mtu wao. Yaani kama wanajitambua ni bora watafute njia nyingine ya kumtetea mtu wao, na sio hicho kipimo cha yule mtu muovu.
 
Nimeona ona humu JF baadhi ya watu wanadai kuwa eti kipindi cha Rais Magufuli watu ambao hivi sasa wanamkosoa Rais Samia, hawakuthubutu kumpinga hadharani kama ambavyo wanampinga huyu mama yao.

Hilo si kweli. Rais Magufuli alipingwa sana na watu. Tena watu wa kada zote.

Kudai kuwa hawa wanaomkosoa Samia hivi sasa enzi za Magufuli walikuwa kimya, huko ni kulazimisha uongo na ni kujisahaulisha kiumakusudi tu.

Magufuli alipingwa na CCM wenzake na alipingwa hata na wabeba maboksi maskini kama mimi na ushahidi upo [risiti zipo].

Kwa mfuatiliaji yeyote yule aliye makini na ambaye hasukumwi wala kuendeshwa na hisia, ukweli huo ni dhahiri kabisa.

Sasa hawa wajulikanao kama ‘chawa wa mama’ [weirdos] ni watu ambao hawatumii akili katika majadiliano yoyote yale yamhusuyo huyo mama yao.

Wao ni hisia tu kwa kwenda mbele. Huwezi kufanya nao majadiliano yoyote yale yaliyo ya maana.

Kwao kila kitu ni ‘whataboutism’ [sijui Kiswahili chake] tu.

Hawana kabisa hoja. Na hawawezi kabisa kujenga hoja.

Ukihoji chochote kuhusu Samia, wao jibu lao ni ‘what about Magufuli’.

No one is above criticism and no one is below praise.

And anybody can get it. That includes Samia as well.

Just suck it up, buttercups.
Kwa hili Nakuunga mkono. Akina Bagonza, Niwemugiz8, Lissu Mwamakula, Mbowe na Mnyika na wengineo wengi tuu walimpa za uso.

Wanatafuta kichaka cha kujifichia tu hao.
 
Tatizo ni katiba yetu

Anayesema Magufuli hakupingwa ni mwongo,Mimi ni mwana ccm niliyekuwa na neutralize hoja nyingi sana za kumuhusu JPM

JPM tulimtetea kwenye tangible asset yanayohusiana na construction tu,

Kwenye suala la CAG Assad mimi pia nilimpinga live JPM

Masuala ya kukanyaga katiba tulimpinga live JPM

Mwenyekiti wa chama cha siasa ndie Rais wa nchi halafu yupo juu ya katiba

Wanaotakiwa kumsimamia Bunge na Mahakama ndio hao wanaomba pesa kwake za matumizi na wengine anawateua kwenye nafasi za uwaziri mkuu na wengine majaji

Tatizo wanaompinga Samia hawana hoja za msingi bali ni kelele za uzanzibar,utanganyika na udini tu

Na wale wanaomtetea pia sijaona hoja zao za msingi

Issue Tanzania hatuna mifumo/Institutional imara inayoweza kujisimamia,Mifumo yetu ni teua na tengua na nguvu hii ya teua na tengua anayo mtu mmoja

Kweli wewe ulimkosoa Magufuli kwenye baadhi ya mambo, lakini hao watetezi hawaongelei sisi wenye fake I'd huku mitandaoni, maana huku mitandaoni ndio sehemu pekee Magufuli aliweza kuambiwa ukweli uliomuumiza. Hivyo huwezi kusema ulimpinga huku mitandaoni kwa fake I'd ambayo hakuna anayejua ww ni nani.

Tunataka watu waliompinga Magufuli kwa kufahamika wazi wao ni akina nani, kama wanavyofanya kina Shivji, Slaa, Tibaijuka nk kwa sasa, ambao huko nyuma hawakuthubutu. Hapa ndipo kilipo kichaka cha watetezi wa Samia kwa sasa kwenye hili sakata la bandari.
 
Kwa hili Nakuunga mkono. Akina Bagonza, Niwemugiz8, Lissu Mwamakula, Mbowe na Mnyika na wengineo wengi tuu walimpa za uso.

Wanatafuta kichaka cha kujifichia tu hao.
Hawa uliowataja ndio hao watu wachache sana waliothubutu kumkosoa Magufuli kwa gharama kubwa. Ila hawa watetezi wa Samia sasa,wanashangaa hata mabubu wa wakati wa Magufuli wanapata wapi uhalali, wakati walikalia kimya uovu wa wazi wa Magufuli?
 
Back
Top Bottom