Kuna hawa waheshimiwa wanaotaka kuipeleka Serikali mahakamani kudai kwamba kodi ya magari machakavu ni ya kibaguzi kwa vile iinabagua watu masikini dhidi ya matajiri.
Ukinunua gari lililotumika miaka kumi au zaidi unalipia kodi kama asilimia 20. Ukinunua jipya hulilpi kodi hii. Mimi nawaunga mkono, ila sijui uwezo wa sheria kutusaidia sisi akina yahe.
Ukinunua gari lililotumika miaka kumi au zaidi unalipia kodi kama asilimia 20. Ukinunua jipya hulilpi kodi hii. Mimi nawaunga mkono, ila sijui uwezo wa sheria kutusaidia sisi akina yahe.
Mimi kama Mtanzania nasikitishwa na viongozi wetu wa serikali na watunga sheria kwa ujumla.
Kodi za Magari ambazo Watanzania wengi wanalipa wanapotoa magari nje si za msingi na hazijafikiriwa kitaalamu. Kwa sasa kuna watu wanalipa kodi zaidi ya 50% ya gharama ya gari. Hizi hapa ni faida za gari kuingia Tanzania kwenye uchumi wetu.
1. Mafuta: Gari itaweka mafuta ili kutembea na kwenye mafuta kuna kodi, kunampa biashara gas station ambayo inatoa ajira na kulipa kodi, ujenzi wa gas station unasaidia kampuni za cement kama twiga, magari ya kubeba mafuta yanapata kazi, bank zinapata pesa kutokana na mikopo na biashara na zinaajiri, tanesco inapata pesa za umeme wa kusukuma mafuta n.k.
2. Maisha: Magari yanaraishisha maisha na kufanya shughuli ziweze kufanyika kwa haraka zaidi. Inaongeza "Productivity", magari yanasaidia kwenye maafa, kusafirisha abiria kama taxi, kwenye sehemu za mbali kama vijijini, kufanya biashara kama za utalii, ulizi, kubeba wagojwa.
3. Vipuli: Magari yana kaa zaidi ya miaka kumi kwa muda huo yatanunuliwa vipuli vya utengenezaji, maduka ya vipuli yatalipa kodi na kuajiri, vijana watapata kazi za ufundi, serikali itapata kodi ya uingizaji wa vipuli, viwanda vitatengenezwa n.k hii ni kwenye vipuli tu.
4. Matairi: Magari yanahitaji matairi hivyo maduka ya matairi yatauza na kulipa kodi, vijana watapata kazi kwenye kampuni hizi, mabaki ya matairi yatatumika kwenye shughuli nyingine na serikali itafaidika.
5. Utengenezaji: Kampuni za utengenezaji kama kupiga rangi zinafanya biashara na kulipa kodi, zitaajiri, zitaagiza au kununua rangi na kulipia kodi n.k
Hizi ni faidi chache tu za kuingiza gari. Sasa je serikali ikipunguza kodi na iwe kama nchi nyingine 8%-10% watapata hasara gari ukilinganisha na watu kuacha kabisa kuingiza magari? Kama serikali itaanza kuingiza kodi kwenye magari ya mizigo na magari ya ujenzi itakuwa hasara kubwa kwa nchi.
Tatizo la viongozi wetu ni kwamba wakiona vitu vinaongezeka kidogo wanakimbilia kuweko kodi wakithani kwamba vitu vitaongezeka tu bila kujali athari za uchumi.
Jamani wana JF,
Nimekuwa nafuatilia baadhi kodi zilizopandishwa kwenye bajeti ya serikali mwaka huu. Cha ajabu ni kuwa kodi hizi hasa hili la kwenye magari na umri wa magari ya kuingiza nchini si tu ni kero bali ni kuua ari ya watanzania wanaojiinua kiuchumi na kibiashara. Kitendo hichi ni kinyume kabisa na mwenendo wa serikali yenyewe ambayo EWURA kwa mfano wanapotangaza bei mpya basi makampuni yanapewa grace period zimalize stock iliyopo ndani. Katika hili utangua serikali yetu inawajali matajiri kuliko watanzania walio wengi – maskini wanaotaka kujikomboa.
Fikiria mtanzania aliyeamua kufuata sheria iliyokuwepo kabla ya July inayotaka mtu kuagiza isiyozidi miaka kumi ili asilipishwe dumping fees. Sasa ni watu wengi wameagiza magari yao tena kwa kukopa ili wakaanzishie biashara zao. Kwa bahati mbaya serikali imebadili mwaka wa kuingiza bila dumping fees uwe 8 years. Bila kujali sasa serikali inataka wote ambao gari zao zitaingia baada ya mwezi Julai kulipa dumping fees. Hii ina maana mtu aliyetarajia kulipa labda 1,800,000 kama kodi sasa atalipa karibu million 5 kama kodi tu. Kwa mujibu wa makampuni mbalimbali yanayotoa magari bandarini watu wengine watalipa kodi mpaka kufikia million kumi na sita. Hii ni sawa na kununua gari lingine nzuri tu tena bila ya kodi ya uchakavu.
Cha ajabu watanzania ni kuwa hizi kodi zimeanza kulipishwa wakati hata finance bill haikupitishwa na bunge. Finance bill ilikataliwa bungeni kama sikosei na sasa inategemewa kuwasilishwa mwezi wa nane. Je, wabunge wetu hili mnalionaje? Kwani msiiamuru serikali isilipishe wale wote walionunua magari yao kabla ya mabadiliko ya sheria? Ni wazi kuwa siyo kosa kubadili sheria, lakini siyo kuwalazimisha watu gharama ambazo hawakuyapanga. Huu ni uhuni wa hali juu kabisa wa kuwafanya watanzania maskini waendelee kuwa maskini na kuwaacha wenye fedha waendelee kuifaidi nchi kwani ndo wanaweza kukwepa kodi na kumiliki wanachotaka kumiliki.
Kwa upande mwingine wa kiuchumi, serikali yetu ingepata hela za kutosha kama ingeruhusu watu wengi wakamiliki magari kwani kutokana na matumizi ya mafuta serikali ingekusanya hela nyingi sana. Mfano, kama sikosei, kwa kila lita moja ya petrol serikali inachukua sh 500, sasa piga mahesabu. Ni kiasi gani kinakusanywa sasa hivi na serikali yetu. Ni ngapi ingekusanywa kama tungekuwa na magari mengi?
Ongezea na makato mengine kama vile leseni, road license, etc etc. Yaani mpaka basi tu.
WABUNGE WETU Please amkeni na hili suala mkalishughulikie mapema sana
Habari za jioni wana JF!
Hapa nataka kuzungumzia kidogo bajeti ya 20012/2013 na marekebisho ya kodi ya magari!
Iko hivi:
a) Hakuna excemption kwa wafanyakazi wa serikali,
b) Magari ya mashirika ya dini yatalipiwa kila kitu
c) Magari chakavu yanapigwa penalty less than 8 years not 10 years kama ilivyokuwa
Hii imepitishwa na ile wanaita general budget and imeanza kauwa implemented pale TRA!
Jamani hivi wafanyakazi wa kawaida wa serikali wana benefits gani! manake ilikuwa walau hii ya excemption kwa wale wachache walioweza kuchukua mikopo wananunua magari walau ya biashara ndogondogo sasa excemption imefutwa mfanyakazi gani wa serikali wa kawaida anaweza kununua gari kwa Tanzania! Wabunge chondechonde msiipitishe hii kwenye budget ya wizara ya fedha bila kujali itikadi za kisiasa na bila kujali kuwa ninyi kwa sababu ya uwezo wenu wa kifedha mtaweza kutoa magari yenu! Chonde chonde wabunge wetu sisi walalahoi wa serikali hapa hatutatendewa haki kiukweli!
Magari ya mashirika ya dini hasa vijijini ndo ambulence za wananchi akitokea mgonjwa wananchi wanakimbilia kanisani kuomba msaada wa gari! Leo magari haya yalipiwe kodi mimi naona hii si sawa! Tunawakilisha kero zetu!
Me nafikiri tukubali mzunguko wa shekeli nchi hii ni mdogo there is no equal distribution of money! Watu wachache wanashikilia uchumi wa nchi sasa kama hizi sheria zikupitishwa maana yake mtu wa kawaida hawezi kuingiza gari nchini! Aliye nacho ataongezewa ndipo tunapokwenda!
Mimi sidhani kama kwa kufanya marekebisho haya itasaidia kukuza uchumi wa nchi! Serikali ikusanye kodi kwa wafanyabiashara ukienda kkoo ni maduka mangapi hutoa risiti hana maduka hasa ya wahindi wanakupa bei mbili bidhaa pamoja na risiti ina bei yake na bila ina bei yake! Hivi ninavyoongea kuna watu wameshindwa kutoa magari yao policy imebadilika gafla na watu hawajajiandaa wako frustrated! Ni changamoto ki ukweli!
Haya ni mawazo yangu lakini wabunge mliangalie hili kwa jicho la ziada!
MIONGONI MWA KILIO KIKUBWA KWA BAJETI ILIYOPITISHWA MWAKA JANA ILIKUWA NI KODI KUBWA YA KUTOA MAGARI BANDARINI.
REFER TO THE ATTACHMENT: View attachment 56330
Je bajeti hii itatuangalia walalahoi ili angalau kusiwe na mlolongo wa kodi katika kutoa gari na kulisajiri??