Mtaka umesifiwa mbio mpaka umepapita kwenu.

N

Fikiri watanzania wengi na watumishi wa umma wengi ndio wana uelewa mdogo wa kupembua mambo. Hapo mnachokifanya ni mashambulizi binafsi kwa mkuu wa mkoa ambayo hayawezi kamwe kubadiri maisha yenu.

Kikokotoo kimepitoshwa bungeni ambao kila mmoja wenu ana mwakilishi wake uwe ulimchagu au hukumchagua. Kuna vyama vya wafanyakazi pia. Mkiitwa kwenye maandamano na CHADEMA kupaza sauti hamjitokezi mnajidai hamtaki kukosana na mwajiri wenu.

Ni lini vyama vya wafanyakazi vimeitisha maandamao au mgomo kupinga kikokotoo? Kama hawakipendi mbona hawakipingi hadharani? Mnategemea mtu kujificha huku jamii forum na kutukana mtu binafsi?

Ni lini watumishi kwa ummoja wenu mmeingia barabarani kupinga uamuzi wa bunge? Kazi kudandia mada. Wengine wanadhani kikokotoo kimepitoshwa juzi. Kweli tangu 2018 leo hii ndo midhipa inawatoka?

Nani umemsikia akigoma kwenda kazini kisa kikokotoo.

Watanzania wasipoambiwa maneno machungu hawaamki. Ni umbea, majingu na takataka zote.

Mtu kusema ukweli ndo tumshambulie. Na baada ya kumshambulia tumepata nini? Lazima tujitambue hasa watumishi.

Hii inaonyesha dhahiri hata watumishi hawajui kikokotoo kimetoka wapi, kimeletwa na nani na wakitaka kiondoke wafanyeje. Hawa wengine tunawaonea tu.
Mshambulizi haya yangetolewa hadhari kwa aliyeleta kikokotoo. Kwa taarifa yako kikokotoo kabla hakijaletwa bungeni, kinaandaliwa na watumishi walioko kwenye ofisi zinazihusika. Lazima watumishi wajue mbaya wao kwanza.
Jamii forum inatakiwa kuwa na watu wajenga hoja na sio personal attack. Kwa hiyo Mtaka akiwa sio mkuu wa mkoa ndo kikokotoo kimeondoka?
Hapo kwa akili yako onesha huo ukweli aliosema.
 
We jamaa, hivi huoni kuwa huna akili kabisa! Bado unaendelea kujaza upuuzi kwenye uzi! Ume comment inatosha acha tusome na mawazo ya wengine pia.
kwanza kabisa mihemko na maneno yako mbofumbofu ikusaidie wewe mwenyewe, pande hii ni useless kabisa:spandauB:

jambo la pili,
daima siwezi kuchoka wala kunyamazia upotoshaji wa wazi hata kidogo, wala siwezi kuwafurahisha wavivu na walalamikaji kwa uvivu wao :spandauB:
 
kwanza kabisa mihemko na maneno yako mbofumbofu ikusaidie wewe mwenyewe, pande hii ni useless kabisa:spandauB:

jambo la pili,
daima siwezi kuchoka wala kunyamazia upotoshaji wa wazi hata kidogo, wala siwezi kuwafurahisha wavivu na walalamikaji kwa uvivu wao :spandauB:
Nimefuta post yangu hapo juu baada ya kuona post ya member mmoja kuwa unahangaika kujibu watu humu wengine ni zuzu
 
Kipindi ameondolewa Dodoma watu wakalalamika humu, probably wenye maslahi nae, niliandika humu the guy si overrated.

Mtaka ana haiba ya kupendeza, lakini haimaanishi ni kiongozi mzuri, tatizo la waTz huwa wanadhani kiongozi anayefaa ni yule wanaye mpenda "kimahaba". 🗑
binti kiziwi katika ubora wake. Sisi watanzania tumejaa ubinafsi na ushabiki maandazi na pia harufu za udini. Hii inatufanya tusielewe hasa matatizo yetu kama nchi yanasababishwa na nini na tuyaondoe vipi. Huyu Mtaka sijui aliwezaje kuwaghilibu baadhi ya watu wakafikia kusema ni kiongozi mzuri. Mwanzisha thread anasema waliokuwa wanapinga siyo kiongozi mzuri eti ''waliona mbali'' kumbe wala haikuhitaji kuona mbali ili kujua ni wale wale. Inaonekana hilo tamko la Mtaka limegusa maslahi yake ndiyo maana anamgeuka sasa. Ubinafsi huu!
 
#TANZANIA: UMEANZA KAZI MWAKA HUU UNALALAMIKIA KIKOKOTOO, SASA WEWE UNALALAMIKA NINI? MSUBIRI RAIS WAKO - MKATA
"Kuna watu hapa wameanza kazi mwaka huu na wao wanatukana kuhusu kikokotoo ,anastaafu 2070 anatukana leo kikokotoo, sasa unamuuliza kwani wewe unastaafu lini? Leo ana miaka 22, mwalimu"

"Unakuta mtu ana ajira mpya hata miaka miwili hajafikisha anaanza kulalamikia kikokotoo, sasa wewe unamlalamikia nani? Maana muda wako wa kustaafu utakapofika Rais hatakuwa huyu aliyepo sasa, wewe msubiri Rais wako wa miaka hiyo utakayostaafu ndipo ulalamike" - Antony Mtaka, Mkuu wa Mkoa wa Njombe.

NB; Haya ndo mawazo ya RC maarufu?
Hapa Mtaka amepotoka.
Hata hivyo, siyo yeye peke yake, ni fikra za viongozi karibia wote wa serikali na hata jamii kulingana na kiwango cha kustaarabika.
Kila mtu katika taifa ana wajibu wa kupigania haki yake na ya wengine.
Hoja aliyoitoa inashawishi ubinafsi na nia ovu dhidi ya wengine, tena kwa uwazi ambayo husababisha ubutu wa akili.
Hata watoto wadogo wanatakiwa wajue kuna mafao na yanaweza kuwa pungufu au makubwa, kikokotoo kizuri au kibaya, serikali yenye sera nzuri au mbaya,..... ili baadaye wawe raia wenye uwezo wa kujenga taifa lenye mustakabali mwema.
Hatuhitaji kufikiria leo tu. Hao walioajiriwa leo ndiyo watakaofanya maamuzi kesho.
 
Kipindi ameondolewa Dodoma watu wakalalamika humu, probably wenye maslahi nae, niliandika humu the guy si overrated.

Mtaka ana haiba ya kupendeza, lakini haimaanishi ni kiongozi mzuri, tatizo la waTz huwa wanadhani kiongozi anayefaa ni yule wanaye mpenda "kimahaba". 🗑
Huwa yuko overrated sana
 
binti kiziwi katika ubora wake. Sisi watanzania tumejaa ubinafsi na ushabiki maandazi na pia harufu za udini. Hii inatufanya tusielewe hasa matatizo yetu kama nchi yanasababishwa na nini na tuyaondoe vipi. Huyu Mtaka sijui aliwezaje kuwaghilibu baadhi ya watu wakafikia kusema ni kiongozi mzuri. Mwanzisha thread anasema waliokuwa wanapinga siyo kiongozi mzuri eti ''waliona mbali'' kumbe wala haikuhitaji kuona mbali ili kujua ni wale wale. Inaonekana hilo tamko la Mtaka limegusa maslahi yake ndiyo maana anamgeuka sasa. Ubinafsi huu!
Itachukua muda sana kuelewa mambo kwa ufasaha katika jamii yetu, tena na hii new era ya uchawa ndio kabisa we are doomed!
 
Back
Top Bottom