Tulibomoa nyumba za wananchi Kimara -Mbezi ili matajiri wajenge vituo vya mafuta? Je, hivi vituo vingi kiasi hiki vinapataje kibali?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
939
4,426
Natoka Mwanza, kutoka Kibaha hadi Kimara nimeona tayari vituo zaidi ya Nane vya Mafuta vimejengwa kwenye hifadhi ya barabara.

Ninaamini hivi vituo havikuwepo kwenye ramani ya barabara kwa wingi huu. Lakini pia naamini haya maeneo hayakutengwa kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya mafuta lakini kwa sababu ya rushwa kila mtu amemega eneo lake anajenga anavyojisikia.

Kwa namna hii miaka siyo mingi foleni itakuwa kubwa sana kwa sababu magari yatakuwa yanaingia kwenye vituo vya mafuta na kutoka hivyo kupelekea speed tarajiwa kupungua barabarani.

Lakini pia vituo hivi vinaonekana vimeanza kutumika kupaki malori makubwa huku baadhi ya malori kutoka bandarini yakija kujaza mafuta nakupanga foleni barabarani katikati.

Mimi ninayekuja mara moja moja huku tayari nimeona huu uhalifu ,je wananchi wa DAR mnafurahia haya?

Lakini pia tunazungumzia kupanga miji, hakuna mji wowote uliopangwa Duniani wenye utitiri wa petrol station Duniani. Sisi tunashindwa nini kuiga wenzetu walivyofanikiwa?

Mwisho, hivi vituo kwa majina tu inaleta picha kwamba wapo watumishi wa umma wanapiga fedha serikalini na kuja kuzielekeza kwenye biashara ya mafuta. Hakuna wafanyabiashara wenye business plan watatega vituo vya mafuta kama inavyofanyika sasa.

Labda TANROADS watueleze kama haya wanayofanya ndiyo yaliyopelekea kuwavunjia watu nyumba na biashara zao bila fidia wakati wa JPM? Kwanini tunatumia madaraka yetu kuharibu kesho ya watoto na wajukuu wetu? Nini tathimini ya kimazingira kwenye mji wenye watu wengi kama huu kujaza vituo vya mafuta?

Kwanini kama tulitaka kuwekeza tusingeweka vituo vya gesi?
 
Natoka Mwanza, kutoka Kibaha hadi Kimara nimeona tayari vituo zaidi ya Nane vya Mafuta vimejengwa kwenye hifadhi ya barabara.

Ninaamini hivi vituo havikuwepo kwenye ramani ya barabara kwa wingi huu. Lakini pia naamini haya maeneo hayakutengwa kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya mafuta lakini kwa sababu ya rushwa kila mtu amemega eneo lake anajenga anavyojisikia.

Kwa namna hii miaka siyo mingi foleni itakuwa kubwa sana kwa sababu magari yatakuwa yanaingia kwenye vituo vya mafuta na kutoka hivyo kupelekea speed tarajiwa kupungua barabarani.

Lakini pia vituo hivi vinaonekana vimeanza kutumika kupaki malori makubwa huku baadhi ya malori kutoka bandarini yakija kujaza mafuta nakupanga foleni barabarani katikati.

Mimi ninayekuja mara moja moja huku tayari nimeona huu uhalifu ,je wananchi wa DAR mnafurahia haya?

Lakini pia tunazungumzia kupanga miji, hakuna mji wowote uliopangwa Duniani wenye utitiri wa petrol station Duniani. Sisi tunashindwa nini kuiga wenzetu walivyofanikiwa?

Mwisho, hivi vituo kwa majina tu inaleta picha kwamba wapo watumishi wa umma wanapiga fedha serikalini na kuja kuzielekeza kwenye biashara ya mafuta. Hakuna wafanyabiashara wenye business plan watatega vituo vya mafuta kama inavyofanyika sasa.

Labda TANROADS watueleze kama haya wanayofanya ndiyo yaliyopelekea kuwavunjia watu nyumba na biashara zao bila fidia wakati wa JPM? Kwanini tunatumia madaraka yetu kuharibu kesho ya watoto na wajukuu wetu? Nini tathimini ya kimazingira kwenye mji wenye watu wengi kama huu kujaza vituo vya mafuta?

Kwanini kama tulitaka kuwekeza tusingeweka vituo vya gesi?
Mkuu umefanya vizuri kukiri kuwa wewe sio mmenyeji wa jiji la Dar es salaam hasa maeneo ya Morogoro road.

Pamoja na hayo ungeweza kupita Tanroad ukawauliza ili kuondoa mashaka yako, kuliko kutoa tuhuma za jumla kwa kuhisi tu.

Hifadhi ya barabara za taifa zote nchi zipo chini ya milki/mamlaka ya Tanroads, wao ndio wenye uamuzi wa ama kutumia wao au kwa kukodisha watu mbali mbali hususan parking space, petrol stations na biashara nyingine yoyote.

Masharti yao kwa sasa usiweke jengo la kudumu basi! Huduma ya kupaki magari na mafuta ni muhimu kwa matumizi ya wenye vyombo vya moto mjini!

Kuhusu vibali, hii ni biashara huria Mkuu na huduma muhimu kwa jamii. Serikali inapata kodi, ajira nyingi kupatikana kwa vijana na kuongeza mnyororo manufaa ya kiuchumi kwenye eneo husika.

Mkuu acha mambo na ukuda wa Tibaijuka huko Muleba!

Mkuu sio kila jambo linaambatana na rushwa au ufisadi, tuwe tunapata taarifa sahihi kabla ya kutuhumu tu.

Kumbuka siku zote sheli hujengwa pembeni mwa barabara!

Karibu Dar.
 
Mtoa hoja ninaunga mkono hoja yako,pale kinondoni studio kuna petrol station right kwenye residential area!,royal families zitanyanyasa sana Tanzania,wao wapo kwenye safe areas
 
Mtoa hoja ninaunga mkono hoja yako,pale kinondoni studio kuna petrol station right kwenye residential area!,royal families zitanyanyasa sana Tanzania,wao wapo kwenye safe areas
Mkuu unalalamikia hiyo petrol station ya Kinondoni studio imekuathiri wewe binafsi kivipi??? Ondoa wenge la chuki!

Royal family ipi hapaTanzania na imekunyanyasa wewe na nani?? Na kivipi?? Kwa nini hujaenda mahakamani??

Mkuu unataka petrol station zijengwe wapi?? Mbugani au baharini?? Umepanga mji ukaacha wazi maeneo ya huduma hiyo??

Mkuu unapotuhumu wawekezaji wa petrol stations umeconsider maslahi ya wa tumia vyombo vya moto?? Waajiriwa wa vituo hivyo na biashara nyemelezi??

Mkuu unamaanisha mamlaka zinazotoa vibali kuruhusu petrol station zote ni wajinga??

Tuache chuki za kijinga!!
 
Mkuu unalalamikia hiyo petrol station ya Kinondoni studio imekuathiri wewe binafsi kivipi??? Ondoa wenge la chuki!

Royal family ipi hapaTanzania na imekunyanyasa wewe na nani?? Na kivipi?? Kwa nini hujaenda mahakamani??

Mkuu unataka petrol station zijengwe wapi?? Mbugani au baharini?? Umepanga mji ukaacha wazi maeneo ya huduma hiyo??

Mkuu unapotuhumu wawekezaji wa petrol stations umeconsider maslahi ya wa tumia vyombo vya moto?? Waajiriwa wa vituo hivyo na biashara nyemelezi??

Mkuu unamaanisha mamlaka zinazotoa vibali kuruhusu petrol station zote ni wajinga??

Tuache chuki za kijinga!!
Hapa ni wazi umeonesha wewe ndiye mjinga.
 
Mkuu umefanya vizuri kukiri kuwa wewe sio mmenyeji wa jiji la Dar es salaam hasa maeneo ya Morogoro road.

Pamoja na hayo ungeweza kupita Tanroad ukawauliza ili kuondoa mashaka yako, kuliko kutoa tuhuma za jumla kwa kuhisi tu.

Hifadhi ya barabara za taifa zote nchi zipo chini ya milki/mamlaka ya Tanroads, wao ndio wenye uamuzi wa ama kutumia wao au kwa kukodisha watu mbali mbali hususan parking space, petrol stations na biashara nyingine yoyote.

Masharti yao kwa sasa usiweke jengo la kudumu basi! Huduma ya kupaki magari na mafuta ni muhimu kwa matumizi ya wenye vyombo vya moto mjini!

Kuhusu vibali, hii ni biashara huria Mkuu na huduma muhimu kwa jamii. Serikali inapata kodi, ajira nyingi kupatikana kwa vijana na kuongeza mnyororo manufaa ya kiuchumi kwenye eneo husika.

Mkuu acha mambo na ukuda wa Tibaijuka huko Muleba!

Mkuu sio kila jambo linaambatana na rushwa au ufisadi, tuwe tunapata taarifa sahihi kabla ya kutuhumu tu.

Kumbuka siku zote sheli hujengwa pembeni mwa barabara!

Karibu Dar.
Tunapojadili hapa siyo mali za wafanyakazi wa Tanroads ni mali za umma; sisi ndiyo wamiliki wa roard reserves siyo Tanroad

Hoja ya kupanua barabara ilikuwa kupunguza foleni, unapojenga vituo vya mafuta unaongeza foleni; siyo hadi ukasome chuo kikuu.

Umesema Duniani, tuonyeshe huko Duniani nchi zilizoendelea ni wapi wamejenga vituo vya mafuta kila sehemu?

Jambo jingine, wakati tunachora barabara kulikuwa na vituo vya mafuta? Vingapi? Maeneo gani?

Kama ni biashara huria kwanini tuliwavuniia wananchi? Si tungewaambia walipe kodi tu?
 
Back
Top Bottom