Lengo la benki wanakulazimisha ukope tena kwao hiyo tabia ni kawaida sanaa kwa benki za bongo, wanakopesha ili wakufilisi kwa kushindwa kulipa sasa hapo wakutegemea kama utamaliza, hati utapewa ila baada ya kuisotea .Juzi rafiki yangu alikuwa ananipa stori kuhusu mama yake. Alichukua mkopo NMB kama miaka 5 iliyopita, akaweka hati ya nyumba yake kama dhamana.
Uyo Mama kahangaika sana hadi akalipa deni lote, AJABU NMB SENGEREMA hawataki kumpa hati yake. Mbona kama nanusa mchezo mchafu? Inakuwaje benki kubwa hivi hawajahifadhi hati ya huyu mteja kwamba akimaliza mkopo wamrudishie mali yake?
Ziadi ya miaka 4 wanamzungusha mama wa watu amejaribu hata kutafuta watu anaojuana nao huko NMB ila nao hawasaidii kitu hebu anayeweza kufikisha taarifa, afikishe.
NMB tawi la SENGEREMA kuna mtu anataka kumpiga huyo Mama nyumba yake. Sio sawa