Nauliza kwanini hatuna safari za meli Mtwara to Dar

ndege JOHN

JF-Expert Member
Aug 5, 2015
20,753
48,626
Je, ni wafanyabishara wa mabus wanahujumu? Mbona nchi zilizoendelea huko tunaona usafiri aina zote unaendelea meli, treni na mabus yanapiga kazi vilevile.

Kwanini huku miradi hii inasua sua Kwa mfano mafuriko yaliyoharibu barabara ya Kilwa Lindi huko kupelekea watu kuzunguka njia ya Songea pale kama meli ingekuwepo watu wangeenda Dar Kwa njia ya bahari.

Kwanini meli zinabakia kwenye maziwa tu.
 
TACOSHILI...Tanzania Coastal Shipping Line ni shirika la meli lililokuwa na jukumu la kutoa huduma ya usafiri majini kwenye mwambao wote wa bahari. Ili kufika Mtwara enzi zile za Muasisi ililazimu kuabiri meli za shirika tajwa lakini baadaye hata meli za Zanzibar zilifanya safari za Mtwara.
Mkanganyiko wa ubinafsishaji ndio uliokuja kuua mashirika na makampuni ya umma hadi sasa ambapo uwekezaji mkubwa kama huo hufanywa na wątu binafsi lakini kwa baraka za chama cha zamani.
 
Je, ni wafanyabishara wa mabus wanahujumu? Mbona nchi zilizoendelea huko tunaona usafiri aina zote unaendelea meli, treni na mabus yanapiga kazi vilevile.

Kwanini huku miradi hii inasua sua Kwa mfano mafuriko yaliyoharibu barabara ya Kilwa Lindi huko kupelekea watu kuzunguka njia ya Songea pale kama meli ingekuwepo watu wangeenda Dar Kwa njia ya bahari.

Kwanini meli zinabakia kwenye maziwa tu.
Mbona Dar kwenda Zanzibar zipo safari nadhani hakuna mwamko wa kusafiri kwa meli
 
Je, ni wafanyabishara wa mabus wanahujumu? Mbona nchi zilizoendelea huko tunaona usafiri aina zote unaendelea meli, treni na mabus yanapiga kazi vilevile.

Kwanini huku miradi hii inasua sua Kwa mfano mafuriko yaliyoharibu barabara ya Kilwa Lindi huko kupelekea watu kuzunguka njia ya Songea pale kama meli ingekuwepo watu wangeenda Dar Kwa njia ya bahari.

Kwanini meli zinabakia kwenye maziwa tu.
Hivi,kwa wastani kutoka Dar kwenda Mtwara kwa meli,safari hiyo huchukua muda gani kufika?
 
Zaidi ya masaa 14..kwa zile meli zilizotajwa hapo juu zilikuwa zinatoka Mtwara saa 10 jioni zinafika Dar saa tano asubuhi siku inayofuata.
Halafu kulikuwa na uhuni wakiona vyakula ndani ya meli havijanunuliwa na abiria wataichelewesha hiyo meli ili kuwatia njaa.
Kwa wakati huo kwa vile barabara haikuwa na uhakika ambapo ungeweza kutumia siku tatu hadi wiki moja(wakati wa masika) meli ilionekana nafuu,kwa sasa labda zije meli za mwendo kasi ambazo zitaenda chini ya masaa 6 kwani mabasi yanatumia masaa 8 hadi Mtwara.
Hivi,kwa wastani kutoka Dar kwenda Mtwara kwa meli,safari hiyo huchukua muda gani kufika?
 
Back
Top Bottom