Mambo Manne Muhimu ya kuzingatia kabla ya kuoa au kuolewa

Meneja CoLtd

Member
Mar 6, 2021
58
55
Vijana wengi wamekua wakishindwa kuchagua ni binti yupi anafaa kuolewa, hivyo hivyo wanawake nao wameshindwa kutambua ni mwanaume mwenye vigezo vipi anafaa kukubaliwa kuolewa nae.
Mambo mnne muhimu ya kuzingatia kabla haujafanya maamuzi ni;

1. HOFU YA MUNGU (DINI)
Hiki ni kigezo muhimu sana cha kuzingatia, kwani mume au mke mwenye hofu ya mungu kuna asilimia nyingi atakua mkweli na kukupenda kwa dhati kama mafundisho yanavyotaka

2.CHIMBUKO AU ASILI YAO
Unatakiwa kuchunguza historia au asili ya yule unaetaka kuoa au kuolewa nae.
Wahenga wamesema mtu hawezi kuacha asili yake; ikiwa na maana kama ukoo wao ni wawatu wenye maadili mabaya kuna asilimia kubwa nayeye akawa hivyo au watoto wenu wakawa hivyo
Pia wahenga wamesema malipo hapahapa duniani; hapa unaweza jikuta unapata watoto wenye tabia mbaya wasumbufu ikawa ni kama malipo ya tabia mbaya alizofanya mke/Mme kwa wazazi wake. Au urithi wa tabia mbaya za babu zao.
NB: HAPA TUNAANGALIA ASILI NASIO KABILA

3. TABIA NA UZURI WAKE
Ili usije juta kutamani wanawake au wanaume wengine baada ya ndoa inapaswa uoe au kuolewa na mtu mwenye Tabia na uzuri unaoutaka. Hapa msisitizo ni TABIA maana Uzuri na muonekano hubadilika mda na mda.

4. MALI
Mwisho kabisa tutaangalia mali, duniani hamna anayetaka kuishi maisha magumu yeye wala familia yake, sasa kama akitokea mtu mwenye sifa kuu tatu za juu na ana mali (Mwanamme/Mwanamme) Basi huyo ndo mtu sahihi kwako.
 
Hofu ya Mungu haisaidii chochote.

Kufanya makosa ni kawaida kwa binadamu

Halafu unakuja kuongelewa mali, inaonesha kabisa wewe huna hiyo hofu ya mungu
Alafu jambo la mali utakeusitake lipo na ndomaana tunatoa Mahali ya kuolewa ili kulipa jambo umuhimu. Hapa sijamaanisha wasio na mali wasioe lahasha. Kama anavigezo vyengine anaweza kuoa bila shida.
 
Mawazo mazuri, lakini kuna asilimia nyingi mtu mwenye hofu ya mungu kutofanya upumbavu. (Hili litapingwa nawasio na hofu ya mungu)
Shida ya hizo hofu zenu za miungu, ni za kinafki

Mtu akiwa anaenda kanisani ovyo, ni kijana lakini anaongea kama mzee, ananyoa upara, basi ana 'hofu ya mungu'

Oa/kuolewa nae bila kumchunguza uone
 
Mwanaume awe na uwezo kuzidi mwanamke hiyo ndoa itadumu, ila kama mwanaume penda dezo unataka kuoa kwa fulani kisa pesa ipo, hiyo pesa sio yako, mwanaume tafuta pesa yakoooooo ndo heshima yako.
Basi hapo mwanammke atakua hana hofu ya mungu, maana kumsaidia mmeo ni jambo la kawaida tu. Mtu unayempenda utamlinda kwa gharama yoyote
 
Mwanaume awe na uwezo kuzidi mwanamke hiyo ndoa itadumu, ila kama mwanaume penda dezo unataka kuoa kwa fulani kisa pesa ipo, hiyo pesa sio yako, mwanaume tafuta pesa yakoooooo ndo heshima yako.
Hata sisi wanaume hatutaki kuoa familia masikini, mambo yamegeuka mkuu dunia haitaki watu tegemezi tena, ndio maana hata nyie hamjabweteka, mpo mnatoka na kupambania kombe kama sisi.
 
Hamna kitu hapo vyote ni dynamic kuna watu kariakoo wanatumika uchawi ambao hawakutoka nao kwenye kabila lao, ukoo wala familia zao
 
Hamna kitu hapo vyote ni dynamic kuna watu kariakoo wanatumika uchawi ambao hawakutoka nao kwenye kabila lao, ukoo wala familia zao
Sasa hapo tunazungumzia tabia, kama anatabia mbaya ya kishirikina usioe au kuolewa nae
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom