Hapana hapo Huwa wanamaanisha kuwa sio kwamba umefeli mazima maana yake Ile post husika huwezi kupata kutokana na ufinyu wa nafasi Cha msingi ni kuendelea kuchungulia PDF lolote linaweza kutokea ni ushahidi kuhusu hili
Hamna mkuu ukiona not selected for oral after oral inamaana huwezi kupata post husika kwa sababu wenye vigezo wametimia Cha msingi endelea kufatilia PDF lolote linaweza kutokea kupitia database lakini kama walitangaza na kwingine tena kada the same na yako apo huenda umekosa mazima.
Database ya academician ipo mkuu sema kule watu wanafeli sana hawafikishi 70% ila kwenye miongozo Yao database ya wakufunzi ipo mbona.
NB. Mbona Kuna mtu namfahanu juzi apa kapata tutorial assistant alikosaga mwaka Jana akapotezea kaja kupata mwaka huu.
Mkuu ukitoka kwenye oral unajua kabisa umezingua au?? Kama nafasi ilikua moja huenda upo database although Kuna ushauri mzuri juu hapo kwa Wana jukwaa unaweza kuufuata utakusaidia.
Ukiacha kufundisha panel maana Kuna maswali pia after presentation Yale general question kama ya interview za kawaida. anyway ndo utaratibu wao hatuwezi badilisha kitu
ila 70% sio poa wakuu unatakiwa uwe vizuri kweli kweli kwaiyo ukipata chini ya 70% ndo kwa heri au wataku place kwenye hizi kazi za kawaida ambazo passmark ni 50%
Waliopata insurance officer hao wameula kweli kweli TIRA Kuna asali nzito sana hapo nikitaja salary scale zao hapa tutakimbiana humu Wana mishahara mizuri sana
Mi watu nawashangaa sana wanaoamini sjui status wala nini watu tuna selected for oral tangu mwaka Jana mpaka leo hola hakuna Cha placement ukipiga oral achana na status pambana na pdf tu ndo kila kitu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.