Aina sita ya vyakula ambavyo vikichanganywa hugeuka sumu

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,045
9,941

Kifi

Kila binadamu ana kile alichojaaliwa na Mungu. Siku zote anachoamua mmoja kula huenda kikawa sumu kwa mwingine.
Chakula anachokula mtu kinaenda sanjari na hali ya kiafya. Wengine huumwa hadi kusababisha kupoteza uhai na hii ni baada tu ya kupendelea kuchanganya chakula.
Mtu mmoja anaweza kula sawa na kwa urahisi, ila kwa mwingine kikageuka sumu.

Hali hii huchochewa zaidi na matokeo ya baadae pale unaposhindwa kuweka mchanganyiko sahihi na wenye afya zaidi .
Kila aina chakula ina faida zake, ila kinapochanganywa kinaweza kusababisha shida kwa mtu.

Kwa watu ambao wanataka kuchanganya lishe ili kupunguza unene na vichocheo vyake ni vyema kushauriana na wataalamu jinsi ya kupanga lishe bora.
Mtaalam wa lishe wa Nigeria Habiba Haruna ameiambia BBC kuhusu aina sita za chakula ambazo zinaweza kuwa sumu kwa mtu yeyote.

Samaki na Maziwa​

samaki

Samaki na Maziwa ni vyakula vyenye virutubisho lukuki na kuvichanganya katika sehemu moja vinaweza visiwe na uwezo wa kutengeneza virutubisho sahihi na hii inaweza kuleta shida baadaye.

Mwili wa binadamu hauhitaji vyakula vya aina tofauti vyenye kemikali za aina moja kuchanganywa. Huweza kusababisha sumu itakayopelekea mtu kutapika na hata kuharisha.

Maji ya limao na Maziwa​

Maziwa na limao huwa haviwezi kukaa sehemu moja kwani vikichanganywa lazima maziwa yaweze kukatika.

Ikiwa mtu atachanganya maziwa na maji ya limao anaweza kutengenezea sumu, vilevile yanaweza kuleta shida katika moyo.

Karanga na Mafuta ya mzeituni​

ayaba da gyada


Karanga ina umuhimu mkubwa sana katika mwili wa binadamu na hutumika katika sehemu nyingi sana.

Pia karanga ina kiwango kikubwa sana cha protini na wanga, vilevile Karanga ni moja ya virutubisho muhimu katika lishe, haswa kwa wale ambao wanataka kupunguza uzito.

Kwa mafuta ya mzeituni yanamsaada mkubwa pia hasa katika masuala ya tiba kwa baadhi ya magonjwa, lakini mchanganyiko wa mafuta hayo na karanga yanaleta shida ila inashauriwa kutumika pale moja inapokosekana lakini sio kwa pamoja.

Dawa pamoja na sharubati ya limao
limao

Kuchukua dawa na kuchanganya na kitu chenye gesi ina madhara makubwa, wataalamu wanasema kuwa kunywa dawa na soda kama fanta au Coca-Cola inaweza kukusababishia kifo kutokana tu ongezeko kubwa la gesi.

Ameongeza kwa kusema kuwa limao au kinywanji chochote chenye gesi hakipaswi kuchanganywa na dawa ni hatari.

Nyama na mayai mabichi​

mayai

Kuchanganya nyama ambayo haijaungwa na mayai mabichi inaweza kusababishia matatizo katika mwili wa binadamu.

Inaweza kuwa sumu kwa wengine, zingine zinaweza kusababisha kutapika na kuhara kwa sababu haifai kutumika hivyo.

Nyama mbichi inaweza kusababisha athari ikiwa usindikaji wake haufuatwi ili kupunguza kiwango cha virutubishi vilivyomo.

Mtaalamu anasema kuwa mayai mabichi hayana virutubisho kwenye mwili wa binadamu, yakiwa bado kwenye hali hiyo hayapaswi kuliwa mpaka pale yatakapochemshwa au kukaangwa ndio hujenga mwili.

"Mayai mabichi sio ya kuyaamini," Anasema Mtaalamu wa chakula kutoka Nigeria, Habiba Haruna.

Wataalamu wanashauri watu kula kile wanajua kitakuwa na faida na haitawasababishia matatizo yoyote.

Kujaribu kitu kipya kunaweza kuwa na faida kwa wengine lakini pia kunaweza kuwa na madhara.
Kuna aina nyingi sana ya vyakula ambavyo vikichangwanywa vinaweza sababisha madhara.
Mtu anapaswa kuwa mwangalifu katika uchaguzi wa vyakula ni vyema aweke vyeme virutubisho na kuepuka kuvichanganya.
 
Nilisikia (nilipokua dogo) kua, ukichanganya Tango na asali unakufa, hivi ni kweli?

Maana hiyo imani imenitawala mpaka leo.
Na Mimi nangoja jibu toka kwa wataalamu kuhusu hili. Nilishasikia sana na nimetoa tahadhari kwa familia juu ya hili. Tuwasubiri wataalamu.
 
Nikiwa hospital kipindi fulani nesi aliwahi kuniruhusu kunywa dawa kwa soda ya sprite na sikupata shida yoyote
 
Nikiwa hospital kipindi fulani nesi aliwahi kuniruhusu kunywa dawa kwa soda ya sprite na sikupata shida yoyote

Mimi kuna sehemu nilishamsikia nesi akisema walimpa mama mjamzito bia aina ya castle milk stout akapata uchungu na kujifungua,wataalamu wa afya hii imekaa vipi
 
Nina mushkel kidogo kwenye samak na maziw kwasababu huku kwetu watu wanatumia maziw kama nazi kwaiyo wanaweka kwenye mchuz then tunakula na mpk sasa sijakufa au nitakufa baadae?
 
Nina mushkel kidogo kwenye samak na maziw kwasababu huku kwetu watu wanatumia maziw kama nazi kwaiyo wanaweka kwenye mchuz then tunakula na mpk sasa sijakufa au nitakufa baadae?

Mkuu kama utakufa baadaye siyo mbaya kwa sisi sote ni marehemu watarajiwa
 
Na Mimi nangoja jibu toka kwa wataalamu kuhusu hili. Nilishasikia sana na nimetoa tahadhari kwa familia juu ya hili. Tuwasubiri wataalamu.
Bila Hata Kusubiri Wataalam Muu. Mimi ninakula tango na Assli Kila siku kama Moja ya matibabu yangu na sijaona madhara yoyote.
Lakini kama ulivyosema Imani Yako...Subiri Wataalamu wakuhakikishie...!
 
  • Thanks
Reactions: y-n

Similar Discussions

Back
Top Bottom