UZUSHI TANESCO wameshindwa kesi Marekani na wametakiwa kutoa bilioni 320 kwa IPTL

Baada ya tathmini, tumebaini kuwa taarifa hii ni ya uzushi
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
Salaam,

Ndugu zangu kuna habari nimeona inasambaa kwa kasi Twitter ikidai kwamba Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) limeshindwa kwenye kesi yake na IPTL -Independent Power Tanzania Limited.

Taarifa hiyo inadai TANESCO yashindwa kesi Marekani na kutakiwa kuilipa IPTL billioni 320!

Je kuna ukweli hapa?

Tazama mwenyewe:

1692211456588.png
 
Tunachokijua
JamiiForums imepitia vyanzo mbalimbali na kubaini kuwa Taarifa hii imeibuliwa na ukurasa wa X (Zamani Twitter) ya Tanzania Abroad TV na kisha kuletwa na kuanza kusambaa kwenye mitandao mingine ya kijamii.

Je, ni kweli TANESCO wameshindwa kesi na wametozwa bilioni

JamiiForums imepitia vyanzo mbalimbali na kubaini kuwa taarifa hii ni ya kweli lakini ilikuwa ni ya Septemba 19, 2016 ambapo ilitokana imetokana na uzi ulioletwa na Mwanachama wa JamiiForums aliyeitwa Jerrytz. Tazama picha hapa chini:

1692214044004-png.2719318

Sehemu ya andiko lililoletwa na Jerrytz Septemba 19, 2016​

Aidha, JamiiForums imebaini kuwa ukurasa wa X (Zamani Twitter) ya Tanzania Abroad TV umeichukua mada hiyo ya Septemba 19, 2016 na kuifanya kama imetokea Agosti 16, 2023.

Zaidi ya hayo, taarifa hizi hazipatikani katika kurasa zote rasmi za TANESCO.

Hivyo, kutokana na vyanzo hivi, hoja inayodai TANESCO imeshindwa kesi siku za karibuni haina ukweli.
Hiyo kesi lazima kuna watanzania wenzetu watakuwa wametuuza.

kwa sababu haiwezekani kila kesi za kimataifa lazima Tanzania tushindwe. Na mwisho wa siku lazima tuishie kulipa mabilioni.

Na wakati huo hii nchi yetu yenyewe ni maskini.
 
Safi... Hongera Jamiiforums maana hapo nyuma kidogo tulitatizika sana hii source 1 na source 2 kwenye post zetu ina maaisha nini na kwa bahati mbaya sikupata ufumbuzi ila leo nimeelewa maana yake sasa
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom