DOKEZO Arusha: Kituo kikuu cha Mabasi ya kwenda mikoani chawa kero kwa watumiaji wake, hakilingani na hadhi ya jiji

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Bushmamy

JF-Expert Member
Aug 18, 2019
8,847
15,260
Kituo kikuu cha mabasi ya kwenda mikoani kilichopo jijini Arusha kimekuwa kero kwa watumiaji wake kutokana na adha mbalimbali zinazowakabili abiria pamoja na wanaowasindikiza.

Kituo hicho kikuu cha mabasi kipo hapo tangu uhuru hadi na sasa kitu ambacho hakiendani na hadhi ya leo hii kutokana na changamoto lukuki zilizopo kituoni hapo.

Moja ya changamoto zilizopo kituoni hapo ni usalama mdogo wa abiria na mizigo yao na hii inatokana na Kukosekana kwa uzio Kuzunguka kituo hicho.

Kukosekana kwa huduma muhimu kama vile choo, sehemu ya kujikinga mvua/jua ni moja ya changamoto muhimu inayoikabili kituo hicho.

Makundi ya vibaka, matapeli. Wahuni na madalali wasiokuwa waaminifu wamekuwa wakishinda katika eneo hilo la kituo kutokana na Kukosekana kwa miundombinu rafiki kituoni hapo.

Udogo wa kituo. Haukidhi idadi ya mabasi yaliyopo kulinganisha na hali ya maisha ya sasa ambapo idadi ya wasafiri ni wengi kulinganisha na miaka iliyopita, kituo hicho kwa sasa hakiwezi kukidhi mabasi 20 kwa wakati mmoja.
435d8a915554002841c0b58dce80a34f.jpg
 
Tumsuniri Lema mzalendo wa kweli arejeshewe ubunge uone kama hapatakuwa na ubora. Wasasa wanazipiga Kwa kwenda mbele! Hela za Halmashauri na Mkoa wanakusanya Kona zote lakini!
 
Yani stendi ya Arusha huwa naishangaa sana, wanapitwa hadi na Iringa

Bora hata kue Dar express walau kuna nafuu ila sio pale kati,
 
Yani stendi ya Arusha huwa naishangaa sana, wanapitwa hadi na Iringa

Bora hata kue dar express walau kuna nafuu ila sio pale kati,
Ni aibu, jina kubwa lakini hamna kitu cha maana huko chuga, nilipokuwa nikisikia Arusha nilidhani ni sehemu moja ya kipekee, doh saiv sasa sijui naionaje
 
Kituo kikuu cha mabasi ya kwenda mikoani kilichopo jijini Arusha kimekuwa kero kwa watumiaji wake kutokana na adha mbalimbali zinazowakabili abiria pamoja na wanaowasindikiza.

Kituo hicho kikuu cha mabasi kipo hapo tangu uhuru hadi na sasa kitu ambacho hakiendani na hadhi ya leo hii kutokana na changamoto lukuki zilizopo kituoni hapo.

Moja ya changamoto zilizopo kituoni hapo ni usalama mdogo wa abiria na mizigo yao na hii inatokana na Kukosekana kwa uzio Kuzunguka kituo hicho.

Kukosekana kwa huduma muhimu kama vile choo, sehemu ya kujikinga mvua/jua ni moja ya changamoto muhimu inayoikabili kituo hicho.

Makundi ya vibaka, matapeli. Wahuni na madalali wasiokuwa waaminifu wamekuwa wakishinda katika eneo hilo la kituo kutokana na Kukosekana kwa miundombinu rafiki kituoni hapo.

Udogo wa kituo. Haukidhi idadi ya mabasi yaliyopo kulinganisha na hali ya maisha ya sasa ambapo idadi ya wasafiri ni wengi kulinganisha na miaka iliyopita, kituo hicho kwa sasa hakiwezi kukidhi mabasi 20 kwa wakati mmoja.
435d8a915554002841c0b58dce80a34f.jpg
Tatizo ni serikali ya ccm au nimekosea ndugu zangu, basi wajenge.
 
Back
Top Bottom