Kutoka kwenye familia tuliyosomeshwa kwa gharama kubwa kumeniathiri kiuchumi, Kupeleka watoto kayumba ni aibu, Napambana kukwepa aibu

gearbox

JF-Expert Member
Apr 20, 2024
262
760
Chekechea na Primary nimesoma english medium private.

Sekondari Form 1 hadi 6 nimesoma Boarding private, Msosi Pilau kila J5 na J2, Ugali ni nadra sana.

Chuo kikuu sikupata mkopo ila si haba sikuwahi kupata changamoto za kiuchumi.

Rasmi na mimi nikawa baba, nikaanza kuwaza watoto waje kusoma KAYUMBA wakati mimi sijasoma huko ?

Hali yangu ni tofauti na waliowahi kusoma kayumba wao hata wakiwa matajiri wanaweza kusomesha watoto kayumba kwa uhuru, wana uzoefu na hizo shule kwahiyo wanaweza kuwasaidia watoto mawazo na ushauri, sasa mimi sijasoma kayumba wala siyajui mazingira yapoje nitamshauri nini mtoto ?

Natoa mfano mwepesi hata kama umesoma kayumba lakini ulipambaniwa ule milo mitatu, ni kwamba na wewe ukiwa mzazi kuna msukumo unakuingia upambane watoto wale milo mitatu, ukikutana na mzazi aliekulia maisha ya milo miwili nae analisha watoto mara mbili, akikupa ushauri kwamba ulishe watoto mara mbili ni ngumu kumuelewa hata kama watoto wake wana nguvu na afya kuzidi wako.

Ndivyo ilivyo kwa upande wangu, nilipambaniwa ili maisha yangu ya shule yawe mepesi ni ngumu mimi kuwapeleka watoto Kayumba, pia hata wazazi watanichukuliaje ? wamenipambania nisome kwa raha kisha waje kuona wajukuu wanaenda kayumba ?


Kwa sasa nina watoto watatu nawapambania wasije pitia maisha ambayo mimi sikupitia,
  • First yupo form 1 boarding, ada milioni 2 na nusu kwa mwaka
  • wa pili yupo Primary day ada laki 9.
  • Huyu mwengine nae soon anaanza shule hio ya laki 9
  • Sina mpango wa kuongeza mtoto wa ziada labda uchumi ukae sawa

Suala la kufaulu wapo wanafunzi wanaokalia ndoo wanapasua vibaya mno, Kusomesha private kumelenga zaidi kumrahishia mtoto maisha ya shuleni

  • Vyoo visafi kila siku vinasafishwa
  • Chakula kizuri shuleni
  • Mazingira tulivu
  • Usafiri shuleni hadi nyumbani
  • kutumia kiingereza kwenye masomo tangu shule ya msingi
  • Kila mwanafunzi ana kiti na dawati lake
  • Hakuna kujazana darasani
  • kujifunza computer utotoni
  • Library
  • masomo ya kupika, kushona, kuchora, n.k.
  • watoto wengi hutokea familia zinazojali malezi na maadili.
  • wanafunzi wengi hufika elimu ya juu (shule ya msingi 80% niliosoma nao tuna degree, kuna msukumo unaupata usiachwe sana na wenzako kielimu)
  • n.k.

Ninajua zipo shule za bei rahisi mfano kuna shule za serikali za englsh medium, shule za sekondari za jumuia ya wazazi, n.k. kwa research yangu zimetofautiana kidogo na Kayumba.

Kwa sasa nina miaka 36 kiuchumi bado najibana sana hasa kwasababu bado najenga ili nihamie kwangu, imenibidi nitembelea IST ili kupunguza gharama za usafiri, Simu yangu ina miaka mitatu sijabadili, wife nae nashukuru anajua tunayopitia nae kapunguza vizinga
 
Chekechea na Primary nimesoma english medium private

Sekondari Form 1 hadi 6 nimesoma Boarding private, Msosi Pilau kila J5 na J2, Ugali ni nadra sana.

Chuo kikuu sikupata mkopo ila si haba sikuwahi kupata changamoto za kiuchumi.

Nilipokuwa baba uchumi haukuwa vizuri ila nikaanza kuwaza watoto waje kusoma KAYUMBA ??? Kwa maisha niliyopambaniwa niyaishi kupanda magari ya njano, watoto waanze kutembe na vidumu??

Ndipo nilipoanza mapambano ya ziada kuwaandalia watoto future, yote hii ni kukwepa aibu.

Nina watoto watatu napambana mno watoto wasije pitia maisha ambayo mimi sikupitia,

Hivi hata wazazi watanichukuliaje aisee ?? Baba ulisomeshwa kwa raha watoto usomeshe kayumba ??

Hadi sasa

Mtoto moja yupo form 1 ada milioni 2 na nusu

Moja yupo Primary ada laki 9

Huyu mwengine nae soon kwenye shule hio ya laki 9
Inawezekana ukafanikiwa kulitimiza hilo,lisimamie kwa vitendo panapo majaliwa.
 
Fanya kwa uwezo wako.

Kayumba na shule za hela watakutana Vyuo (Vikuu) na zaidi mtaani.

Muhimu hakikisha watoto wako wana interpersonal skills.
English Medium zinamrahishia mtoto maisha ya shule, sio kwamba atafanikiwa kuzidi wanafunzi wote wa Kayumba.

  • Vyoo visafi kila siku vinasafishwa
  • Chakula kizuri shuleni
  • Mazingira tulivu
  • Usafiri shuleni hadi nyumbani
  • kutumia kiingereza kwenye masomo tangu shule ya msingi
  • Kila mwanafunzi ana kiti na dawati lake
  • Hakuna kujazana darasani
  • kujifunza computer utotoni
  • Library
  • masomo ya kupika, kushona, kuchora, n.k.
  • Marafiki wengi hutokea familia zinazojali malezi
  • n.k.
 
English Medium zinamrahishia mtoto maisha ya shule, sio kwamba atafanikiwa kuzidi wa Kayumba, mimi mwenyewe nimesoma huko ila nina maboss waliosoma Kayumba.

  • Vyoo visafi kila siku vinasafishwa
  • Chakula shuleni
  • Usafiri shuleni hadi nyumbani
  • Kujifunza kiingereza (Lugha ya kimataifa)
  • Kila mwnafunzi ana kiti na dawati lake
  • Hakuna kujazana darasani
  • n.k.
Hivyo vyote vinapatikana kayumba kasoro usafiri ambao hata kwa shule za English Medium za kibongo ni yaleyale. Ninafikiri wazazi wengi wanapeleka watoto English Medium kwa sababu ya peer pressure.
 
Back
Top Bottom