UZUSHI Pen (kalamu) zinazolipuka kama Bunduki zinagawiwa na kuuzwa kwenye Shule za Tanzania

Baada ya tathmini, tumebaini kuwa taarifa hii ni ya uzushi
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
Leo nimeona video ambao imewekewa sauti ya mtu akisema wametumiwa video hiyo kwenye group la shule ya Themihill, video hiyo inaonesha mtu akifungua kitu kinachoonekana kama pen (kalamu) ambacho ndani yake kina risasi na baadaye kufyatuliwa.

1000032648.jpg


Anayeelezea video hiyo anadai pen hizo zinagawiwa mashuleni na kuuzwa huku akionesha hofu ya watoto kuuana au wao wenyewe kujidhuru kwa peni hizo.

Ningependa kufahamu ukweli kuhusu video hiyo.


 
Tunachokijua
Bunduki ya kalamu ni bunduki inayofanana na kalamu ya wino. Kwa ujumla ni za kiwango kidogo (k.m., .22 LR, .25 ACP, .32 ACP, .38-caliber, n.k.) Na huwa na uwezo wa kubeba risasi moja pekee.

images
Siku za hivi karibuni imesambaa video ikionesha mikono na kusikika sauti ya ya mtu mmoja anayeongea lugha ya kigeni huku akionesha Kitu kama kalamu ambacho aliweka risasi na kisha kukifyatua na kikalipuka mithiri ya bunduki. Hali hiyo ya kulipuka inafanya tuamini bila shaka hiyo ni bunduki ndogo iliyotengenezwa katika umbo la kalamu.

Katika video hiyo ambayo ilianza kusambaa wiki mbili zilizopita Kuanzia tarehe 8 April 2024 ambapo kulingana na video iliyopo mtandao wa Youtube inaonesha video hiyo ilianza kusambaa kutokea South Africa katika mtandao wa Youtube kisha kuenea mitandao mingine japo video hiyo imekuwepo mtandaoni muda mrefu.

Baadaye tena ilisambaa video hiyohiyo kwene mitandao ya kijamii Nchini Tanzania ikiwa imewekwa sauti ya mwanamke anayeongea lugha ya kiswahili ambaye alidai wametumiwa video hiyo kwenye kundi sogozi (group) la Shule ya ThemiHill ambapo wameambiwa kalamu hizo zinagawiwa mashuleni na kuuzwa, huku akiongea kuonesha wasiwasi juu ya watoto kuuana au kujeruhiana kwa kutumia kalamu hizo.

Je, ukweli ni upi juu ya uwepo wa kalamu hizo nchini?

Jamiicheck
ilichukua hatua ya kuifatilia taarifa hiyo ili kubaini ukweli wake, ambapo tulimtafuta Mkurugenzi na mwanzilishi wa Shule ya Themihill, Michael Stien Mambo ambaye alieleza kuwa:

Clip hiyo ameiona na kuisikiliza, Mkuu wa shule amesema clip ya kwanza aliwahi kuiona muda mrefu siyo leo wala mwaka jana, ambayo inaongea lugha ngeni.

"Clip kwenye mitandao zipo 3, clip ya kwanza inaongea lugha ngeni na inatembea yenyewe na ipo mtandaoni sio leo wala mwaka jana
".
Alisema Mkurugenzi wa shule ya Themi hill

Aliendelea kusema kuwa clip hiyo hiyo kuna mama mmoja anayeongea kiswahili ambaye hamfahamu wala hafamu lengo lake, ameiwekea sauti video hiyo huku akiituhumu Themihill kugawa kalamu za bunduki kwa wanafunzi.

"Clip hiyo hiyo kuna Mama mmoja ameiwekea voice clip akitutuhumu Themihill kwamba sisi tunagawa kalamu bunduki kwa wanafunzi. Sasa mimi ninachojua bunduki zote pamoja na risasi kwa Tanzania ni mali ya Serikali, ukitaka kumiliki lazima bastola au risasi lazima uwe na kibali maalum cha kumiliki".


Mkurugenzi wa Shule ya Themihill, Michael Stien Mambo amesema kuwa suala hilo si la kweli na kwamba mama huyo amezusha kwa lengo la aidha kuichafua taasisi yao au kumchafua yeye binafsi, na kwamba hajui anaongea Themihill ipi, ni hiyo ya Tabora au Arusha ukizingatia Arusha kuna Themihill.

Katika kupambana na jambo hili amesema alilitolea taarifa kwenye vyombo ya usalama na Vyombo vya usalama walimhakikishia kuwa clip hiyo haina mantiki yoyote na yeye aipuuze na kuachana nayo, nao Vyombo vya usalama walimuahidi kuendelea kuifatilia kubaini muhusika aliyeweka sauti hiyo ya kiswahili.

"Nilipowaambia vyombo vya usalama waliniambia Mambo, clip hiyo haina mantiki yoyote wewe ignore tu maana ukisikiliza kwa makini huyo mtu ni kama anataka kukuchafua tu kwa Tanzania hakuna kitu kama hicho hivyo nisiwe na wasiwasi".

Mambo amesema hafahamu kwa nini mtu huyo kaamua kurekodi clip hiyo, kwa nini kaisambaza na alikuwa na lengo gani, pia amesema yeye hana hakika hata kama kwa Tanzania kuna weza kuwa na bunduki ya aina hiyo, Piaamesema yeye hela ya kununua Bunduki za kuwagawia wanafunzi anazipata wapi iwa hata kalamu wala daftari hajawahi kutoa.

Ameeleza kuwa hata mwananfunzi afaulu kwa kiwango kikubwa sana hajawahi kutoa zawadi ya aina yoyote zaidi ya kumpa punguzo la ada, sasa iweje aanze kugawa bunduki, hivyo amekanusha kuwa taarifa hizo za kwenye clip si za kweli na wala hazihusiani naye wala shuleya Themihill.

Pia ili kujiridhisha zaidi Jamiicheck ilimtafuta Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Richard Abwao ambaye alithibisha kutokuwepo kwa kalamu hizo za bunduki.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Richard Abwao, Kasema kwenye Mkoa wake hakuna tukio Kama hilo la kugawa Bunduki au Silaha.

"Kwenye akili ya Kawaida ni kitu ambacho hakiwezekani. Kama kutakuwepo kalamu yenye Silaha itakuwa na thamani kubwa sana, uwezekano wa kusema inaweza ikasambazwa kwa wanafunzi bure ni Kitu ambacho hakiwezekani". Amesema ACP Abwao

Kulingana na maelezo ya Mkurugenzi w wa Shule ya Themihill na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tabora na uwepo wa video clip hiyo mtandaoni kwa muda mrefu Jamiicheck inathibitisha kuwa clip hiyo iliyowekwa sauti ya kiswahili ni ya uzushi.
Upo serious kabisa ukaja ku post hiki kitu? Aisee, achana na hizo kelele za huyo mwanamke anayeongea, jitahidi usikilize sauti ya huyo jamaa hapo.
Uchambuzi mwingine tuuweke kando japo hata hauhitaji akili timamu
Huyo mama ameshasema shule gani hapo Bongo unataka ushahidi gani mpaka watoto wafe ndipo utakapo amini? Miafrika Bwana Ndivyo ilivyo. Kazi hiyo nimewapa Polisi Waifanyie kazi Sio kazi yangu na wala sio kazi yako kuthibitisha acha kubisha kitu haukijuwi. Jambo usilolijuwa ni kama usiku wa giza tototoro.
 
Kwa akili zako na wewe unaamini kabisa?
Kila kitu kinawezekana Wazungu wanatulazimisha tuwe mashoga SisiWafrika ili tusipate kuzaliana Wazungu wameleta ugonjwa wa korona wakapeleka nchini china ili kupunguza watu duniani itakuwa kutengeneza silaha ya peni kuwa maliza watoto wetu? Kwa Akili yako wewe unafikiri Wazungu wanawapenda Watu weusi?
 
Huyo mama ameshasema shule gani hapo Bongo unataka ushahidi gani mpaka watoto wafe ndipo utakapo amini? Miafrika Bwana Ndivyo ilivyo. Kazi hiyo nimewapa Polisi Waifanyie kazi Sio kazi yangu na wala sio kazi yako kuthibitisha acha kubisha kitu haukijuwi. Jambo usilolijuwa ni kama usiku wa giza tototoro.
Hiyo shule ipo Tabora, huyo mama ni mzushi ameamua kuzua taharuki tu.
Huyo aliyeshika pen ukimsikiliza uongeaji wake, wala hayupo Tanzania.
Kwa akili za kawaida hiyo silaha wewe unaona inaweza ikauzwa kwa bei ya Pen hata zisambazwe mashuleni? Ili iweje?
Huo mlio umeisikia?
 
Huyo mama ameshasema shule gani hapo Bongo unataka ushahidi gani mpaka watoto wafe ndipo utakapo amini? Miafrika Bwana Ndivyo ilivyo. Kazi hiyo nimewapa Polisi Waifanyie kazi Sio kazi yangu na wala sio kazi yako kuthibitisha acha kubisha kitu haukijuwi. Jambo usilolijuwa ni kama usiku wa giza tototoro.
Unaweza kuta Kuna mtoto alichukua ya mzazi au mlezi wake mtu wa kitengo au muhalifu au ya kujilinda mtoto alidhani peni .
Sasa nyie mnakuja kusambaza uzushi.
Kwanza aliye shika ktk video anaonekana siyo mtanzania kwa jinsi anavyo ongea.
Hapa mnaichafua shule tu.
 
😂😂 kwa hiyo pen ya risasi iuzwe 200 ili watoto wauane , halafu kwa faida ya nani sasa ?

Kweli huenda zimetengenezwa lakini sio kwa ajili ya kuuzwa kwa watoto na huenda shule ikafika kwa mazingira ya mtoto kuichukua nyumbani kwa baba bila kujua madhara yake. Kama ambavyo mtoto anaweza kuchukua kisu nyumbani kuja kukatia maembe shuleni ila mzozo ukatokea watoto wakauana.

Ila eti kusambazwa mashuleni hapo msituzuge mnatafuta attention tu kuonekana mpo makini na jamii kumbe ni kwenye kufuatilia vitu visivyo na msingi na kuzua taharuki.
 
Kwa akili zako na wewe unaamini kabisa?
Upo serious kabisa ukaja ku post hiki kitu? Aisee, achana na hizo kelele za huyo mwanamke anayeongea, jitahidi usikilize sauti ya huyo jamaa hapo.
Uchambuzi mwingine tuuweke kando japo hata hauhitaji akili timamu
Swali: Je, Silaha au vifaa vya namna hii vipo au havipo ktk uhalisia?Jibu ni kuwa; Vipo.
Swali la Pili: Je, kwa hapa Tanzania vifaa vya namna hii tayari vimeshaingia au bado?Jibu ni kuwa: Haijulikani bayana kama tayari vimeshaingia au bado.

Lakini yawezekana ni kweli kwamba vifaa vya namna hii tayari vimeshaingia hapa nchini Tanzania. Aidha, hata kama vifaa hivyo tayari vimeshaingia hapa nchini, haviwezi kuuzwa kiholela ktk maduka ya Wafanyabiashara wa kawaida kwa sababu kwa 'nature' ya kifaa chenyewe jinsi kilivyo ni LAZIMA kitakuwa 'classified' kama 'Military Equipment', hivyo hakiwezi kutumika kiholela na watu ambao hawako ktk Mifumo ya kijeshi. This device is designed for Military purposes only, and most probably for the Secret Intelligence Operations, such as "Clandestine Covert Operations' ili kutekeleza 'missions' zao mbalimbali.
 
Unaweza kuta Kuna mtoto alichukua ya mzazi au mlezi wake mtu wa kitengo au muhalifu au ya kujilinda mtoto alidhani peni .
Sasa nyie mnakuja kusambaza uzushi.
Kwanza aliye shika ktk video anaonekana siyo mtanzania kwa jinsi anavyo ongea.
Hapa mnaichafua shule tu.
Wabongo wanapenda haya mastory , eti mchele wa plastic , mara kuna mayai yanatengenezwa huko china ni rahisi sana kuzua taharuki
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom