Nape: Ikiwezekana tuweke kodi kwenye vitochi (Viswaswadu) ili kila Mwananchi amiliki Simu Janja tuendane na teknolojia ya Dunia

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
85,645
145,384
Waziri Nape anasema wanashauriana Serikalini ama kupunguza Kodi Kwenye Simu Janja au kuweka Kodi Kwenye Vitochi (viswaswadu) Ili Watu wote waweze kumiliki Simu Janja.

Huko tunakoelekea teknolojia ya Vitochi itapotea hivyo ni Bora kujihami mapema, amesisitiza Waziri wa Sayansi na Teknolojia mh Nape.

===

“Nadhani tunapoenda tunashawishiana serikalini kuangalia namna aidha ya kutoa kodi kwenye simu janja ili zishuke bei zaidi na ikiwezekana tuweke kodi kwenye vitochi (viswaswadu/ simu ndogo) kwa sababu hivi vitochi huko tunakoenda teknolojia yake itapotea, sasa tunaweza tukajikuta na vitochi vingi vikawa uchafu tu mtaani, kwa sababu Ulaya huwezi kutumia kitochi, haipo tena, sasa wameanza kuvitupa kuja bara la Afrika Kwa hiyo na sisi huku lazima tulinde bara letu, watu waendelee kupata huduma ila taratibu tuvisafishe zipatikane simu za kisasa (simu janja/ simu kubwa), vifaa vya kisasa na kompyuta za kisasa”

Nape Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye amesema hayo leo, Jumatano ya tarehe 15 Mei 2024 wakati akifanya mahojiano katika kipindi cha Good Morning cha Wasafi FM

Source: Jambo TV
 
No no no mwanafunzi wa sheria open University

Yahn internet kuzima hizi siku tatu teyari mitandao ya simu ishamuhonga huyu mropokaji aje afanye comeback ya hasara kwa style hii????

Unataka kila mtanzania awe na simu janja kwa quality ipi ya watoa huduma za mtandao.hawa ambao huna habari unashangaa salio limekatwa umejiunga na huduma za ajabu.....hawa ambao salio la kwako wanakupangia utumie mpaka lini

Viswaswadu haviepukiki smartphones is very destructive kwa watoto.

Punguzeni kodi kwenye mafuta watu wapate ahueni ya maisha kenge nyie.
 
Hayo mabadiriko yaambatane na internet ya satellite vinginevyo ni mkakati wa kunufaisha Tigo, voda,eartel na halotel
 
Waziri Nape anasema wanashauriana Serikalini ama kupunguza Kodi Kwenye Simu Janja au kuweka Kodi Kwenye Vitochi (viswaswadu) Ili Watu wote waweze kumiliki Simu Janja

Huko tunakoelekea teknolojia ya Vitochi itapotea hivyo ni Bora kujihami mapema, amesisitiza Waziri wa Sayansi na Teknolojia mh Nape

Source: Jambo TV
Kishakuwa Waziri wa Sayansi na Teknolojia!
 
Waziri Nape anasema wanashauriana Serikalini ama kupunguza Kodi Kwenye Simu Janja au kuweka Kodi Kwenye Vitochi (viswaswadu) Ili Watu wote waweze kumiliki Simu Janja

Huko tunakoelekea teknolojia ya Vitochi itapotea hivyo ni Bora kujihami mapema, amesisitiza Waziri wa Sayansi na Teknolojia mh Nape

Source: Jambo TV
Starlink anaiogopea Nini Kama kweli anataka tuendane na teknolojia?
 
Back
Top Bottom