UWAMATA na wamiliki wa mabasi dhibitini wauza madawa na vitu kwenye mabasi ya mikoani

crome20

JF-Expert Member
Feb 5, 2010
1,130
721
Kwa wale wastaarabu tu ndio wanaoelewa. Ni kero kwa abiria wachuuzi kuingia ndani ya mabasï kuuza vitu vyao. Mwenye shida anunué hapo nje na sio kupishana na matenga, maboksi na kupigiwa kelele. Nilishangaa nikiwa kwenye basi la NEW FORCE kuelekea Lindi hadi mabeseni ya samaki yanapita.

Kuna na ile tabia ya kitapeli ya kufanya promotiòn ndani ya mabasi wakiuza vipodozi, mafuta, dawa za meno n.k. Huu mtindo unaofadhiliwa na madereva ni kero kubwa sana. Usafiri wa mikoani unatakiwe uwe wa viwango vya kistaarabu sana maana tunakutana watu wenye picha tofauti kabisa.
 
Umesahau na wanao hubiri kupitia dini zote. Japo ni jambo zuri.
 
Nkajua wauza ngada
Mkuu kemea hilo pepo, kila mtu ana njia yake ya kutafutia ridhiki

Aya wakizuiliwa utawapa ww ajira?
 
waacheni jamani watafute hela sidhani kama anakaa mda mrefu mpaka kusema inakuwa kero,samaki hapo ndo kuna shida kidogo
 
Kwa wale wastaarabu tu ndio wanaoelewa. Ni kero kwa abiria wachuuzi kuingia ndani ya mabasï kuuza vitu vyao. Mwenye shida anunué hapo nje na sio kupishana na matenga, maboksi na kupigiwa kelele. Nilishangaa nikiwa kwenye basi la NEW FORCE kuelekea Lindi hadi mabeseni ya samaki yanapita.

Kuna na ile tabia ya kitapeli ya kufanya promotiòn ndani ya mabasi wakiuza vipodozi, mafuta, dawa za meno n.k. Huu mtindo unaofadhiliwa na madereva ni kero kubwa sana. Usafiri wa mikoani unatakiwe uwe wa viwango vya kistaarabu sana maana tunakutana watu wenye picha tofauti kabisa.
Okay
 
Back
Top Bottom