Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,988
ROSTAM, TAFADHALI BWANA!
Na. M. M. Mwanakijiji
Wananishangaza sana wale ambao wametoa kauli za kupongeza uamuzi wa Bw. Rostam Aziz kujiuzulu hasa wale wanaodai amefanya hivyo kwa maslahi ya taifa. Wananishangaza zaidi wanasiasa wa chama tawala na wa upinzani ambao wameweza kudai hadharani kuwa alichokifanya Rostam ni kitendo cha kuigwa. Lakini wanaonishangaza zaidi ni watu wote ambao wamefikia mahali pa kutukuza uamuzi wa Rostam kujiuzulu kana kwamba alifanya hivyo kuitikia wito wa baadhi yetu kumtaka ajiuzulu au alifanya hivyo kwa sababu ya kile kinachoitwa kujivua gamba.
Ninashangaza na wote hao kwa sababu wanaopongeza uamuzi wa Rostam kujiuzulu wanafanya hivyo kama watu ambao hawajachukua muda kusoma hotuba yake. Ni kama watu walio wavivu kusoma, wagumu kuelewa, na wepesi kusahau. Rostam Aziz kujiuzulu kwani ni kwa kubeza; amefanya hivyo kwa sababu nyingine zote isipokuwa ile ya maslahi ya taifa. Simsingizii.
Hotuba yake iliyokuwa na karibu kurasa nane ilikuwa na jumla ya maneno 3067. Kati ya maneno hayo:
Neno Wazee wangu linatokea mara 34;Maneno chama chetu yanatokea mara 13; Neno CCM linatokea mara 16; Maneno Halmashauri Kuu ya Taifa linatokea mara 4
Maneno Kamati Kuu yanatokea mara 6; Neno biashara linatokea mara 6; Neno taifa linatokea mara 8 - Mara 5 kati ya hizo likiwa linahusiana na Halmashauri Kuu ya Taifa au Kamati Kuu ya Taifa (vyombo vya uongozi wa CCM). Mara 1 likimtaja Baba wa Taifa na mara 1 likizungumzia Waasisi wa Taifa letu na sehemu nyingine likiwa kama sehemu ya neno jinginie yaaani kitaifa, kimataifan.k; Neno Tanzania linatokea mara 6. Mara 3 kati ya hizo likitaja watanzania, mara 2 ikitaja nchi ya Tanzania Bara na mara 1 ikihusisha Tanzania na kufanyika kwa siasa chafu; Neno nchi yetu linatokea mara 7 - kati ya hizo mara 1 ni sababu ya yeye kuzungumza na wazee wa Igunga. Mara nyingine 6 ni katika kuendeleza wazo fulani; Neno nchi yangu linaonekana mara 1; Neno Taifa langu linaonekana mara 0; Neno Watanzania wenzangu linaonekana mara 1; Neno wananchi linatokea mara 4 na kati ya hizo hakuna kitu kama wananchi wenzangu na Neno Wazee wetu linatokea mara 1.
Ndugu zangu, hapa ninawauliza wale wenye uwezo wa kufikiria, ni kitu gani kimewafanya waamini kuwa Rostam alijiuzulu au ameachia nafasi zake kwa sababu ya maslahi ya Taifa? Neno lenyewe maslahi linatokea mara moja na tena hapo ni katika kutaja maslahi binafsi ya kikundi fulani cha watu. Kimsingi hakuna sababu ya kiakili ambayo inaweza kutolewa na watu ya kwanini wanaamini kuwa Rostam alijiuzulu kwa sababu ya maslahi ya Taifa.
Nyerere aliwahi kujiuzulu Ubunge kwa sababu ya msingi
Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius K. Nyerere (mgongano na wale ambao wanajaribu kumvua Ubaba wa Taifa unaendelea) aliwahi kujiuzulu Ubunge wake wa kuteuliwa akikataa kuburuzwa na serikali ya Mkoloni wakati tunaelekea Uhuru. Inanishangaza kuwa leo hii watu wanaojiona ni wanasiasa hasa wameshindwa kufuata mfano wa kujiuzulu katika hali ya kupinga serikali inavyofanya mambo. Wengi bila ya shaka wanajua zaidi kuhusu kujiuzulu kwa Nyerere nafasi ya Uwaziri Mkuu na kumuachia Kawawa baada ya Uhuru, wachache wanakumbuka kuwa Nyerere alijiuzulu Bunge kupinga sera na jinsi wakoloni walivyokuwa wakijaribu kumburuza pamoja na jitihada zake zote za kujaribu kufikia muafaka wa aina fulani.
Mwezi Julai 1957 Nyerere aliteuliwa kuwa Mbunge katika Baraza la Kutunga Sheria. Miezi michache kabla ya hapo alipigwa marufuku kuhutubia mikutano ya hadhara na mkoloni. Tarehe 14 Disemba 1957 aliandika barua ya kujiuzulu na siku mbili baadaye alielezea uamuzi wake wa kwanini alijiuzulu katika makala iliyotoka kwenye kijarida Sauti ya TANU. Katika maelezo yake marefu alielezea ni kwanini alikubali kuteuliwa kuingia Bungeni ya kuwa alifanya hivyo akiamini kuwa serikali ilikuwa na malengo ya kweli ya kushughulikia matatizo ya kisasa ya wakati huo. Miezi sita baadaye alijikuta kwamba amekubali kuachilia mambo mbalimbali ya msingi katika bona fide akiamini kwamba serikali nayo itakubali kuachilia madai au kubadilisha hatua zake mbalimbali.
Mwisho wa siku aligundua kuwa serikali haikuwa tayari kubadili mwelekeo katika dhamira safi alijua kuwa asingeweza kuendelea kuwemo ndani ya Bunge ambalo haliko tayari kusikiliza hoja zake na hasa kwenye mambo ya msingi. Aliandika hivi (tafsiri toka Kiingereza yangu) Kama ningeamini kuwa jukumu langu ndani ya baraza lilikuwa kutoa na siyo kuchukua, bado ningejiuzulu. Nimeweza kutoa kila kilichokuwa kwenye uwezo wangu kukitoa na vyote nilivyovitoa vimekataliwa. Niliingia Bungeni nikiwa na roho kidogo ya kutoa na kupokea. Hiyo roho haipo pale. Ningekuwa nawaibia wananchi, na kukiibia chama changu (angalia mfuatano wa wananchi na chama) kama ningeendelea kubakia humo, nikipokea posho na kuhudhuria tafrija kama Mbunge, watu wakiamini kuwa nilikuwa na manufaa fulani, wakati nilikuwa najua siku na manufaa yoyote. Hivyo sikuwa na uchaguzi bali kujiuzulu.
Uamuzi wa Nyerere kujiuzulu uliongozwa na kanuni; kanuni kwamba maslahi ya wananchi yako juu ya maslahi mengine yoyote yale. Leo hii Rostam amejiuzulu kwa sababu kubwa mbili - kama umesoma vizuri hotuba yake au kumsikiliza. Kwanza, ni kwa sababu ya Chama chake na pili ni kwa sababu ya biashara zake. Na kama alivyosema ni kweli basi suala la biashara zake lilikuwa juu zaidi. Rostam anasema Athari kama hizo za kibiashara huingia ndani zaidi kuliko vichwa vya habari vya magazeti vinavyolenga kuchafuana, na athari hizo huwa kubwa zaidi kwa mtu kama mimi kwa sababu tofauti na wengine wengi hapa nchini, mimi ni mfanyabiashara wa kimataifa.
Na anamalizia hoja yake kwa kusema aliamua kujiuzulu kwa dhamira ya dhati ya kuachana na siasa hizi uchwara (gutter politics) na kutumia muda wangu kushughulika na biashara zangu. Kwa ufupi, Rostam hakujiuizulu kwa ajili ya maslahi ya Watanzania - wazo la kusababisha uchaguzi mdogo ambao utasababisha matumizi makubwa ya fedha, kulifanya jimbo la Igunga kutokuwa na mwakilishi wakati wa kipindi cha bajeti haviwezi kamwe kutafsriwa kuwa ni maslahi ya taifa
Kama kweli Rostam aliona kuwa anahitaji kujishughulisha na biashara zake kwanini aliamua kurudisha fomu za kugombea Ubunge? Kwanini alikubali kusimama na Kikwete jukwaani na kuomba kura za wananchi ambao walimrudisha tena Bungeni kwa mara ya nne? Yote haya yanatufanya tubakie na jibu moja tu kwamba Rostam alijiuzulu kwa sababu ya maslahi ya Rostam. Maana kama angekuwa na maslahi mengine yoyote angeyasema au angekwepa kwa sababu maneno juu yake hayakuanza leo na hizo athari za kibiashara hazijaanza sasa.
Lakini jambo la mwisho ambalo binafsi naamini linatudokeza zaidi ni kuwa Rostam hakumwomba radhi mtu yeyote. Alizungumza kama mhanga wa siasa mbaya na chafu. Sote tunajua kuelekea uchaguzi mkuu jinsi vyombo mbalimbali vya habari vikiwemo vyenye kuhusishwa naye vilivyoshiriki katika kuchafua watu mbalimbali. Wengi tunakumbuka kauli zake yeye mwenyewe alipojitokeza na kufanya siasa chafu alipowashambulia wale aliowaita mafisadi nyangumi. Lakini kote huko yeye alikuwa sahihi na hakuona kuwa ni siasa mbaya. Angekuwa na chembe ya uungwana angeliomba radhi taifa kwa sababu sehemu ya uchafu wa siasa zetu leo hii ni matokeo ya moja kwa moja ya yeye Rostam. Hakukiomba chama chake radhi, hakumwomba Rais radhi, hakuliomba Bunge radhi na zaidi sana hakuwaomba radhi wa Tanzania hasa kwa kuwa mshirika wa mambo ambayo yamekuwa misumari ya moto migongoni mwa Watanzania.
Binafsi ninaamini, kuna hatua zaidi za kuchukuliwa:
1. Kwanza ni kuvifunga vyombo vyake vyote vya habari ambavyo vimeshiriki katika kuwachafua watu wengine kama vile ambavyo amefanya yule mfanyabiashara maarufu Rupert Murdoch mmiliki wa vyombo kadhaa vya habari aliyelazimika kufunga gazeti maarufu duniani baada ya kukumbwa na kashfa.
2. Kujipeleka yeye mwenyewe vyombo vya usalama na kuweka ushahidi wa kuhusika kwake na kashfa ya Kagoda na EPA kwa ujumla. Asipofanya hivyo DPP aanzishe uchunguzI mara moja na kama na yeye anajiuma meno basi aruhusu Mwendesha Mashtaka Huru chini ya Sheria ya Uendashaji Mashataka ya 2007 ili kuanzisha uchunguzI wa jumla wa kuhusika kwa Rostam na kashfa mbalimbali. Ni uchunguzI huru tu utakaoweza kumsafisha Rostam na tuhuma zote ili asibakie huko uraiani akiwa amezungukwa na wingu hili la kashfa. Kujiuzulu uongozi tu hakuondoi msururu wa tuhuma dhidi yake. Mtu akijitamba ana sabuni, haina maana kasema msafi.
3. Chama cha Mapinduzi kimvue uanachama chini ya Kanuni za Maadili za CCM na Katiba ya CCM kwa kukisababishia chama kashfa. Kwa kadiri ya kwamba Rostam anaendelea kuwa mwana CCM, Chama cha Mapinduzi hakiwezi kudai kabisa kuwa kimejivua gamba. Watu hawakuwa na tatizo na Rostam kwa sababu alikuwa ni mbunge au mjumbe wa NEC, tatizo lao la msini linatokana na kuwa mwana CCM ambaye ameweza kutumia uwezo wake wa kila namna kushawishi siasa za CCM na hata za kitaifa. Yeye kawavulia gamba hadi mkiani, je NEC na CC wataweza kulimalizia?
Kitu pekee ambacho naweza kumpongeza na kumshukuru Rostam kwa uamuzi wake wa kujiuzulu ni kuwa angalau sasa tumebakiwa na mtu mmoja Bungeni ambaye ana nguvu kuliko mwanasiasa mwingine yeyote nchini na ambaye natumaini naye atafuata mkumbo wa kuachia ngazi na huyo atafanya kweli kwa maslahi ya Taifa. Hapana, siyo Lowassa.
Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com
Na. M. M. Mwanakijiji
Wananishangaza sana wale ambao wametoa kauli za kupongeza uamuzi wa Bw. Rostam Aziz kujiuzulu hasa wale wanaodai amefanya hivyo kwa maslahi ya taifa. Wananishangaza zaidi wanasiasa wa chama tawala na wa upinzani ambao wameweza kudai hadharani kuwa alichokifanya Rostam ni kitendo cha kuigwa. Lakini wanaonishangaza zaidi ni watu wote ambao wamefikia mahali pa kutukuza uamuzi wa Rostam kujiuzulu kana kwamba alifanya hivyo kuitikia wito wa baadhi yetu kumtaka ajiuzulu au alifanya hivyo kwa sababu ya kile kinachoitwa kujivua gamba.
Ninashangaza na wote hao kwa sababu wanaopongeza uamuzi wa Rostam kujiuzulu wanafanya hivyo kama watu ambao hawajachukua muda kusoma hotuba yake. Ni kama watu walio wavivu kusoma, wagumu kuelewa, na wepesi kusahau. Rostam Aziz kujiuzulu kwani ni kwa kubeza; amefanya hivyo kwa sababu nyingine zote isipokuwa ile ya maslahi ya taifa. Simsingizii.
Hotuba yake iliyokuwa na karibu kurasa nane ilikuwa na jumla ya maneno 3067. Kati ya maneno hayo:
Neno Wazee wangu linatokea mara 34;Maneno chama chetu yanatokea mara 13; Neno CCM linatokea mara 16; Maneno Halmashauri Kuu ya Taifa linatokea mara 4
Maneno Kamati Kuu yanatokea mara 6; Neno biashara linatokea mara 6; Neno taifa linatokea mara 8 - Mara 5 kati ya hizo likiwa linahusiana na Halmashauri Kuu ya Taifa au Kamati Kuu ya Taifa (vyombo vya uongozi wa CCM). Mara 1 likimtaja Baba wa Taifa na mara 1 likizungumzia Waasisi wa Taifa letu na sehemu nyingine likiwa kama sehemu ya neno jinginie yaaani kitaifa, kimataifan.k; Neno Tanzania linatokea mara 6. Mara 3 kati ya hizo likitaja watanzania, mara 2 ikitaja nchi ya Tanzania Bara na mara 1 ikihusisha Tanzania na kufanyika kwa siasa chafu; Neno nchi yetu linatokea mara 7 - kati ya hizo mara 1 ni sababu ya yeye kuzungumza na wazee wa Igunga. Mara nyingine 6 ni katika kuendeleza wazo fulani; Neno nchi yangu linaonekana mara 1; Neno Taifa langu linaonekana mara 0; Neno Watanzania wenzangu linaonekana mara 1; Neno wananchi linatokea mara 4 na kati ya hizo hakuna kitu kama wananchi wenzangu na Neno Wazee wetu linatokea mara 1.
Ndugu zangu, hapa ninawauliza wale wenye uwezo wa kufikiria, ni kitu gani kimewafanya waamini kuwa Rostam alijiuzulu au ameachia nafasi zake kwa sababu ya maslahi ya Taifa? Neno lenyewe maslahi linatokea mara moja na tena hapo ni katika kutaja maslahi binafsi ya kikundi fulani cha watu. Kimsingi hakuna sababu ya kiakili ambayo inaweza kutolewa na watu ya kwanini wanaamini kuwa Rostam alijiuzulu kwa sababu ya maslahi ya Taifa.
Nyerere aliwahi kujiuzulu Ubunge kwa sababu ya msingi
Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius K. Nyerere (mgongano na wale ambao wanajaribu kumvua Ubaba wa Taifa unaendelea) aliwahi kujiuzulu Ubunge wake wa kuteuliwa akikataa kuburuzwa na serikali ya Mkoloni wakati tunaelekea Uhuru. Inanishangaza kuwa leo hii watu wanaojiona ni wanasiasa hasa wameshindwa kufuata mfano wa kujiuzulu katika hali ya kupinga serikali inavyofanya mambo. Wengi bila ya shaka wanajua zaidi kuhusu kujiuzulu kwa Nyerere nafasi ya Uwaziri Mkuu na kumuachia Kawawa baada ya Uhuru, wachache wanakumbuka kuwa Nyerere alijiuzulu Bunge kupinga sera na jinsi wakoloni walivyokuwa wakijaribu kumburuza pamoja na jitihada zake zote za kujaribu kufikia muafaka wa aina fulani.
Mwezi Julai 1957 Nyerere aliteuliwa kuwa Mbunge katika Baraza la Kutunga Sheria. Miezi michache kabla ya hapo alipigwa marufuku kuhutubia mikutano ya hadhara na mkoloni. Tarehe 14 Disemba 1957 aliandika barua ya kujiuzulu na siku mbili baadaye alielezea uamuzi wake wa kwanini alijiuzulu katika makala iliyotoka kwenye kijarida Sauti ya TANU. Katika maelezo yake marefu alielezea ni kwanini alikubali kuteuliwa kuingia Bungeni ya kuwa alifanya hivyo akiamini kuwa serikali ilikuwa na malengo ya kweli ya kushughulikia matatizo ya kisasa ya wakati huo. Miezi sita baadaye alijikuta kwamba amekubali kuachilia mambo mbalimbali ya msingi katika bona fide akiamini kwamba serikali nayo itakubali kuachilia madai au kubadilisha hatua zake mbalimbali.
Mwisho wa siku aligundua kuwa serikali haikuwa tayari kubadili mwelekeo katika dhamira safi alijua kuwa asingeweza kuendelea kuwemo ndani ya Bunge ambalo haliko tayari kusikiliza hoja zake na hasa kwenye mambo ya msingi. Aliandika hivi (tafsiri toka Kiingereza yangu) Kama ningeamini kuwa jukumu langu ndani ya baraza lilikuwa kutoa na siyo kuchukua, bado ningejiuzulu. Nimeweza kutoa kila kilichokuwa kwenye uwezo wangu kukitoa na vyote nilivyovitoa vimekataliwa. Niliingia Bungeni nikiwa na roho kidogo ya kutoa na kupokea. Hiyo roho haipo pale. Ningekuwa nawaibia wananchi, na kukiibia chama changu (angalia mfuatano wa wananchi na chama) kama ningeendelea kubakia humo, nikipokea posho na kuhudhuria tafrija kama Mbunge, watu wakiamini kuwa nilikuwa na manufaa fulani, wakati nilikuwa najua siku na manufaa yoyote. Hivyo sikuwa na uchaguzi bali kujiuzulu.
Uamuzi wa Nyerere kujiuzulu uliongozwa na kanuni; kanuni kwamba maslahi ya wananchi yako juu ya maslahi mengine yoyote yale. Leo hii Rostam amejiuzulu kwa sababu kubwa mbili - kama umesoma vizuri hotuba yake au kumsikiliza. Kwanza, ni kwa sababu ya Chama chake na pili ni kwa sababu ya biashara zake. Na kama alivyosema ni kweli basi suala la biashara zake lilikuwa juu zaidi. Rostam anasema Athari kama hizo za kibiashara huingia ndani zaidi kuliko vichwa vya habari vya magazeti vinavyolenga kuchafuana, na athari hizo huwa kubwa zaidi kwa mtu kama mimi kwa sababu tofauti na wengine wengi hapa nchini, mimi ni mfanyabiashara wa kimataifa.
Na anamalizia hoja yake kwa kusema aliamua kujiuzulu kwa dhamira ya dhati ya kuachana na siasa hizi uchwara (gutter politics) na kutumia muda wangu kushughulika na biashara zangu. Kwa ufupi, Rostam hakujiuizulu kwa ajili ya maslahi ya Watanzania - wazo la kusababisha uchaguzi mdogo ambao utasababisha matumizi makubwa ya fedha, kulifanya jimbo la Igunga kutokuwa na mwakilishi wakati wa kipindi cha bajeti haviwezi kamwe kutafsriwa kuwa ni maslahi ya taifa
Kama kweli Rostam aliona kuwa anahitaji kujishughulisha na biashara zake kwanini aliamua kurudisha fomu za kugombea Ubunge? Kwanini alikubali kusimama na Kikwete jukwaani na kuomba kura za wananchi ambao walimrudisha tena Bungeni kwa mara ya nne? Yote haya yanatufanya tubakie na jibu moja tu kwamba Rostam alijiuzulu kwa sababu ya maslahi ya Rostam. Maana kama angekuwa na maslahi mengine yoyote angeyasema au angekwepa kwa sababu maneno juu yake hayakuanza leo na hizo athari za kibiashara hazijaanza sasa.
Lakini jambo la mwisho ambalo binafsi naamini linatudokeza zaidi ni kuwa Rostam hakumwomba radhi mtu yeyote. Alizungumza kama mhanga wa siasa mbaya na chafu. Sote tunajua kuelekea uchaguzi mkuu jinsi vyombo mbalimbali vya habari vikiwemo vyenye kuhusishwa naye vilivyoshiriki katika kuchafua watu mbalimbali. Wengi tunakumbuka kauli zake yeye mwenyewe alipojitokeza na kufanya siasa chafu alipowashambulia wale aliowaita mafisadi nyangumi. Lakini kote huko yeye alikuwa sahihi na hakuona kuwa ni siasa mbaya. Angekuwa na chembe ya uungwana angeliomba radhi taifa kwa sababu sehemu ya uchafu wa siasa zetu leo hii ni matokeo ya moja kwa moja ya yeye Rostam. Hakukiomba chama chake radhi, hakumwomba Rais radhi, hakuliomba Bunge radhi na zaidi sana hakuwaomba radhi wa Tanzania hasa kwa kuwa mshirika wa mambo ambayo yamekuwa misumari ya moto migongoni mwa Watanzania.
Binafsi ninaamini, kuna hatua zaidi za kuchukuliwa:
1. Kwanza ni kuvifunga vyombo vyake vyote vya habari ambavyo vimeshiriki katika kuwachafua watu wengine kama vile ambavyo amefanya yule mfanyabiashara maarufu Rupert Murdoch mmiliki wa vyombo kadhaa vya habari aliyelazimika kufunga gazeti maarufu duniani baada ya kukumbwa na kashfa.
2. Kujipeleka yeye mwenyewe vyombo vya usalama na kuweka ushahidi wa kuhusika kwake na kashfa ya Kagoda na EPA kwa ujumla. Asipofanya hivyo DPP aanzishe uchunguzI mara moja na kama na yeye anajiuma meno basi aruhusu Mwendesha Mashtaka Huru chini ya Sheria ya Uendashaji Mashataka ya 2007 ili kuanzisha uchunguzI wa jumla wa kuhusika kwa Rostam na kashfa mbalimbali. Ni uchunguzI huru tu utakaoweza kumsafisha Rostam na tuhuma zote ili asibakie huko uraiani akiwa amezungukwa na wingu hili la kashfa. Kujiuzulu uongozi tu hakuondoi msururu wa tuhuma dhidi yake. Mtu akijitamba ana sabuni, haina maana kasema msafi.
3. Chama cha Mapinduzi kimvue uanachama chini ya Kanuni za Maadili za CCM na Katiba ya CCM kwa kukisababishia chama kashfa. Kwa kadiri ya kwamba Rostam anaendelea kuwa mwana CCM, Chama cha Mapinduzi hakiwezi kudai kabisa kuwa kimejivua gamba. Watu hawakuwa na tatizo na Rostam kwa sababu alikuwa ni mbunge au mjumbe wa NEC, tatizo lao la msini linatokana na kuwa mwana CCM ambaye ameweza kutumia uwezo wake wa kila namna kushawishi siasa za CCM na hata za kitaifa. Yeye kawavulia gamba hadi mkiani, je NEC na CC wataweza kulimalizia?
Kitu pekee ambacho naweza kumpongeza na kumshukuru Rostam kwa uamuzi wake wa kujiuzulu ni kuwa angalau sasa tumebakiwa na mtu mmoja Bungeni ambaye ana nguvu kuliko mwanasiasa mwingine yeyote nchini na ambaye natumaini naye atafuata mkumbo wa kuachia ngazi na huyo atafanya kweli kwa maslahi ya Taifa. Hapana, siyo Lowassa.
Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com